GE2025 Zitto: Tukishinda Mahakamani tutapiga jalamba nchi nzima na Tutaitoa CCM Madarakani

GE2025 Zitto: Tukishinda Mahakamani tutapiga jalamba nchi nzima na Tutaitoa CCM Madarakani

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mgombea Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema chama hicho kitafanya kampeni katika kila kona ya nchi endapo Mahakama Kuu itatoa maamuzi yatakayoruhusu Luhaga Mpina kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho

Akizungumza Oktoba 6, 2025 katika mkutano wa kampeni uliofanyika Kata ya Katanga, Jimbo la Kakonko mkoani Kigoma, alipokuwa akimnadi mgombea ubunge wa chama hicho katika jimbo hilo, Olaf Kaboboye, Zitto alisema wapo tayari kuingia barabarani mara tu watakaporuhusiwa na mahakama

“Hata kama itabaki wiki moja ya kampeni, tukiruhusiwa kugombea, tutapiga jaramba kila kona ya nchi hii, tutashinda na kuing’oa CCM madarakani,” alisema Zitto

Aliongeza kuwa endapo chama hicho hakitashinda mahakamani, kitatoa maelekezo kwa wananchi kuhusu namna watakavyopiga kura katika nafasi ya urais

Mnamo Septemba 15, 2025, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johari Hamza, aliwasilisha pingamizi dhidi ya Mgombea Urais wa ACT Wazalendo, Luhaga Mpina, hatua iliyosababisha Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kumtoa kwenye kinyang’anyiro cha urais


 
Zito anashangaza! Wiki tatu atawezaje kuzunguka nchi nzima kama mgombea wa ccm hajaweza kufika nchi nzima pamoja na kuwa na helkopta? Zito acha utani mjuba, labda makao makuu ya mkoa, nako si yote. Wale vikaragosi wa vyama shikizi pamoja na kupewa magari na tume hawajaweza kufika nchi nzima. zito acha urongo
 
Siasa ni akili tuu, unawabeba wajinga wajinga wote kwenda kukupigia kura.
 
Mgombea Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema chama hicho kitafanya kampeni katika kila kona ya nchi endapo Mahakama Kuu itatoa maamuzi yatakayoruhusu Luhaga Mpina kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho

Akizungumza Oktoba 6, 2025 katika mkutano wa kampeni uliofanyika Kata ya Katanga, Jimbo la Kakonko mkoani Kigoma, alipokuwa akimnadi mgombea ubunge wa chama hicho katika jimbo hilo, Olaf Kaboboye, Zitto alisema wapo tayari kuingia barabarani mara tu watakaporuhusiwa na mahakama

“Hata kama itabaki wiki moja ya kampeni, tukiruhusiwa kugombea, tutapiga jaramba kila kona ya nchi hii, tutashinda na kuing’oa CCM madarakani,” alisema Zitto

Aliongeza kuwa endapo chama hicho hakitashinda mahakamani, kitatoa maelekezo kwa wananchi kuhusu namna watakavyopiga kura katika nafasi ya urais

Mnamo Septemba 15, 2025, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johari Hamza, aliwasilisha pingamizi dhidi ya Mgombea Urais wa ACT Wazalendo, Luhaga Mpina, hatua iliyosababisha Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kumtoa kwenye kinyang’anyiro cha urais


Huyo mnafiki bado anaendelea kuwadanganya!

Juzi juzi alisambaza vipeperushi akimpigia kampeni mgombea wa urais wa chana changu tawala, je atavikusanya hivyo vipeperushi au atavikana?

Endeleeni kudanganywa naye wakati yeye kishajihakikishia ubunge.
 
Zito anashangaza! Wiki tatu atawezaje kuzunguka nchi nzima kama mgombea wa ccm hajaweza kufika nchi nzima pamoja na kuwa na helkopta? Zito acha utani mjuba, labda makao makuu ya mkoa, nako si yote. Wale vikaragosi wa vyama shikizi pamoja na kupewa magari na tume hawajaweza kufika nchi nzima. zito acha urongo

..Zitto ni mwendawazimu.

..Ni afadhali Baba Levo ashinde hilo jimbo.
 
“Hata kama itabaki wiki moja ya kampeni, tukiruhusiwa kugombea, tutapiga jaramba kila kona ya nchi hii, tutashinda na kuing’oa CCM madarakani,” alisema Zitto
Hahaha Zitto yupo humu, eti mkuu Zitto haya unayosema yana ukweli au unatupiga fix?
 
Back
Top Bottom