Zitto: Tutairejesha Meremeta bungeni

Zitto: Tutairejesha Meremeta bungeni

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,803
MJADALA kuhusu hatma ya kampuni ya Meremeta iliyokuwa inamilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) sasa utarejeshwa tena bungeni katika kikao cha Bunge linaloanza Aprili mwaka huu mara baada ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali kukamilisha uhakiki wa hesabu za matumizi ya kampuni hiyo.

Maelekezo ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe, yamethibitisha hivyo.

Meremeta ni moja ya makampuni yaliyotuhumiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa, kwamba yalifanya wizi mkubwa wa fedha za umma lakini Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika Bunge lililopita alizima mjadala juu ya suala hilo akidai kuwa hiyo ilikuwa ni kampuni ya jeshi na kwamba masuala yanayogusa usalama wa nchi hayawezi kujadiliwa hadharani.

Hata hivyo, Pinda alionekana dhahiri kuwa alikuwa akificha ukweli.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Zitto Kabwe (CHADEMA), alisema kamati yake imeitaka ofisi ya Msajili Hazina kuhakikisha inatoa ushirikiano kwa CAG ili kukamilisha utarabu wa kufanya hesabu maalum kwa kampuni hiyo kwa haraka.

Alisema kamati yake ilitoa maagizo kwa CAG kufanya kazi ya ukaguzi lakini kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa katika taarifa yake Msajili Hazina hajatoa ushirikiano wala majibu juu ya hatua hiyo.

Kufuatia hali hiyo kamati hiyo imelazimika kutaka maelezo ya kina kwa nini hesabu hizo hazijakalimika kwa mujibu wa sheria.

“Tunahitaji Bunge la Aprili suala la Meremeta liwe limekwisha na kama serikali haitaki kufanya hivyo kupitia kamati yetu tutawaeleza wananchi nini kinachoendelea, Bunge ni chombo chenye mamlaka ya kuisimamia serikali kwa asilimia mia moja”

“Tunahitaji mgodi wa Buhemba, wapewe Stamico lakini kwa sasa huwezi ukawakabidhi kitu ambacho hakijafanyiwa uhakiki wa hesabu zake …kwa Meremeta serikali ilikuwa ikimiliki hisa asilimia mia moja,” alisema Zitto.

Kampuni ya Meremeta, ambayo inadaiwa haijasajiliwa chini ya Ofisi ya Hazina kama kampuni au shirika, ilichota malipo tata zaidi ya sh bilioni 215 zilizolipwa na Benki Kuu (BOT) kwa Kampuni ya Nedcor Trade Service, baada ya udhamini wa kampuni yenye hisa ya Triennex (PTY) limited ya Afrika Kusini.

Hata hivyo, alisema kamati hiyo inahitaji kufahamu hatma ya uuzwaji wa hisa za kampuni ya Zain kwenda kampuni ya simu ya Airtel.

Alisema kwa mujibu wa maelezo inaonyesha kuwa kuuzwa kwa kampuni hiyo serikali haijanufaika kupata kodi na kuhitaji maelezo ya kina ya Msajili wa Hazina, Kamishna wa TRA.

“Hisa za Zain zimeuzwa lakini hakuna kodi iliyongia serikalini sasa tunahitaji kupata ufafanuzi wa kina juu ya hali hii kwani ili nchi iweze kujiendesha sio kufanya ujanja; kinachotakiwa Airtel ni kulipa kodi tu,” alisema Zitto.

Alisema katika kuhakikisha wanasimamia hilo kamati yake imeazimia siku ya Ijumaa kukutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Ramadhan Kijah, Kamishna Mkuu wa TRA, Hanry Kitilya, na Msajili Hazina.
 
Tuendelee kumuombea kwa mungu kijana wetu zitto arudishe makali yake.
 
simuamin zitto nasikilizia akiweza hili nitarejesha imani kwake
 
Duh? Yaani serikali haijapata kodi ya mapato kwenye mauzo ya Zain na JK ndiye aliyekwenda kuzindua Airtel!? Haya si ndio yale mambo ya kuzindua hotel hapa Ar kumbe fence yake ipo kwenye hifadhi ya barabara? Mr President is acting photogenic by just enjoying to lounch taasis hata za wavunja sheria! My God!? What a President!
 
