Zitto Vs Mkulo, Nani Mwongo? IMF yaikalia kooni serikali

josiah2008

Member
May 22, 2010
51
23
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe alisema atamthibitishia bungeni, Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo kuwa Serikali imefilisika.Zitto alisema jana mjini Sumbawanga kuwa wataweka hadharani jinsi Serikali ilivyokopa fedha benki ili Waziri Mkulo aweze kuwajibika kutokana na kauli yake aliyoiita ya kukataa kusema ukweli.

Alisisitiza kwamba serikali haina fedha na kudokeza kuwa taarifa ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ya mapitio ya uchumi ya mwezi Machi mwaka huu, inaonyesha kuwa imeshindwa kukusanya kodi kwa asilimia 15.

"Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Serikali katika makusanyo ya kodi zote imeshindwa kukusanya kodi kwa asilimia 15 isipokuwa ushuru wa forodha. Hivyo haikufikia malengo ya ukusanyaji wa kodi," alisema Zitto.

Kwa mujibu wa Zitto, Machi, mwaka huu Serikali ilikopa fedha katika Benki ya Exim na benki zote za biashara nchini na ilikuwa ikihangaika ili iweze kuwalipa wafanyakazi.

"Mkulo atueleze ni serikali gani duniani inakopa kwenye benki za biashara kwa kuwa kitendo hicho ni hatari sana kwa nchi," alisema na kuongeza:"Bajeti ya mwaka uliopita ilikuwa ni Sh11 trilioni ambayo Serikali ilishindwa kufikia malengo ya Sh 1.6 trilioni kutokana na kushindwa kukusanya kodi kwa asilimia hiyo 15 isipokuwa ushuru wa forodha."
Alimtaka Mkulo kuacha kuwaona wanaosema kwamba serikali haina fedha si wazalendo kwa kuwa wawekezaji hawatakuja nchini, bali atambue kuwa kukosekana kwa fedha si suala la uzalendo.

"Serikali ni kweli haina fedha na hakuna suala la uzalendo katika hili. Tatizo la uwekezaji ambalo analizungumzia, linatokana na sera mbovu za CCM kwa kuwa tangu mwaka 2007, hakuna uwekezaji wowote wa maana uliofanyika hapa nchini," alisema Zitto.

Akiwahutubia wanachama wa Chadema na wananchi wa mji wa Vwawa, Mbozi, mkoani Mbeya hivi karibuni, Zitto alisema Serikali ina hali mbaya kifedha kwa sasa kiasi cha kukopa ili kulipa mishahara ya wafanyakazi.
Alidai kuwa hali hiyo mbaya kifedha kwa serikali imesababisha watumishi wake pamoja na wabunge kutolipwa mishahara hadi Mei 7, 2011.

Alisema Serikali sasa inatafuta fedha za kuwalipa watumishi wake mishahara ya mwezi Aprili.
"Hata sehemu ya posho za wabunge mkutano uliopita, zikiwemo za kugharimia mafuta ya safari za wabunge majimboni bado hazijalipwa kutokana na Serikali kukosa fedha," alidai Zitto.

Alisema kutokana na hali hiyo, Serikali imekwenda kukopa Sh540 bilioni kutoka benki za ndani ili watu wasijue kuwa inakabiliwa na ukata."Serikali haikopi fedha ili ijenge bandari, viwanda au kugharimia miradi ya maendeleo, bali inakopa ili ilipe mishahara ya wafanyakazi," alisema Zitto.
source; mwananchi
 
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe alisema atamthibitishia bungeni, Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo kuwa Serikali imefilisika.Zitto alisema jana mjini Sumbawanga kuwa wataweka hadharani jinsi Serikali ilivyokopa fedha benki ili Waziri Mkulo aweze kuwajibika kutokana na kauli yake aliyoiita ya kukataa kusema ukweli.

Alisisitiza kwamba serikali haina fedha na kudokeza kuwa taarifa ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ya mapitio ya uchumi ya mwezi Machi mwaka huu, inaonyesha kuwa imeshindwa kukusanya kodi kwa asilimia 15.

"Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Serikali katika makusanyo ya kodi zote imeshindwa kukusanya kodi kwa asilimia 15 isipokuwa ushuru wa forodha. Hivyo haikufikia malengo ya ukusanyaji wa kodi," alisema Zitto.

Kwa mujibu wa Zitto, Machi, mwaka huu Serikali ilikopa fedha katika Benki ya Exim na benki zote za biashara nchini na ilikuwa ikihangaika ili iweze kuwalipa wafanyakazi.

"Mkulo atueleze ni serikali gani duniani inakopa kwenye benki za biashara kwa kuwa kitendo hicho ni hatari sana kwa nchi," alisema na kuongeza:"Bajeti ya mwaka uliopita ilikuwa ni Sh11 trilioni ambayo Serikali ilishindwa kufikia malengo ya Sh 1.6 trilioni kutokana na kushindwa kukusanya kodi kwa asilimia hiyo 15 isipokuwa ushuru wa forodha."
Alimtaka Mkulo kuacha kuwaona wanaosema kwamba serikali haina fedha si wazalendo kwa kuwa wawekezaji hawatakuja nchini, bali atambue kuwa kukosekana kwa fedha si suala la uzalendo.

"Serikali ni kweli haina fedha na hakuna suala la uzalendo katika hili. Tatizo la uwekezaji ambalo analizungumzia, linatokana na sera mbovu za CCM kwa kuwa tangu mwaka 2007, hakuna uwekezaji wowote wa maana uliofanyika hapa nchini," alisema Zitto.

Akiwahutubia wanachama wa Chadema na wananchi wa mji wa Vwawa, Mbozi, mkoani Mbeya hivi karibuni, Zitto alisema Serikali ina hali mbaya kifedha kwa sasa kiasi cha kukopa ili kulipa mishahara ya wafanyakazi.
Alidai kuwa hali hiyo mbaya kifedha kwa serikali imesababisha watumishi wake pamoja na wabunge kutolipwa mishahara hadi Mei 7, 2011.

Alisema Serikali sasa inatafuta fedha za kuwalipa watumishi wake mishahara ya mwezi Aprili.
"Hata sehemu ya posho za wabunge mkutano uliopita, zikiwemo za kugharimia mafuta ya safari za wabunge majimboni bado hazijalipwa kutokana na Serikali kukosa fedha," alidai Zitto.

Alisema kutokana na hali hiyo, Serikali imekwenda kukopa Sh540 bilioni kutoka benki za ndani ili watu wasijue kuwa inakabiliwa na ukata."Serikali haikopi fedha ili ijenge bandari, viwanda au kugharimia miradi ya maendeleo, bali inakopa ili ilipe mishahara ya wafanyakazi," alisema Zitto.
source; mwananchi
 
imefika wakati viongozi wetu wawe wasema kweli.Mkulo unashindwaje kuukubali ukweli huu anaoeleza Mhe. Zitto??
 
Mkulo hatasema kitu wala hatajiuzuru atakaa kimyaa yatapita, kwani ameshazoea huwa yanapita anaendelea kupeta. Nani wakumwajibisha Mkulo?
 
ccm wamezoea ubishi wa kijinga...wanalazimisha mambo sana
 
Ndio maana Exim bank imeshindwa kutoa mikopo ya magari kwa wafanyakazi wake waliotuma maombi tangu February! Kumbe benki imeikopesha Serikari! Asante Mh Zitto kwa kutujuza!
 
Tanzania tanzaniaaaaa, ukweli ni kwamba sisi wananchi ndio tumeshindwa kuipeleka nchi yetu kule inakotakiwa kwenda...lets say enough is enough tujue moja!

hawa watu wanapata wapi nguvu za kuudanganya uma na kufanya mambo ya kipuuzi namna hii?

huyu mkulo si ndio alidanganya kwenye budget hadi wafadhili wa EU wakashtukia?
 
