Zitto Kabwe tena katika issue ya ndege ya Boeing

Zitto Kabwe tena katika issue ya ndege ya Boeing

Sasa kama na hawa wameanza mambo haya hatuna wa kumuamini ndani ya ccm
Acha siasa nyepesi, serikali imeshakuhakikishia ndege yetu si miongoni mwa "terrible teen", wewe unaendelea tu neno la Mange na Zitto, muda utawaumbua tu.
 
Zitto ameishiwa siku hizi, hana tofauti na Mange tu, mnunuzi serikali anakwambia ndege yetu sio miongoni mwa "terrible teen", muuzaji na yeye data zake zinaonyesha hivyo hivyo, yeye third part anaendelea kung'ang'ania ni terrible teen, hakuna cha kumsaidia zaidi ya kuacha muda uje kumuumbua tu.


Hata rada mlitetea hivihivi
 
Haka ka zitto si ndo kalisema eti zile bombardier nilikuwa bajaji lakini baadae akaumbuka mana zunapiga mzigo na yeye anazipanda sana tu. Watanzania msidanganyike na haka ka chizi
 
Acha siasa nyepesi, serikali imeshakuhakikishia ndege yetu si miongoni mwa "terrible teen", wewe unaendelea tu neno la Mange na Zitto, muda utawaumbua tu.
Siasa nyepes zp mkuu hilo suala lipo usubir ni muda tu utaongea
 
Nafikiri tunamiss point. Kwanza tungehoji ununuzi wa ndege moja tu ya aina hiyo. Ikiwa kweli biashara itachanganya na ATCL ikapata wateja wa kujaza ndege hiyo kwa route anayoisema Mh Rais (route ya Marekani hadi Kilimanjaro), je kukitokea tatizo watatumia ndege gani kuhudumia njia hiyo? Kumbuka pia kuwa ndege zina matengenezo yake kwa mujibu wa ratiba ya matengenezo na mengine uchukua hadi zaidi ya wiki mbili. Je kipindi hicho watatumia ndege gani. Hii ni moja ya sababu nyingi ya mashirika ya ndege kuanguka. Unajitanua au kuanzisha njia ambazo huwezi kuzihudumia kwa wakati wote (sustainably). Natumaini Mdhibiti (TCAA) watawashauri vyema kabla ya kujiingiza kwenye route. Ndiyo maana kuna kanuni ambayo inaonyesha kuwa ikiwa huduma unazozitoa kwa safari zinahitaji ndege 2 wanatakiwa wawe na ndege 3 kutoa huduma hiyo kwa uendelevu (yaani mara 1.5).

Natumai pia kuwa kuanzisha njia na safari za Marekani, ATCL watafanya uchambuzi yakinifu kwa makini kwani sidhani kama safari hizo zitakuwa za faida. Lakini hata hivyo siyo rahisi kama inavyoelezwa ili ATCL waweze ruhusiwa kuingia katika soko la Marekani. Ni mchakato mrefu ambao unahusisha uwezo wa nchi kusimamia usalama wa usafiri wa anga (kwa mujibu wa viwango vyao vinavyosimamiwa na FAA). Ni juzi tu Kenya wamepitishwa baada ya mchakato wa muda mrefu ulioanza karibu miaka kumi iliyopita.
 
Acha siasa nyepesi, serikali imeshakuhakikishia ndege yetu si miongoni mwa "terrible teen", wewe unaendelea tu neno la Mange na Zitto, muda utawaumbua tu.
Sasa kama siyo terrible teens ni ndege za aina gani? Mbona Serikali haisemi ni series ipi ya Dreamliner?
 
Zitto ameishiwa siku hizi, hana tofauti na Mange tu, mnunuzi serikali anakwambia ndege yetu sio miongoni mwa "terrible teen", muuzaji na yeye data zake zinaonyesha hivyo hivyo, yeye third part anaendelea kung'ang'ania ni terrible teen, hakuna cha kumsaidia zaidi ya kuacha muda uje kumuumbua tu.


Kama unaamini kinachosemwa na serikali...utakuja umbuka hapa siku si nyingi.
 
Zitto ameishiwa siku hizi, hana tofauti na Mange tu, mnunuzi serikali anakwambia ndege yetu sio miongoni mwa "terrible teen", muuzaji na yeye data zake zinaonyesha hivyo hivyo, yeye third part anaendelea kung'ang'ania ni terrible teen, hakuna cha kumsaidia zaidi ya kuacha muda uje kumuumbua tu.
kama ndege aliyonunua Magu na Mwanae dotto ni boeing 787-8 LIN 20 hiyo ni terrible teens. hata ukidhikiri uchi haitabadili ukweli
 
Naomba tusiweke siasa za uchama katika hili. Naamini tutamtetea sana mkuu kwa sababu tunataka kumtetea, lakini ikithibitika maneno ya Zitto ni ya kweli, tutainamisha vichwa chini kwa aibu. Binafsi nimemuelewa sana Zitto.
 