Tusubiri tuone.. lakini mimi nimeshapoteza imani na Zitto!
 
"Tunahitaji mgodi wa Buhemba wapewe Stamico lakini kwa sasa huwezi ukawakabidhi kitu ambacho hakijafanyiwa uhakiki wa hesabu zake" Eeh! Kwanini Stamico! Je ni jukumu la kamati kuamua ktk hili? Na ni kwa kiasi gani?
 
Tusubiri na kuona hiyo APRIL, muda wa kupeana matumaini umekwisha tunaitaji vitendo.
 
Zitto zubery sina imani na wewe,ilishanitoka kitambo ila namna ulivozungumza nimefurahi sana kama kweli mtafanya hivo na ukakomaa mwanzo mwisho ntarudisha imani kwako. nilikuwa nakukubali lkn ulivoanza ukinyonga flani siku za kati hapa nilikuwa nafaidhaishwa sana. nakuombea ktk hili. go! go! plz
 
simuamini zitto,..nahisi kama kuna mchezo na ccm wanaupanga ili kwenda kuisafisha hiyo kashfa ili aonekane dr slaa alikurupuka kusema kuna ufisadi meremeta,..nahisi mwisho mbaya kwa hili.zitto uh huh sina imani naye,..something fishy is smelling
 
Mmh! Huyu kabwe zito ALIYE BEMENDWA NA NA CCM? siyo rahis kuzaliwa upya, labda kuna ki2 nyumaye, binafsi sina iman naye tena!
 
Kwani huyo si mkwere jamani mlitaka afanye nini na zitto anajikomba kwa mkwere si ulisikia kuwa alimwangukia ili ampe uenyekiti wa hiyo kamati? Hiyo, ni janja ya nyani kula nyama mbichi tu hakuna kitu hapo.
 
Aaah mie sio kijana wangu huyu,period! kama litakua na manufaa kwa taifa basi itakua ni kwa chance au mistake....Haswa haswa Mistake,..yes...bahati mbaya yaani! Kwamba ishu libumbuluke hukoo mara beneficiaries ndo tuwe sie! But if all goes well...Let's wait and see!
Tuendelee kumuombea kwa mungu kijana wetu zitto arudishe makali yake.
 
Zitto achen usanii
ungekuwa nyu kwenye kamati nisngepiga kelele...nyie kaen kimya msitafute umaarufu kama mmeushindwa hottym watu wanataaka ukweli sasa wala atuuitaji tena mkahongane
 
Kama uko sirias na meremeta kamuulize mboma..akupe siri yake@@@na ule kile kiwanja anapoishi mbezi beach
 
meremeta ya nini bana....!

nendeni mkajadili maswala yenye tija kwa maslahi ya taifa kwa ujumla wake!meremeta iliweza kuvuka kigingi kikubwa cha riport ya mwanakijiji MTAWEZA NINYI?

jadilini
-inflations
-namna ya kuboresha viwango vya elimu
-namna ya kuboresha miundo mbinu
-namna ya kuboresha huduma za jamii kama maji,umeme,hospitali n.k
-namna ya kuboresha maisha ya mpiga kura
 
Meremeta?Kama imeibuka safari hii lazima tuwe na dought,nakumbuka Pinda alishawahi kusema kwamba hatakubali meremeta ichunguzwe kwa sababu ni kampuni iliyokuwa inamilikiwa na jeshi
Sasa kitu gani kimebadilika?Kama ni kwa wema twashukuru,lakini tusubiri muda uje
 
Itarudishwa bungeni may be 2015 wakati mama Anna na Pinda wameshaondoka. Napendekeza hiyo irudishwe wa wananchi kuliko kuipeleka kwenye bunge la CCM ambapo ni kama kupoteza muda. Walishasema hiyo haitakaa ijadiliwe au Zitto ameamua kutufurahisha?
 
Back
Top Bottom