IMF yaikalia kooni serikali



*Yaitaka iangalie upya misamaha ya kodi
*yasisitiza ongezeko la kodi katika madini

Na Mnaku Mbani

Source Majira - 11/05/2011

MAOFISA wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) wameitaka serikali kuangalia upya suala la misamaha ya kodi, kuongeza wigo wa malipo ya Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT), pamoja na kuongeza wigo wa kodi katika madini ili kuongeza mapato ambayo nyanazidi kudorora.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mapema wiki hii na IMF, baada ya kumalizika mazungumzo baina ya maofisa wake na wale wa serikali, ushauri huo unalenga katika kuiwezesha serikali ya Tanzania kuongeza wigo wa ukusanyaji wa kodi.

“Wakurugenzi wamependekeza umuhimu wa kuongeza wigo wa kodi, kupunguza misamaha na kuongeza udhibiti wa fedha za umma. Wamependekeza kuongeza wigo wa ulipaji wa VAT na kuongeza wigo wa kodi katika madini,” ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo pia imekemea suala la Tanzania kuendelea kutegemea wafadhiri wa nje katika kuendesha bajeti yake kwani utegemezi unatarajia kukua hadi kufikia asilimia 10 ya pato la ndani la taifa (GDP) kwa mwaka huu.

Hali hii inakuja ikiwa ni siku chache baada ya kuwepo na taarifa kwamba serikali ya Tanzania inakumbwa na ukata mkubwa ambao umesababisha baadhi wa watumishi kuchelewezewa mishahara yao, huku ikiwa imebakia mwezi mmoja tu kumalizika kwa mwaka wa fedha 2010/2011.

Hata hivyo, waziri wa fedha, uchumi na mipango Mustafa Mkulo alikanusha vikali habari hizo juzi na kusema kuwa serikali ina hali nzuri ya kifedha na yote yanayosemwa ni siasa za kujitafutia umaarufu.

“Hali ya upatikanaji wa mapato na matumizi bado ina changamoto zaidi kipindi hiki: makusanyo ya kodi kwa mwaka wa fedha 2010/2011 hayataweza kutimiza malengo ya bajeti kutokana na hali mbaya ha hewa, ukata wa fedha za matumizi ya serikali pamoja na riba za madeni ya nyuma. Kumekuwepo na upunguzaji wa matumizi lakini tunatarajia uthibiti zaidi wa matumizi,” imesema taarifa ya IMF.

“Wakurugenzi wamekubali kwamba mwaka 2011/2012 utakuwa ni hatua moja au nyingine ya serikali ya Tanzania kuboresha uthibiti wa fedha za umma. Tunatambua kwamba bei kubwa ya mafuta, hali ya hewa na upungufu wa misaada utasababisha matatizo katika kugharamia mipango ya bajeti, wameitaka serikali kuendelea kubana matumizi ili yalingane na hali halisi ya mapato.”

Maafisa hao wameiomba serikali kuongeza matumizi katika huduma za kijamii na miundombinu ambayo ina mrejesho mkubwa.

“Wakurugenzi wamesisitiza maofisa wa serikali kukamilisha mkakati wa kuratibu madeni ili kuhakikisha kwamba mikopo yote itakayokopwa inazingatia kupunguza riba,” inasema taarifa hiyo.

Hata hivyo, wakurugenzi hao wa IMF wamesisitiza umuhimu wa serikali kuangalia maendeleo ya mfumuko wa bei kwa kubana masharti ya masoko ya fedha ikiwa ni pamoja na kuangalia tatizo ya kushindwa kurudisha mikopo katika benki kwa baadhi ya wakopaji hasa watu binafsi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo yenye kumbukumbu namba No. 11/53 iliyotolewa Mei 9, 2011, maafisa hao walisema kwamba ukuaji wa uchumi wa nchi kwa mwaka 2011 utashuka hadi kufikia asilimia 6 ikiwa hali ya bei za mafuta, umeme zinaendelea kwa muda mrefu.

“Kwa makadirio yetu ya kipindi cha kati, tunaona kwamba hali ya kiuchumi sio mbaya sana lakini kutakuwepo na changamoto za kisera. Kuongezeka kwa idadi ya watu kutaongeza changamoto katika utoaji wa huduma za kijamii achilia mbali kushuka kwa kodi na misaada,” ilisema taarifa hiyo.

