Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA


may be anataka amwachie Nafasi ya kugombea uwenyekiti BENARD SANANE. bkoz we cant know
 
Uvivu wa kusoma na kuelewa. Umesoma hadi mwisho na kuelewa? Acha kukurupuka.

Kama wewe umesoma hadi mwisho umeelewa nini la ziada kwenye hiyo habari?
 
Zitto anajua kuwa Mbowe ni kichwa zas y alijaribu kupima urefu wa bahari kwa miguu but akagundua kwamba Mbowe ashikiki ni mtu mwenye msimamo na hana njaa, sasa anajaribu kupima moto wa slaa ngoja tumwache then atatupa jibu.
Exactly mkuu, walianza kumpima Mbowe wameona maji marefu, sasa mashambulizi yameelekezwa kwa Slaa wanafikiri hicho ni kina kifupi, wanajidanganya. Ndio maana siku hizi waliokuwa mafundi wa kumtukana Mbowe wanamsifia huku wakimponda Slaa kuwa ni wa kuja. Si uliona hata waraka wa Zitto kuwa yeye na Mbowe ndio wameijenga Chadema akimaanisha kina Slaa, Mnyika na wengine ni watu wa kuja?...

Hongera Zitto kwa kuliona hilo...'If you can't fight them join them' achana hawa mamluki wanaotaka kukupoteza.
 
may be anataka amwachie Nafasi ya kugombea uwenyekiti BENARD SANANE. bkoz we cant know
Ben Saanane huyu Masalia ya Zitto yaliyopukutishwa CHADEMA?.........Yaani mtu ambaye hana sifa za kuwa kiongozi kwenye Baraza la vijana atapata wapi sifa za kuwa kiongozi wa chama? hapa ndipo ninapomkumbuka Makamba Sr visisimizi kama hivi alikuwa anaviponda kwa nyundo nzito.
 
Hongera Zitto kwa kuliona hilo...'If you can't fight them join them' achana hawa mamluki wanaotaka kukupoteza.

Mkuu ina maana kwa yeye kuamua kutogombea uongozi wowote Chadema, effectively has joined them? Anadai "Sina interest (nia) na sifikirii kama nitagombea uongozi ndani ya chama katika uchaguzi wa ndani wa Chadema mwaka huu, naona timu iliyopo inatosha na inafaa kuendelea kukiongoza chama."

Lakini si ni mingonini mwa watu walio kwenye timu ilioyopo sasa ambayo anaona inatosha? Kwa hiyo akiondoka, timu itaendelea kutosha? Au tusema role yale kwenye timu ya sasa ni kama haipo to the extent kwamba hata asipogombea tena timu mpya itaendelea kutosheleza?

I mean what exactly does he want to convey?
 
Hivi wewe una akili kwani hayo ni maneno yangu hata husomi source ya habari? mpuuzi kweli kweli.

Mpuuzi ni wewe uliyeleta habari nusunusu, kama unashindwa kufupisha habari ni bora usilete habari kulingana na hisia zako. Hebu karudie kusoma habari yote then ujiangalie mapungufu yako.
 
Zitto kama haya ni maamuzi yako kabisa toka moyoni uko sahihi ni maamuzi yako,ila itafika kipindi Watakutaka ugombee nafasi.kwa hiyo siyokuwa hutaki ila wananchi kwa kukupima wakaamua uchukue kiti fulani jiandae kwa hilo.
 
EMT, ukiangalia kwa mbali unaweza kuona ni timu moja lakini ukichungulia kwa darubini kali si timu moja, ndio maana nikasema hivyo 'if he can't fight them better join them' by doing so he has surrendered the battle he started last 3 or 4 years ago. Lakini vile vile inaweza kuwa ni kwa nia njema tu ya kukijenga chama kiwe kitu kimoja. Nampongeza sana kwa hili.
 
Reactions: EMT
Mpuuzi ni wewe uliyeleta habari nusunusu, kama unashindwa kufupisha habari ni bora usilete habari kulingana na hisia zako. Hebu karudie kusoma habari yote then ujiangalie mapungufu yako.
Mkuu msitoane mapovu bure, hii thread imejirudia mara labda muanzisha thread azipitie hizi thread zote mbili then amuombe mod aziunganishe. easy guys relax......
 
Mpuuzi ni wewe uliyeleta habari nusunusu, kama unashindwa kufupisha habari ni bora usilete habari kulingana na hisia zako. Hebu karudie kusoma habari yote then ujiangalie mapungufu yako.
Ni kitu gani hukukielewa kwenye hii qoutation ya Easyfit.

 
It could be the other way too. Labda hataki tena kugombea ili nae aunde informal timu yake nje ya uongozi ujao?
 
I see!......kwahiyo unamshauri Jakaya Kikwete asigombee uenyekiti wa CCM mwaka huu maana ni kujishusha!!.....no wonder ndio maana ukaripoti kwamba ile meli iliyozama Nungwi imeonekana inaelea, kwa akili hizi hakuna la kushangaza.

Tatizo Matola uandishi wako wa shule za kata haujifichi hata ukitumia ID mia, mnatakuna humu JF mnafanya JF sehemu ya kutolea matusi yenu Mods kuweni makini na hii ID ni muendelezo wa makusudi kuichafua JF kwa Multiple ID's
 
Anatikisa kiberiti ili wajuwe nguvu yake ndani ya chama, lets wait and see.
 
Kama wewe umesoma hadi mwisho umeelewa nini la ziada kwenye hiyo habari?

ETM hebu kuwa realistic hata wewe. Ukisoma post yake ya pili imejieleza vizuri kwa kifupi. Hiyo ndiyo ilistahili kuwa post ya kwanza. Si vizuri kuchukulia mistari miwili kubeba kichwa cha habari. Tuendelee na mjadala.

 
Reactions: EMT
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…