Zitto, unatuachaje?

Zitto, unatuachaje?

Manu.

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2014
Posts
689
Reaction score
180
Wazungu wanasema... "Charity begins at home".

Mheshimiwa Zitto Kabwe najua wewe ni maarufu sana nje ya Kigoma Kaskazini. Lakini huku hamna ulichofanya.

-Tunakufa na kipindupindu katika soko la kibirizi.

-Hakuna hospitali hata ya kumzalisha mama wa Kigoma Kaskazini.

-Ukiacha barabara ya Mwandiga-Manyovu barabara zingine hazipitiki jimbo zima.

-Hatuna soko la kuuzia mazao yetu.

-Si kwamba watu wa Kigoma hatuna akili, tunafeli kuwa mkiani kimkoa kila mara. Hali ya Elimu jimboni ni mahututi.

Hakuna High School hata moja.
Sisi bado ni mkoa uliokuwa nyuma kimaendeleo... Mwisho kwa maana ya mkiani.

Mara nyingi umekuwa ukijisifia kwa maendeleo ya majimbo mengine ya mkoa wa Kigoma, mathalan Barabara ya mwandiga-Manyovu ambayo hata hivyo ililenga kuifikia jimbo la manyovu ambalo liko CCM basi tu kwa vile Kigoma Kask ikaangukia njiani...........

Tuoneshe kitu ambacho ni tangible cha kujivunia kwa Kigoma Kaskazini.......

Utupu

UNATUACHAJE??

Sasa huko Kigoma mjini utapaweza?
 
Maswali magumu hayo , anasema alijenga kiwanda cha kubangua kahawa ......
 
Hakuna kiwanda processing ya kahawa. Kigoma
 
Amewaambia wana Kigoma mjini kuwa anataka kuwafanyia mambo matamu kama Kazkazini,kila kitu kamaliza kule,barabara shule,hospitali vyote tiyari.kanukuliwa hivyo alipokuwa anachukua form ya kugombea ubunge Kigoma mjini.
 
mbona anadai kila kitu mlichotaka katimiza na kwamba baada ya kuona uwezo wake wakazi wa kigoma mjini wakiongozwa na serukamba wamemuomba asaidie kigoma mjini kuwa kama dubai .
 
Hilo lina faida gani kigoma kaskazini?
 
amesaidi sisi kuwajua watu wa kigoma ni namna gani...
 
manu

leka tutugite sijui leka nini sio maendeleo.....kuwaanzishia chama cha ACT je....si maendeleo hayo..!
 
Last edited by a moderator:
Zito ni Kiongozi Mkuu wa chama,msimwandikeandike mitandaoni hovyo kama hivi.Mnataka kumuumbua kiongozi mkuu wa chama? Mmetumwa nini? Hamkawii kusema Kiongozi Mkuu au Mhusika Mkuu ni gamba!

Shikeni adabu yenu,hasa wewe mleta mada.Mkicheza tutawa-Digest completely.

Pole sana,Kiongozi Mkuu.Kigoma Kaskazini umeiletea neema.Asiye na macho na ambaye haamini atembelee jimbo hata na bajaj.Barabaara murua!Hospitali zimejaa tele,well equiped.Kawaonjeshe na watu wa mjini utamu.
 
manu

Jamani kwani bado kuna matatizo huko Kigoma Kaskazini? Mbona mwenyewe kasema amesha maliza kazi ya kuleta maendeleo huko na kuwa sasa hakuna shida na kuwa huko mko kwenye maisha bora hivyo sasa anahamia kigoma mjini?

Amejitapa kuwa kuwa huko hakuna umasikini tena kila kitu kiko sawa sasa inakuwaje mnalalamika tena? Acheni awapelekee maendeleo na wenzenu wa Kigoma mjini jamani wanateseka. Mimi aliposema Kigoma Kaskazini hakuna matatizo tena watu wanaogolea katika asali na maziwa nilikuwa najipanga kuhamia huko sasa unanitisha mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom