Seif al Islam
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 2,156
- 640
Taarifa zilizopo hapo makao makuu ya cuf maeneo ya buguruni na kuthibitishwa na baadhi ya watu walio karibu na uongozi wa juu wa cuf ni kuwa mbunge wa kigoma kaskazini kupitia chadema bw. zitto kabwe anajiandaa kuhamia cuf na kugombea ubunge wa moja ya majimbo ya mkoa wa mtwara.
Taarifa hizi zinakuja kipindi am,bacho jitihada za zitto mwenyewe na wapambe wake walioko nje na ndani ya chadema kutaka kumpatanisha zitto na mbowe zikiwa zimegonga mwamba hasa baada ya zitto kujikoroga kwa kutoa masharti ya yeye kurudishwa chadema.
Hatua hii ya zitto inachangiwa na kile kinachoitwa kushindwa kwa harakati za chama cha act kujipenyeza katika siasa za mkoa wa kigoma hasa jimbo la kigoma kaskazini ambalo zitto alipanga kugombea ubunge kupitia tiketi ya act.matokeo mazuri ya act katika uchaguzi wa serikali za mitaa ndicho kiliwekwa kama kigezo cha zitto kuhamia act na kugombea ubunge wa kigoma kaskazini.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, kwa kuzingatia kuwa cuf ni sehemu ya ukawa, prof. lipumba tayari alishawasiliana na mwenyekiti wa chadema mh. mbowe na kumweleza jambo hilo ambapo mh. mbowe japo alionyesha awali kutoliunga mkono kwa kuzingatia uzito wa hujuma na tuhuma dhidi ya zitto lakini prof.lipumba alimuhakikishia kuwa anammudu zitto na kuwa jambo hilo lisingeharibu wala kuyumbisha mipango ya ukawa kuelekea 2015.Mkutano wa hivi majuzi uliohutubiwa na lipumba na zitto huko mtwara ni mwanzo tuu wa mpango kamambe wa "kumuandalia zitto makao" huko mtwara.
NAWASILISHA.
Taarifa hizi zinakuja kipindi am,bacho jitihada za zitto mwenyewe na wapambe wake walioko nje na ndani ya chadema kutaka kumpatanisha zitto na mbowe zikiwa zimegonga mwamba hasa baada ya zitto kujikoroga kwa kutoa masharti ya yeye kurudishwa chadema.
Hatua hii ya zitto inachangiwa na kile kinachoitwa kushindwa kwa harakati za chama cha act kujipenyeza katika siasa za mkoa wa kigoma hasa jimbo la kigoma kaskazini ambalo zitto alipanga kugombea ubunge kupitia tiketi ya act.matokeo mazuri ya act katika uchaguzi wa serikali za mitaa ndicho kiliwekwa kama kigezo cha zitto kuhamia act na kugombea ubunge wa kigoma kaskazini.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, kwa kuzingatia kuwa cuf ni sehemu ya ukawa, prof. lipumba tayari alishawasiliana na mwenyekiti wa chadema mh. mbowe na kumweleza jambo hilo ambapo mh. mbowe japo alionyesha awali kutoliunga mkono kwa kuzingatia uzito wa hujuma na tuhuma dhidi ya zitto lakini prof.lipumba alimuhakikishia kuwa anammudu zitto na kuwa jambo hilo lisingeharibu wala kuyumbisha mipango ya ukawa kuelekea 2015.Mkutano wa hivi majuzi uliohutubiwa na lipumba na zitto huko mtwara ni mwanzo tuu wa mpango kamambe wa "kumuandalia zitto makao" huko mtwara.
NAWASILISHA.