Source; Majira 11/05/2011

My Take:
  1. Yaliyosema na Zitto kuhusu ukata Serikalini ni kweli tupu.
  2. Kelele za CHADEMA kuhusu serikali kuongeza mapato, hasa kwenye madini na kuangalia vyanzo vingine ni kweli tupu.
  3. Kelele za wafanyakazi kuhusu wigo finyu wa mapato serikalini ni hakika na kweli tupu
  4. Mkulo ni mwongo na ni hatari kwa nchi hiii
 
IMF yaikalia kooni serikali



*Yaitaka iangalie upya misamaha ya kodi
*yasisitiza ongezeko la kodi katika madini
Na Mnaku Mbani

Source Majira - 11/05/2011

MAOFISA wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) wameitaka serikali kuangalia upya suala la misamaha ya kodi, kuongeza wigo wa malipo ya Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT), pamoja na kuongeza wigo wa kodi katika madini ili kuongeza mapato ambayo nyanazidi kudorora.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mapema wiki hii na IMF, baada ya kumalizika mazungumzo baina ya maofisa wake na wale wa serikali, ushauri huo unalenga katika kuiwezesha serikali ya Tanzania kuongeza wigo wa ukusanyaji wa kodi.

“Wakurugenzi wamependekeza umuhimu wa kuongeza wigo wa kodi, kupunguza misamaha na kuongeza udhibiti wa fedha za umma. Wamependekeza kuongeza wigo wa ulipaji wa VAT na kuongeza wigo wa kodi katika madini,” ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo pia imekemea suala la Tanzania kuendelea kutegemea wafadhiri wa nje katika kuendesha bajeti yake kwani utegemezi unatarajia kukua hadi kufikia asilimia 10 ya pato la ndani la taifa (GDP) kwa mwaka huu.

Hali hii inakuja ikiwa ni siku chache baada ya kuwepo na taarifa kwamba serikali ya Tanzania inakumbwa na ukata mkubwa ambao umesababisha baadhi wa watumishi kuchelewezewa mishahara yao, huku ikiwa imebakia mwezi mmoja tu kumalizika kwa mwaka wa fedha 2010/2011.

Hata hivyo, waziri wa fedha, uchumi na mipango Mustafa Mkulo alikanusha vikali habari hizo juzi na kusema kuwa serikali ina hali nzuri ya kifedha na yote yanayosemwa ni siasa za kujitafutia umaarufu.

“Hali ya upatikanaji wa mapato na matumizi bado ina changamoto zaidi kipindi hiki: makusanyo ya kodi kwa mwaka wa fedha 2010/2011 hayataweza kutimiza malengo ya bajeti kutokana na hali mbaya ha hewa, ukata wa fedha za matumizi ya serikali pamoja na riba za madeni ya nyuma. Kumekuwepo na upunguzaji wa matumizi lakini tunatarajia uthibiti zaidi wa matumizi,” imesema taarifa ya IMF.

“Wakurugenzi wamekubali kwamba mwaka 2011/2012 utakuwa ni hatua moja au nyingine ya serikali ya Tanzania kuboresha uthibiti wa fedha za umma. Tunatambua kwamba bei kubwa ya mafuta, hali ya hewa na upungufu wa misaada utasababisha matatizo katika kugharamia mipango ya bajeti, wameitaka serikali kuendelea kubana matumizi ili yalingane na hali halisi ya mapato.”

Maafisa hao wameiomba serikali kuongeza matumizi katika huduma za kijamii na miundombinu ambayo ina mrejesho mkubwa.

“Wakurugenzi wamesisitiza maofisa wa serikali kukamilisha mkakati wa kuratibu madeni ili kuhakikisha kwamba mikopo yote itakayokopwa inazingatia kupunguza riba,” inasema taarifa hiyo.

Hata hivyo, wakurugenzi hao wa IMF wamesisitiza umuhimu wa serikali kuangalia maendeleo ya mfumuko wa bei kwa kubana masharti ya masoko ya fedha ikiwa ni pamoja na kuangalia tatizo ya kushindwa kurudisha mikopo katika benki kwa baadhi ya wakopaji hasa watu binafsi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo yenye kumbukumbu namba No. 11/53 iliyotolewa Mei 9, 2011, maafisa hao walisema kwamba ukuaji wa uchumi wa nchi kwa mwaka 2011 utashuka hadi kufikia asilimia 6 ikiwa hali ya bei za mafuta, umeme zinaendelea kwa muda mrefu.

“Kwa makadirio yetu ya kipindi cha kati, tunaona kwamba hali ya kiuchumi sio mbaya sana lakini kutakuwepo na changamoto za kisera. Kuongezeka kwa idadi ya watu kutaongeza changamoto katika utoaji wa huduma za kijamii achilia mbali kushuka kwa kodi na misaada,” ilisema taarifa hiyo.

Source; Majira 11/05/2011


My Take:
  1. Yaliyosema na Zitto kuhusu ukata Serikalini ni kweli tupu.
  2. Kelele za CHADEMA kuhusu serikali kuongeza mapato, hasa kwenye madini na kuangalia vyanzo vingine ni kweli tupu.
  3. Kelele za wafanyakazi kuhusu wigo finyu wa mapato serikalini ni hakika na kweli tupu
  4. Mkulo ni mwongo na ni hatari kwa nchi hiii

tatizo Zitto alitoa kauli yake wakati mawaziri wa mr. kikwete wametoka kwenye semina elekezi walikoagizwa kujibu chochote ambacho kinasemwa kuhusu serekali badala ya kukaa kimya.

kwa hiyo bwana mkulo alikuwa anatekeleza agizo la mkuu wake. suala kama alichosema (mkulo) ni uwongo au ukweli, siyo ishu...ishu ni kujibu mapigo kama alivyoagizwa na mkuu wake.
 
Zitto usibadili mada, ulisema Wabunge hawajalipwa.

Waziri kasema wamelipwa na tarehe katoa.

Sasa unakuja na michongo ya makusanyo ya kodi 15% imepungua blah blah blah

Zitto ulibwatuka uzushi, kwa watu makini credibility yako ina suffer!
 
Zitto usibadili mada, ulisema Wabunge hawajalipwa.

Waziri kasema wamelipwa na tarehe katoa.

Sasa unakuja na michongo ya makusanyo ya kodi 15% imepungua blah blah blah

Zitto ulibwatuka uzushi, kwa watu makini credibility yako ina suffer!

Unajuaje......pengine wamelipwa wachache(wa CCM hasa) na wengine bado....yaani Zitto alipwe halafu aseme hajalipwa yeye hajui gharama ya kaulki yake?
 
Matumizi ya kianasa bila uzalishaji, serikali kuu hadi za mitaa... gavana, manaibu, mawaziri, wabunge wote wanalipwa mishahara utafikiri wako ndani ya Taifa linaloingiza mabilioni ya dollar kwa mwezi katika hazina! Tunapenda mno starehe na kuishi maisha ya "u-Pididdy" hata katika uongozi. Uhayawani wa kupenda maisha ya anasa huku tukitegemea misaada. Tabia imeshamiri, kuanzia Rais wa nchi na sasa hata inaambukizwa kwa watoto.

Tulijua tangu mwaka jana kuwa bajeti ya matumizi katika mwaka huu itabidi serikali ikope, tena ikope kwenye benki binafsi. Chaajabu ni kwamba, ili kukabiliana na tatizo hili, hamna pahala serikali ilipoonekana inadhamiria kubana matumizi. Mikutano, makongamano, mishahara, posho, samani maofsini, n.k. vyote vimeendelea kuwa hivyo hivyo... It's unsustainable, haswa ukizingatia huu uzalishaji wetu wa kutegemea mvua za vuli na uwekezaji wenye kutoa misamaha ya kodi utafikiri wameturoga.

Viongozi wetu pamoja na madigrii na maphd yao wameziba masikio na macho kujionea ya serikali ya Ugiriki na austerity measures zilizokuwa imposed huko na IMF ili kuepusha nchi kufirisika.
 
Back
Top Bottom