Zitto mwana mpotevu Tumsamehe

Zitto mwana mpotevu Tumsamehe

Status
Not open for further replies.

twijuke

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2011
Posts
547
Reaction score
252
Naomba wahusika Uzi huu usiunganishwe na nyuzi nyingine zinazo husiana na msamaha kuhusu Zitto lengo ni kufikisha ujumbe.

Ndugu zangu wana jukwaa poleni na majukumu.

Nasema tumsamehe, tulikula naye nasema tumsamehe, Tumetoka naye Mbali nasema tumsamehe, Hiki ndo kipimo cha uungwana wetu nasema Tumsamehe, Chondechonde tusiwape faida wabaya wetu nasema tumsamehe, Hii ni kamba anavuta tunavuta matokeo yake itakatika, nasema tumsamehe.


Ndugu yangu Mbowe umemtoa Mbali kijana huyu, mwenyewe pia amesema hivyo mara kadhaa,naomba tumsamehe, nasema 7 mara 70 tumsamehe, chondechonde babangu mzee wangu Dk Slaa nasema ni mwenzetu tumsamehe,tukumbuke wema wake. Tuwaonee huruma watanzania walio jawa tumaini, uungwana ni vitendo nasema tumsamehe Mandela pamoja na kufungwa miaka 27 nakutemewa mate kwenye kikombe chake cha uji, na kila aina ya mabaya yasiyo stahiki kufanyiwa na binadamu lakini aliwasamehe Makaburu tena msamaha wa kweli. nasema Tumuenzi Mzee wetu Mandela kwa kwa kumsamehe Zitto.


Nasema tumsamehe pasipo masharti, pasipo kujali itikadi zetu , neno moja tu nasema tumsamehe, nasema tukimsamehe naamini aweza kuwa kiongozi mwema na muadilifu,mwaminifu na akawa mfano wa kuigwa. Wabaya wetu wanacheka wana furahi a tunavyo vuana nguo mitaani, wanacheka wanasema kimenuka, wabaya wetu sasa wamejazana baa wanakesha huku wakishikana mikono na kutosi wanasema safi sana, chonde tusiwape ushindi wabaya.


Nasali usiku kucha nasema Mungu inusuru Chadema na watanzania, Mh Mbowe tunatambuwa vyema mmewekeza nguvu,mali na kila namna ya kukijenga chama, lakini jambo kubwa nalo ni hili la watanzanini walio wekeza matumaini yao kuwa chadema ndo mkombozi, pia wako watanzania wanao amini kuwa Keki ya Taifa wataila kupitia Chadema, tuwaonee huruma. Asubuhi kunakucha naomba tuite vyombo vya habari tusiseme mengi bali neno moja tu kuwa tumemsamehe mwezetu tena kwa msamaha wa kweli, Watanzania watafurahi wakisikia tumemsamehe Mh Zitto.


Zitto si mwizi, si jambazi, si mkwapuaji,si kibaka nasema tumsamehe,tena pasipo kuhesebu makosa yake wala umri wa makosa yake, ni mwanzetu ni kijana wetu amejikwaa, alilpotea, tumrudishe kundini tena tumwandalie Karamu tule naye tunywe naye tumkumbatie tena hadhara, wabaya wetu waone kuwa tumemsamehe mwenzetu na tunampenda. Mh Tundu Lissu na Mh Myika na wengine wote nasema Tumsamehe kwa moyo wa dhati tuweke masilahi ya taifa mbele.
Hakika watanzania wenye mapenzi mema na Chama hata wasio wanachama watafurahi kusikia au kuona tukimsamehe mwenzetu, yatupasa kuamini kuwa naye ni binadamu anastahiki kusamehewa, katu hatutolaumiwa kwa msamaha huu kwa mwenzetu. Chonde chonde, kazi iliyofanyika kuijenga chadema nikubwa kuliko, ya kutaka kuibomoa inayofanyika sasa.



NB
Namalizia kwa kusema katika kutatua tatizo unaweza kusababisha tatizo lingine likawa kubwa kuliko lile la awali, lakini pia tukumbuke katika nia njema kabisa ya kutenda mema makosa yanaweza kufanyika, tutangulize umakini katika utatuzi wa jambo hili, lakini pia tutangulize umakini ktika ujenzi wa taifa letu.

Mungu ibariki Chadema Mungu ibariki Tanzania
 
Chadema na Mob justice,
Ukipigiwa kelele za mwizi Kariakoo utapigwa hadi ufe hata kama hujaiba. Ndo kinachomkumba zitto, hata akijitetea vipi sauti yake inafunikwa na kelele za mwiziiii-mwiziii-mwiziiii.......
Na mara nyingi vibaka na wezi huwa msitari wa mbele kumsulubu mpigiwa kelele za wizi....
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), amesema kuanzia sasa hataki malumbano na mtu. Kauli ya Zitto, imekuja siku moja baada ya Mahakama Kuu Kanda ya
Dar es Salaam, kupiga marufuku chombo chochote kujadili uanachama wake.
 
Zitto atasamehewaje wakati hahitaji msamaha.ana chotaka yeye ni mapambano na mapambano anayoyataka siyo ya kukijenga chama ni kwa ajili ya kukibomoa chama.
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), amesema kuanzia sasa hataki malumbano na mtu. Kauli ya Zitto, imekuja siku moja baada ya Mahakama Kuu Kanda ya
Dar es Salaam, kupiga marufuku chombo chochote kujadili uanachama wake.

Ushauri wa Pasco umezingatiwa
 
Last edited by a moderator:
Naunga mkono wana CDM tumsamehe kijana wetu Zitto, japo majeraha hayatafutika kirahisi! ashukuriwe Mungu maana kupitia Zitto tumepata kujua adui yetu anawaza nini juu ya CDM.
 
hata big juda iskariote alisamehewa sembuse small iskariote kabwe,tumsamehee.hamtaki tunaanzisha chama chetu kama julius malema.
 
Naomba wahusika Uzi huu usiunganishwe na nyuzi nyingine zinazo husiana na msamaha kuhusu Zitto lengo ni kufikisha ujumbe.

Ndugu zangu wana jukwaa poleni na majukumu.

Nasema tumsamehe, tulikula naye nasema tumsamehe, Tumetoka naye Mbali nasema tumsamehe, Hiki ndo kipimo cha uungwana wetu nasema Tumsamehe, Chondechonde tusiwape faida wabaya wetu nasema tumsamehe, Hii ni kamba anavuta tunavuta matokeo yake itakatika, nasema tumsamehe.


Ndugu yangu Mbowe umemtoa Mbali kijana huyu, mwenyewe pia amesema hivyo mara kadhaa,naomba tumsamehe, nasema 7 mara 70 tumsamehe, chondechonde babangu mzee wangu Dk Slaa nasema ni mwenzetu tumsamehe,tukumbuke wema wake. Tuwaonee huruma watanzania walio jawa tumaini, uungwana ni vitendo nasema tumsamehe Mandela pamoja na kufungwa miaka 27 nakutemewa mate kwenye kikombe chake cha uji, na kila aina ya mabaya yasiyo stahiki kufanyiwa na binadamu lakini aliwasamehe Makaburu tena msamaha wa kweli. nasema Tumuenzi Mzee wetu Mandela kwa kwa kumsamehe Zitto.


Nasema tumsamehe pasipo masharti, pasipo kujali itikadi zetu , neno moja tu nasema tumsamehe, nasema tukimsamehe naamini aweza kuwa kiongozi mwema na muadilifu,mwaminifu na akawa mfano wa kuigwa. Wabaya wetu wanacheka wana furahi a tunavyo vuana nguo mitaani, wanacheka wanasema kimenuka, wabaya wetu sasa wamejazana baa wanakesha huku wakishikana mikono na kutosi wanasema safi sana, chonde tusiwape ushindi wabaya.


Nasali usiku kucha nasema Mungu inusuru Chadema na watanzania, Mh Mbowe tunatambuwa vyema mmewekeza nguvu,mali na kila namna ya kukijenga chama, lakini jambo kubwa nalo ni hili la watanzanini walio wekeza matumaini yao kuwa chadema ndo mkombozi, pia wako watanzania wanao amini kuwa Keki ya Taifa wataila kupitia Chadema, tuwaonee huruma. Asubuhi kunakucha naomba tuite vyombo vya habari tusiseme mengi bali neno moja tu kuwa tumemsamehe mwezetu tena kwa msamaha wa kweli, Watanzania watafurahi wakisikia tumemsamehe Mh Zitto.


Zitto si mwizi, si jambazi, si mkwapuaji,si kibaka nasema tumsamehe,tena pasipo kuhesebu makosa yake wala umri wa makosa yake, ni mwanzetu ni kijana wetu amejikwaa, alilpotea, tumrudishe kundini tena tumwandalie Karamu tule naye tunywe naye tumkumbatie tena hadhara, wabaya wetu waone kuwa tumemsamehe mwenzetu na tunampenda. Mh Tundu Lissu na Mh Myika na wengine wote nasema Tumsamehe kwa moyo wa dhati tuweke masilahi ya taifa mbele.
Hakika watanzania wenye mapenzi mema na Chama hata wasio wanachama watafurahi kusikia au kuona tukimsamehe mwenzetu, yatupasa kuamini kuwa naye ni binadamu anastahiki kusamehewa, katu hatutolaumiwa kwa msamaha huu kwa mwenzetu. Chonde chonde, kazi iliyofanyika kuijenga chadema nikubwa kuliko, ya kutaka kuibomoa inayofanyika sasa.



NB
Namalizia kwa kusema katika kutatua tatizo unaweza kusababisha tatizo lingine likawa kubwa kuliko lile la awali, lakini pia tukumbuke katika nia njema kabisa ya kutenda mema makosa yanaweza kufanyika, tutangulize umakini katika utatuzi wa jambo hili, lakini pia tutangulize umakini ktika ujenzi wa taifa letu.

Mungu ibariki Chadema Mungu ibariki Tanzania
Mkuu Twijuke, anayestahili kusamehewa ni mwenye makosa, Zitto asamehewe kwa kosa gani?. Kwa msiofahamu Chadema ndio yenye makosa kumvua Zitto nyadhifa zake zote kwa taarifa za uzushi na majungu!. Kosa kubwa zaidi ni kufanya maamuzi kinyume cha sheria , taratibu na kanuni, zilizojiwekea wenyewe!. Anachofanya Zitto, ni kupigania haki yake dhidi ya dhulmati na ukiukwaji wa katiba ya Chadema!. Chadema wakilijua kosa lao ndio wanaopaswa kuomba msamaha kwa kumwangukia Zitto , awasamehe, afute kesi na kumrejeshea nyadhifa zake zote!. Kwenye kesi ya msingi Chadema itaaibika tena na kuendelea ku loose credibility ambayo tayari imeishaanza kuipoteza!.

Pasco.
 
mmejitahidi sana kumwombea msamaha ijapo yeye haelewi kama kuna wanaomwombea msamaha na wala yeye hana mpango wa kuomba msamaha,atasamehewa lakini tayari keshavunja katiba na kama ni kumsamehe kwa vile kavunja katiba basi chama kitatakiwa pia kuwasamehe na wengine wote waliofukuzwa uanachama kwa kuvunja katiba,hiyo itakuwa ni zaidi ya kusamehe na itakuwa ina invalidate maana ya katiba ya chama na ntapendekeza chama kisiwe na katiba tena kwani haina tena mamlaka.

Yangu ndo hayo.
 
Najua Pasco huwa ana hoja, lakini kwa hili ameathiriwa na ushabiki tu ndio maana anajaribu kufumbia ukweli.
Najua unajua kuwa ni Zitto ndie aliyekiuka utaratibu na kukimbilia mahakamani kinyume na katiba ya cha chake.
Najua unajua kuwa tuhuma dhidi ya Zitto sio uzushi wala majungu bali ni ukweli mtupu uliothibitishwa.
Najua unajua kuwa Zitto hapiganii haki yeyote bali lengo lake ni kuvuruga chama

Kikubwa zaidi, najua unajua kuwa pingamizi la Zitto limekubaliwa na mahakama sio kwa sababu Zitto ana hoja yeyote ya maana ya kuzuia KK kumjadili, bali kwa sababu eti Peter Kibatala alikosea vigezo vya kisheria vya yeye kuwepo mahakamani kama wakili, hii ni aibu sio tu kwa mahakama, bali hata kwa Zitto mwenyewe kukubaliwa pingamizi kwa kigezo hicho tu. Hii maana yake ni kuwa, wangeangalia hoja za kisheria zilizotolewa, ndugu kabwe angetupwa nje.

