Nilufer
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 9,762
- 14,005
Anapata taabu kuona akina Lissu wanapiga mzigo kumzidi yeye
kwa hiyo kwa maneno mengine unataka kusema kwamba anakijiba cha roho?
Anapata taabu kuona akina Lissu wanapiga mzigo kumzidi yeye
ally kombo brother upo..? umepotea recently shahr ramadhan inakwendaje...?! nakutakia ramadhan maqbool brother..
Zitto una kera sana! Unajiona wewe ndio wewe! Are you parfect? I hate u kwakweli.
Najitahidi kuamini kuw alikuwa akitania. Kama sivyo, angelitangazia bunge..."tl kanambia a, b, c? Kananiudhi haka kamtu
Angalia nulicho"quote"....sio unakurupuka tu utafikiri umelala kwenye michongoma.U QUICK TYPO ERROR it was ZITTO KABWE; LOL -- TOO QUICK TO MAKE A MISTAKE? LOVE JAMII FORUMS!!!
Angalia nulicho"quote"....sio unakurupuka tu utafikiri umelala kwenye michongoma.
lazima umchukie kawashika pabaya wachaga
I don't think it is big issue kuongelea/kujadili utani wa mh Zitto na Lissu as a capital mistake wale wana haki ya kutaniana. Anyway kama kweli Mh. ZITTO una tatizo la madaraka it's time 2 balance and distance yourself from it, Time will tell.
Sidhani kama kuna mwananchi yeyote aliyemtuma mwakilishi wake bungeni akalete utani ambao uko within a time ya kuwakilisha matatizo yao ambao muda wenyewe hata hautoshi
Kwani zito ana ugomvi wa kikabila na wachaga?lazima umchukie kawashika pabaya wachaga
Ndugu naona mmemwelewa vibaya Zittoo hakuwa na maana hiyo mnayoifikiria. Tulia kwanza kabla ya kutoa hisia zako!!Watu kila mara wanajiuliza kwa nini kila siku, kila mara, kila mahala ni Zitto, Zitto, Zitto hadi inatia kichefuchefu
Ukweli ni kwamba ni yeye anapenda iwe hivyo kwa kuwa hajakamilisha kazi aliyotumwa. Mpaka pale itakapokamilika, tutaendelea kusikia vitimbwi na show mbalimbali za huyu kijana.
Akihitimisha mchango wako Bungeni, Zitto kasema, nilipewa mchango na Tundu Rissu lakini mwandiko wake ni mbaya sana kwa hiyo nimeshindwa kuusoma. Tujiulize:
1. Je, kweli kulikuwa na ulazima wa yeye kutamka au kutoa taarifa hiyo Bungeni? Faida yake ni nini maana haiongezi chochote (katika mchango wake) wala hawezi kuwahi nafasi kwamba pengine Rissu akirudi basi akute nafasi aliyo bukiwa na mwenzake.
2. Hata kama ilikuwa lazima aseme, Je, ilikuwa lazima atamke sababu na kuchagua maneno mwandiko mbaya sana?' angalia kuna kivumishi sana kama vile mbaya haingetosha!
Si kwamba Zitto ni mzito wa kuelewa, la hasha, anafanya makusudi akijua kuwa mambo kama haya ya kuwadhalilisha wenzake yanaweza kuleta vurugu ndani ya chama na hivyo kukisambaratisha.
Amenihudhi sana, kama si kweli yanayosemwa juu yake, kwa nini asingekaa tu na kutulia kisha aje amweleze Rissu sababu iliyofanya asiwasilishe ujumbe wake. Au kama kwa hekima yake ambayo inashangaza bado aliona ni lazima kutoa taarifa hiyo ya makabidhiano ambayo Wabunge wengine hawahusiki na wala haiongezi chochote cha maana kwenye hansad ,kwa nini asingesema tu kuwa nilipewa mchango na Mbunge mwenzetu lakini kwa bahati mbaya nimeshindwa kuusoma .
Kweli sasa tunaaamini, kazi ya double agency ni ya kipuuzi sana maana ni ya kutekeleza kile usichoamini na kuamini kile usichotekeleza! Zitto hawezi kuaminika tena katika jamii ya wasema kweli.
ZITTO KABWE hafai CCM,CHADEMA,TLP,NCCR,UDPP,SERIKALINI na popote pale kwani hekima, busara na uwezo wa kupima mambo ni muhimu kwa binadamu yeyote kwani ulimi unauwezo wa kuondoa amani katika jamii yoyote kwa muda mfupi sana.aende zake hukohuko kwa KAGAME.