Sigma
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 5,006
- 1,254
Na hili ndo linakutofautisha na Babu yako Msekwa na wengi wa aina yake. Si wote walioko CCM wanaridhishwa na utendaji wa serikali ya chama chao, na hata namna ya kufikiri inatofautiana.Mimi nadhani ni vema wawakilishi tukawepo hapa ili kupata elimu zaidi ya diplomasia na kusikia maoni na mawazo kutoka kwa watanzania ili tuwawakilishe vizuri bungeni!
Mh. HAK, MD, ukiwa bungeni, kwanza uwe Mtanzania badae uwe mwanaCCM,
Sitegemei daktari na wewe uwe kati ya wale wagonga madawati kwa kila kinacholetwa na serkali.
Sitegemei upondeponde hoja iliyoletwa na serikali ya chama chako mwanzomwisho halaf kabla ya kukaa unasema unaunga MIA KWA MIA kwa sababu tu ni CCM!
Sitegemei kuwa utaziba masikio na kupinga kila hoja itakayotolewa na mbunge asiye wa chama chako bila kujali ina maslahi ya kitaifa au la.
Dr. HA Kigwa, make a name in the HOUSE by serving Tanzania siyo kulinda chama.
Historia haitakukumbuka kwa kupiga meza, na kutamka MIA kwa MIA ila kwa kuweka Tanzania kwanza na kuitetea bila ghiliba.
Mwisho nakupongeza kwa ujasiri wa "kujianika" jamvini.
Alika wengine.