Kingine ninachojua kwamba unajua ni kuwa mahakama ina mipaka yake, ni kitu ambacho hakipo na au hakitekelezeki na ni ujuha kudhani kuwa mahakama inaweza kulazimisha chama cha siasa kumpa uanachama au vyeo mtu,

Na mwisho kabisa kwa mleta mada ni kwamba Zitto mwenyewe ndiye amekizuia chama chake kumsamehe, chama kimezuiliwa kumjadili na hivyo huwezi kumsamehe mtu bila kumjadili, na sio hilo tu, Kabwe pia amejifunga mwenyewe na kujizibia fursa mbalimbali zikiwemo za kugombea uongozi na kushiriki katika shughuli za chama.
Alichopigania kufa na kupona na ambacho amefaulu kupata ni posho zake tu za ubunge, Zitto is no more, CHADEMA kitaendelea kuchapa kazi na kinamsahau Zitto.
Mkuu Twijuke, anayestahili kusamehewa ni mwenye makosa, Zitto asamehewe kwa kosa gani?. Kwa msiofahamu Chadema ndio yenye makosa kumvua Zitto nyadhifa zake zote kwa taarifa za uzushi na majungu!. Kosa kubwa zaidi ni kufanya maamuzi kinyume cha sheria , taratibu na kanuni, zilizojiwekea wenyewe!. Anachofanya Zitto, ni kupigania haki yake dhidi ya dhulmati na ukiukwaji wa katiba ya Chadema!. Chadema wakilijua kosa lao ndio wanaopaswa kuomba msamaha kwa kumwangukia Zitto , awasamehe, afute kesi na kumrejeshea nyadhifa zake zote!. Kwenye kesi ya msingi Chadema itaaibika tena na kuendelea ku loose credibility ambayo tayari imeishaanza kuipoteza!.

Pasco.
 
Hizi hoja zinakuja baada ya kuona vumbi linalotimka... sasa CDM wanaanza kukiri kuwa Zito si wa kudharau zinaanza hoja za kumsamehe mbona haikuwa hivyo kwa waliopita?
 
Niko tayari kuweka dau la uhai wangu haiwezekani kumsamehe kirahisi namna hii itaonyesha dhahiri zitto alionewa na uongozi wote wa Chadema hauna sifa ya kuwepo madarakani na katiba ya chama na maamuzi yake yawe batili kitu kisichowezekana
 
Where is Malema now?,
An individual can not beat an organisation.

the idea of ECONOMIC FREEDOM FIGHTER had never appear in tanzania politics,ni wazi tunaitaji mtu mfano wa malema.KAFULILA,HAMMAD,ZITTO ni wanasiasa waoga kheri ya MPENDAZOE naweza kumuita mwanasiasa SHUJAA na JASIRI.
 
Niko tayari kuweka dau la uhai wangu haiwezekani kumsamehe kirahisi namna hii itaonyesha dhahiri zitto alionewa na uongozi wote wa Chadema hauna sifa ya kuwepo madarakani na katiba ya chama na maamuzi yake yawe batili kitu kisichowezekana

kuweka dau la uhai sababu ya siasa(mchezo mchafu)!!badilika
 
Mkuu Twijuke, anayestahili kusamehewa ni mwenye makosa, Zitto asamehewe kwa kosa gani?. Kwa msiofahamu Chadema ndio yenye makosa kumvua Zitto nyadhifa zake zote kwa taarifa za uzushi na majungu!. Kosa kubwa zaidi ni kufanya maamuzi kinyume cha sheria , taratibu na kanuni, zilizojiwekea wenyewe!. Anachofanya Zitto, ni kupigania haki yake dhidi ya dhulmati na ukiukwaji wa katiba ya Chadema!. Chadema wakilijua kosa lao ndio wanaopaswa kuomba msamaha kwa kumwangukia Zitto , awasamehe, afute kesi na kumrejeshea nyadhifa zake zote!. Kwenye kesi ya msingi Chadema itaaibika tena na kuendelea ku loose credibility ambayo tayari imeishaanza kuipoteza!.

Pasco.

mkuu pasco thibitisha kuwa zito kazushiwa mambo yote yaliyosemwa kayafanya.
zito ameshinda na ataendelea kushinda kwa sababu tu anasaidiwa na wale aliokuwa anawafanyia kazi.
mimi sioni sababu ya kumsamehe zito kirahisi namna hiyo.
na haiwezekani viongozi wote wa chadema wakawa mbumbumbu kuhangaika na habari za uzushi na majungu. naamini viongozi wa chadema ni makini kabla ya kuyaweka hadharani walijiridhisha kuwa makosa ya zito ni halisi.
zito zuberi kable asisamehewe hata kama ataondoka na wanachama nusu na robo sawa tu kuliko kuendelea kukaa chamani na kukiua taratibu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom