Zitto Kabwe tena katika issue ya ndege ya Boeing

Sasa kama na hawa wameanza mambo haya hatuna wa kumuamini ndani ya ccm
Acha siasa nyepesi, serikali imeshakuhakikishia ndege yetu si miongoni mwa "terrible teen", wewe unaendelea tu neno la Mange na Zitto, muda utawaumbua tu.
 


Hata rada mlitetea hivihivi
 
Haka ka zitto si ndo kalisema eti zile bombardier nilikuwa bajaji lakini baadae akaumbuka mana zunapiga mzigo na yeye anazipanda sana tu. Watanzania msidanganyike na haka ka chizi
 
Acha siasa nyepesi, serikali imeshakuhakikishia ndege yetu si miongoni mwa "terrible teen", wewe unaendelea tu neno la Mange na Zitto, muda utawaumbua tu.
Siasa nyepes zp mkuu hilo suala lipo usubir ni muda tu utaongea
 
Nafikiri tunamiss point. Kwanza tungehoji ununuzi wa ndege moja tu ya aina hiyo. Ikiwa kweli biashara itachanganya na ATCL ikapata wateja wa kujaza ndege hiyo kwa route anayoisema Mh Rais (route ya Marekani hadi Kilimanjaro), je kukitokea tatizo watatumia ndege gani kuhudumia njia hiyo? Kumbuka pia kuwa ndege zina matengenezo yake kwa mujibu wa ratiba ya matengenezo na mengine uchukua hadi zaidi ya wiki mbili. Je kipindi hicho watatumia ndege gani. Hii ni moja ya sababu nyingi ya mashirika ya ndege kuanguka. Unajitanua au kuanzisha njia ambazo huwezi kuzihudumia kwa wakati wote (sustainably). Natumaini Mdhibiti (TCAA) watawashauri vyema kabla ya kujiingiza kwenye route. Ndiyo maana kuna kanuni ambayo inaonyesha kuwa ikiwa huduma unazozitoa kwa safari zinahitaji ndege 2 wanatakiwa wawe na ndege 3 kutoa huduma hiyo kwa uendelevu (yaani mara 1.5).

Natumai pia kuwa kuanzisha njia na safari za Marekani, ATCL watafanya uchambuzi yakinifu kwa makini kwani sidhani kama safari hizo zitakuwa za faida. Lakini hata hivyo siyo rahisi kama inavyoelezwa ili ATCL waweze ruhusiwa kuingia katika soko la Marekani. Ni mchakato mrefu ambao unahusisha uwezo wa nchi kusimamia usalama wa usafiri wa anga (kwa mujibu wa viwango vyao vinavyosimamiwa na FAA). Ni juzi tu Kenya wamepitishwa baada ya mchakato wa muda mrefu ulioanza karibu miaka kumi iliyopita.
 
Acha siasa nyepesi, serikali imeshakuhakikishia ndege yetu si miongoni mwa "terrible teen", wewe unaendelea tu neno la Mange na Zitto, muda utawaumbua tu.
Sasa kama siyo terrible teens ni ndege za aina gani? Mbona Serikali haisemi ni series ipi ya Dreamliner?
 


Kama unaamini kinachosemwa na serikali...utakuja umbuka hapa siku si nyingi.
 
kama ndege aliyonunua Magu na Mwanae dotto ni boeing 787-8 LIN 20 hiyo ni terrible teens. hata ukidhikiri uchi haitabadili ukweli
 
Naomba tusiweke siasa za uchama katika hili. Naamini tutamtetea sana mkuu kwa sababu tunataka kumtetea, lakini ikithibitika maneno ya Zitto ni ya kweli, tutainamisha vichwa chini kwa aibu. Binafsi nimemuelewa sana Zitto.
 
sasa mnunuzi mwenyewe ni dereva wa lori, tutegemee nn tena hapo
A King can do no wrong
 

acha Uongo, website ya Boeing inaonyesha hiyo ni terrible teen. Kujua kama ni terrible teen huambiwi ila unaangalia specs za manufacturer then unaiclassify... Tuache ushabiki kwenye mambo muhimu na tusiishi kwa hisia kama tulivyozoea tukaja kupata hasara..
 
Mkuu,hi comment anzishia uzi wake unaojitegemea.
 
Tanzania ni watu wa kuibiwa kila siku? Ni muda wa kutafakari na kufanya uchunguzi wa kina kabla ya kufikia maamuzi ya mwisho haswa kwenye manunuzi na mikataba
 
Zito mwenyewe bombadia kabla hazijaanza kutumia alikuwa anaziponda kwel, lakini kwa sasa kila leo anazipanda.....tena hadi lift anagongea!
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…