ANAANDIKA ZITTO KABWE: SERIKALI INAFICHA JAMBO KUHUSU DREAMLINER 787-8

“Serikali inaficha jambo kuhusu Dreamliner 787-8, Tunaambiwa kwamba Ndege tunayonunua Boeing 787-8 Dreamliner Ndio kwanza inaundwa. Sio Kweli. Ndege hiyo iliundwa mwaka 2009 na kinachofanyika Sasa ni kubadilisha Injini yake Kwa sababu Injini za ndege hizo zilikuwa na matatizo ya kuwaka moto ( imetokea Kwa Ethiopian na Nippon Air ya Japan ). Hivi sasa kuna ushindani mkubwa kati ya Kampuni ya GE ya Marekani na Kampuni ya Rolls Royce Uingereza kuhusu nani apate biashara ya injini hiyo.
Hata hizi Bombardier tulizonunua hazikuundwa baada ya sisi kuweka order. Ndege hizi ziliundwa mwaka 2014 na zilikuwa tayari zimenunuliwa na Kampuni ya ndege ya Kazakhstan kabla ya baadaye kuuziwa sisi. Ushahidi wa hili ni rahisi Sana, ukipanda ATCL Bombardier tafadhali soma maandishi madogo dirishani utaona S/N 0001519017-040 DATE 10/2014. Hiyo 10/2014 ni Oktoba, 2014.

Serikali inaficha jambo katika suala la ununuzi wa Ndege hii ya Dreamliner. Serikali inajua kuwa imenunua Terrible Teen Kwa bei kubwa kuliko ilivyostahili. Shirika la ndege la Boeing linajua kuwa wametupiga bei ya kuruka na kutudanganyia Kwa kubadili injini. Serikali inajua kuwa haikusimamia maslahi ya Taifa katika mazungumzo kuhusu bei. Bahati mbaya Sana mazungumzo hayo yalimhusisha Rais John Magufuli na Katibu Mkuu Fedha James Doto peke yao. Hapakuwa na Government Negotiation Team Kama ilivyo kawaida ya manunuzi makubwa ya namna haya.

Shirika la Boeing wametumia uzoefu wetu mdogo kutupiga na Ni wajibu wa Watanzania wote Kwa kutumia mahusiano yetu yote duniani kuwataka Boeing wawajibike kwa udanganyifu wao kwetu. Boeing wanapaswa kurudisha sehemu ya Fedha yetu. Ni aibu Kwa Kampuni kubwa Kama Boeing kuiibia Nchi masikini Kama Tanzania. Watanzania mnakumbuka sakata la Radar? Hii ni kurushwa zaidi ya radar. Hela zetu zirudi tujenge Reli au kuongeza Ndege.

Zitto Kabwe
3/5/2017
sasa mnunuzi mwenyewe ni dereva wa lori, tutegemee nn tena hapo
A King can do no wrong
 
Zitto ameishiwa siku hizi, hana tofauti na Mange tu, mnunuzi serikali anakwambia ndege yetu sio miongoni mwa "terrible teen", muuzaji na yeye data zake zinaonyesha hivyo hivyo, yeye third part anaendelea kung'ang'ania ni terrible teen, hakuna cha kumsaidia zaidi ya kuacha muda uje kumuumbua tu.

acha Uongo, website ya Boeing inaonyesha hiyo ni terrible teen. Kujua kama ni terrible teen huambiwi ila unaangalia specs za manufacturer then unaiclassify... Tuache ushabiki kwenye mambo muhimu na tusiishi kwa hisia kama tulivyozoea tukaja kupata hasara..
 
Nafikiri tunamiss point. Kwanza tungehoji ununuzi wa ndege moja tu ya aina hiyo. Ikiwa kweli biashara itachanganya na ATCL ikapata wateja wa kujaza ndege hiyo kwa route anayoisema Mh Rais (route ya Marekani hadi Kilimanjaro), je kukitokea tatizo watatumia ndege gani kuhudumia njia hiyo? Kumbuka pia kuwa ndege zina matengenezo yake kwa mujibu wa ratiba ya matengenezo na mengine uchukua hadi zaidi ya wiki mbili. Je kipindi hicho watatumia ndege gani. Hii ni moja ya sababu nyingi ya mashirika ya ndege kuanguka. Unajitanua au kuanzisha njia ambazo huwezi kuzihudumia kwa wakati wote (sustainably). Natumaini Mdhibiti (TCAA) watawashauri vyema kabla ya kujiingiza kwenye route. Ndiyo maana kuna kanuni ambayo inaonyesha kuwa ikiwa huduma unazozitoa kwa safari zinahitaji ndege 2 wanatakiwa wawe na ndege 3 kutoa huduma hiyo kwa uendelevu (yaani mara 1.5).

Natumai pia kuwa kuanzisha njia na safari za Marekani, ATCL watafanya uchambuzi yakinifu kwa makini kwani sidhani kama safari hizo zitakuwa za faida. Lakini hata hivyo siyo rahisi kama inavyoelezwa ili ATCL waweze ruhusiwa kuingia katika soko la Marekani. Ni mchakato mrefu ambao unahusisha uwezo wa nchi kusimamia usalama wa usafiri wa anga (kwa mujibu wa viwango vyao vinavyosimamiwa na FAA). Ni juzi tu Kenya wamepitishwa baada ya mchakato wa muda mrefu ulioanza karibu miaka kumi iliyopita.
Mkuu,hi comment anzishia uzi wake unaojitegemea.
 
Tanzania ni watu wa kuibiwa kila siku? Ni muda wa kutafakari na kufanya uchunguzi wa kina kabla ya kufikia maamuzi ya mwisho haswa kwenye manunuzi na mikataba
 
Back
Top Bottom