Zitto Kabwe More Than Meets the Eye!

Zitto Kabwe More Than Meets the Eye!

Character X

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
331
Reaction score
382
comrades habari,
Nina tambua umuhimu wakujadili maswala ya kitaifa nakuendelea kutimiza wajibu wa kambi yangu ya upinzani wakuisimamia serikali na kuikosoa kwa hoja makini. Lakini ndugu zangu mniwie radhi tafadhali, Nimesoma threads kadhaa humu ndani zenye collection ya maamdiko ya zitto kabwe in his defense against shutuma flani flani zilizokua zikielezwa juu yake na kuona namna watu walivyo changia kila mmoja akichangia kulingana na mtazamo wake.
Baada ya kusoma sana nimeona vyema nieleze yaliyo mawazo yangu, (kama anavyopenda kusema Mh. Zitto) - Ili kuweka records sawa sawa.

Baada ya kusoma michango ya wengi, wakimuita zitto kila mmoja kwa jina lake, wengine mnafki, wengine msaliti n.k nina Anza kuona kitu ambacho ama sikua na kiona ama nilikiona ila nikahitaji muda zaidi kupata hakika nimekiona. Na mimi nasema tena nitaeleza mawazo yangu ambayo yatakuwa mtazamo wangu, ambao nitauweka wazi kiasi chakitosha ili kutoa nafasi ya kukosolewa.

Kwanza kabisa ninaomba kuweka wazi jambo hapa.

Misingi ya siasa za upinzani iko kwenye hoja, mawazo na mitazamo tofauti, yenye lengo la kuboresha utendaji wa serikali yetu ilikupata the most output from ideas za wakaaji wa nchi husika. Hivyo nikusema nini, hivyo nikusema iwapo vichwa Mia moja vita kaa kujadili jambo na vyote vika fuata hoja ya mtu mmoja bila kufikiri hoja mbadala IPO hatari ya kundi hili kuelekea shimoni wote kwa pamoja kama msafara wa kondoo bila mmoja atakae shtuka na kupona.

Siasa za upinzani nijuu ya hoja tofauti na mawazo mbadala ilikuleta ufanisi bora zaidi katika nchi hiyohiyo moja. Kwaio hoja hapa ni kuboresha ufanisi wa serikali ilikuboresha maisha ya kila siku ya mwananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Hapa swala si uadui na uhasimu tu na chuki zilizo jengwa juu tofauti ya rangi za bendera zetu.

Upinzani sio maana yake uwe adui wa kila mtu ilimradi tu yuko upande wa pili., Laah hasha sivyo hata kidogo.

Kuwa mpinzani haimaanishi huwezi kukubaliana na hoja sahihi za mtu wa upande wapili, Actually ilikuwa mpinzani makini unahitaji kuaminiwa na upande wako lakini na upande wapili pia.,

Tatizo ninalo liona hasa changamoto anayokumbana nayo ng. Zitto, ni ule uswahili, ubinafsi, USHAMBA wa watu wengine ndani ya chama wanao mtazama nakushindwa kumuelewa tu., wanadhani zitto anafanya anayoyafanya ilikupata sifa nakusahau kwamba kiongozi makini huhitaji kuweka misingi wakati mwingine., Lazima afanye gestures (kwakumaanisha kabisa) zinazo onyesha unachokiamini ilikujenga misingi sahihi kwa wale unao waongoza.

Ndugu zangu kuwa mpinzani -result oriented, unahitaji kuaminika!! Lazima sisi wapinzani wenzako tukuamini, lakini lazima tunaowapinga nao wakuamini, kwasababu tunawapinga tukionyesha namnabora zaidi ya kufanya mambo kuliko wanavyo fanya wao. Na hatuwapingi kwakuwa wao ni wao na sisi ni sisi.!
Hatuwapingi CCM kwakua wao ni CCM na sisi ni CHADEMA, tunawapinga kwakua tuna hoja zenyenguvu za kuboresha uendeshaji wa nchi yetu,

sasa ili izo hoja tunazo zipeleka kama wapinzani tukiamini nibora zaidi kuliko za watawala zipate kufanyiwa kazi, lazima hao watawala watuamini, wajue amakwahakika hatuna interest nyingine hidden yoyote isipokuwa tunayoionyesha, -kufanya kazi bora zaidi ya kulijenga taifa hilo hilo. Lazima waone nia ya dhati kwenye maneno yetu na matendo pia ya kuuweka utaifa mbele, nawasipate shaka kuwa huenda hawa agenda Yao ni kukinufaisha chama Chao tu, lazima wajiangalie katika kioo cha utaifa wetu, wayaone madhaifu Yao, wajikosoe!! Hapo ndipo upinzani unapoleta tija kwa taifa.

zipo hoja kwamba mbona zitto anaaminika na serikali ya CCM kuliko wengine, anahongwa!,.

Sasa niseme tu wasi, Zitto kuaminika na watawala is a BIG plus to the change movement.

Namimi nafkiri amefanikiwa kujenga imani kwao si kwa Usaliti ila kwa kazi nzuri ambayo ameifanya so far, kwa professionalism aliyo ionyesha so far.,
Sasa
Kama aliyo yaeleza hapa JF kwenye threads kadhaa alizo ziandika kujitetea kuhusu maswala kama lile la kuamua kutogombea ubunge mwaka 2010, Na kama ni kweli yale aliyo yaeleza kua amefanya bungeni, na kwenye chama, na michango yake ndani na nnje ya nnchi ameyafanya., na kama ni kweli mipango aliyoieleza ni kwasababu alizozieleza hapa na sivinginevyo, na mtazamo alioueleza hapa ndio mtazamo wake halisi.

Basi mimi sioni shida hata kidogo, namuona mtu mwenye uwezo,Nia na sababu ya kufanya mabadiliko ya kweli kwenye siasa zetu, actually na muona mtu mwenye the right mentality for leadership.., if this is what his heart is. then, I think THERE ACTUALLY MIGHT BE MORE TO THIS PARTY STRIFE THAN MEETS THE EYE.

kama ambavyo nilieleza kwenye thread yangu hivi majuzI, Zitto has the right preparation and the right mentality to bring about true change to Africa.,

Naomba niwaonyeshe kitu hapa,wakati wa vita dhidi ya utawala wa apartheid nchini Africa kusini, yalikuwepo makundi mengi sana yakipigana kila moja mwa style yake(maana wengi wanaijua ANC pekeyake) kinyume na utawala ule, lilikuwepo kundi moja lililo ongozwa na jamaa mmoja very radical(Robert somebody,aliekuja fia jela)actually ndilo lililo ongoza maandamano flani yalio sababisha wanafunzi maelfu wa Soweto kuuwawa na jeshi kama kuku, hakukuwahi na hapaja wahi tangu kipindi hicho kutokea mauwaji makubwa namna ile Africa ya kusini. ukiangalia kwajujuu unaweza ukadhani yeye ndiye alikua mpinzani kweli, lakini Nelson Mandela anasema kwenye kitabu chake "the long walk to freedom" kikundi kile kilikuwa very irresponsible, na maandamano Yao yaliendeshwa kwa madhara makubwa sana ya mali na maisha ya raia tafauti na vile maandamano ya ANC yaliendeshwa (ofcourse hii haimaanishi hapakutokea vifo katika maandamano ya ANC). Na by the way Nelson anafika maali nayeye anasema katika kukaribia uhuru akiwa anatokea jela na baada ya watawala wengi kuanza kumuamini, na wazungu wengi zaidi kugundua Kwamba anachofanya nikwaajili ya haki ya ubinaadamu tu nasio kisasi kama yalivyokuwa makundi mengi ya kipindikile,alianza kuitwa na kufanya vikao vingi sana na wakuu waserikali ile, akiwa peke yake na akitokea jela kiasi kwamba watu wa ANC waka Anza kumshutumu kuwa anahongwa na makaburu, nahuyo jamaa Robert nani sjui ndipo akaibeba ile kama agenda yake kusema Mandela anaonekana akifanya vikao na makaburu, amehongwa!
Lakini mandela anasema ilibidi waifikishe mahali ANC iaminike na watu wapande zote, makaburu na waafrica pia, wanachama wa ANC, na wa chama tawala pia, kwamba hoja zao zakipinzani zina Nia moja tu! - kufanya maisha bora zaidi kwa kila mmoja.

Ninachosema hapa ni kitu gani, Zitto kujenga kuaminiwa na seeikali ya CCM hakutakiwi kumaanisha ni msaliti, nandio maana hoja zake nyingi bungeni zimefanyiwa kazi na kuboresha shuguli za bunge na serikali kwa ujumla, wakati hoja za wengine hata pale ambapo hua nzuri na zenyenguvu kabisa hukataliwa bila hata kusikilizwa.

Baada ya kusema hayo mengi niliosema, ninaomba kumalizia kwakusema, Mh. Zitto anahitajika CHADEMA sikwasababu bila yeye CHADEMA haiwezekani kuendelea HAPANA HATA KIDOGO!

Ila kwasababu having him is a Plus!
Nevertheless, kwasababu za kimisingi (principles) kamanilivyoeleza kabla, naeleza tena, uamuzi wa CC ya Chadema ni SAHIHI.

Mh. Zitto, tafadhali, Nina amini uwezo Wako, na Nia yako pengine kuliko wengi ndani ya kambi hii ya upinzani, kama swala ni waraka wa ushindi, na mikakati isiyo halali ilyokuwa ikifanyika ndani ya chama ilikumuondoa mwenyekiti HALALI Kwakueleza madhaifu yake na shutuma za makosa ya kiutendaji nje ya utaratibu wa vikao halali vya chama, fuata maelekezo ya CC tufunge ukurasa huu, Rudi tujenge chama, mimi kama vijana wengi ningetamani kuingia humo pia siku moja lakini tunahitaji mazingira sahihi na mentality sahihi, mentality uliyonayo ndugu zitto.
We need to close this chapter and put it behind us.

Comrades,
Niwashukuru.
 
CDM family na CDM halisi,huo mtazamo wako umewakosoa Chadema family utaitwa msaliti na kukuwinda upewe sumu au ukikoswakoswa #Tindikalijkali

Nasikia aibu sana unapomlinganisha #lema na #ZZK ,eti lema yuko juu...!!ha ha ha
Tangia aingie bungeni yeye ni kama robot hawezi hata kujenga hoja ila kwa #maandamano hapo sawa yuko number moja,VIJANA WENGI WA ARUSHA MTAPATA SANA VILEMA KWA SIASA ZA VIROBA MAANDAMANO ZA LEMA
 
Nasikia aibu sana unapomlinganisha #lema na #ZZK ,eti lema yuko juu...!!ha ha ha
Tangia aingie bungeni yeye ni kama robot hawezi hata kujenga hoja ila kwa #maandamano hapo sawa yuko number moja,VIJANA WENGI WA ARUSHA MTAPATA SANA VILEMA KWA SIASA ZA VIROBA MAANDAMANO ZA LEMA

Sidhani kama nimetaja jina la Mh. Lema katika thread hii.
 
Actually umemtaja na kuelezea kuhusu Mandela kwenye huu ujumbe wako, vema. Umeshindwa kuonyesha wapi makaburu wa iliyo kuwa SA ya ubaguzi wa rangi walisimama kidedea, tena kwa juhudi na maarifa kutumia propaganda kumtetea Mandela, kama tunavyo ona leo hii ccm wanavyofanya kwa zzk. Je wewe kama ni mkweli kwa nafsi yako huoni tayari hapa kuna walakini mkubwa? Asiye ona hilo labda mnafiki tu.

Actually wa baya wa zzk wametajwa kwenye waraka. Na ni wale waliomshauri kuwa akaembali na mambo ya chama chake na akakubali bila ya yeye kujua kuwa harakati katika chama hasa kuleta changamoto katika kusimamia utendaji wa serikali ndio kulimpa umaarufu hapo awali. Mbaya zaidi wanamshauri tena akaembali na viongozi wa juu seikalini baada ya kuona kuwa anakubalika kwao alipo onyesha umahiri wa kukihujumu chama chake.

Actually ukiwa makini utagundua kuwa kuna watu wanafanikisha mkakati wa kummaliza zzk na kukivuruga cdm, mimi na amini mpaka sasa wamefanikiwa kwa kiasi fulani.

Actually itakuwa vigumu sana kwake (kama haya mambo tunayosikia na kusoma kuhusu zzk) kuaminika si kwa cdm pekee bali kwa hao wanao mtumia. Na rudia kama haya tunayo yasikia yana ukweli wowote.

Actually, actually....!
 
comrades habari,
Nina tambua umuhimu wakujadili maswala ya kitaifa nakuendelea ....................................... maelekezo ya CC tufunge ukurasa huu, Rudi tujenge chama, mimi kama vijana wengi ningetamani kuingia humo pia siku moja lakini tunahitaji mazingira sahihi na mentality sahihi, mentality uliyonayo ndugu zitto.
We need to close this chapter and put it behind us.

Comrades,
Niwashukuru.
Mkuu you just nailed it!kuna watu wanafikiri upinzani ni kutosocialize kwa hali yeyote na upande wa pili na wengine hufikiri ile phyisical violency ndio upinzani uliotukuka!
 
Actually umemtaja na kuelezea kuhusu Mandela kwenye huu ujumbe wako, vema. Umeshindwa kuonyesha wapi makaburu wa iliyo kuwa SA ya ubaguzi wa rangi walisimama kidedea, tena kwa juhudi na maarifa kutumia propaganda kumtetea Mandela, kama tunavyo ona leo hii ccm wanavyofanya kwa zzk. Je wewe kama ni mkweli kwa nafsi yako huoni tayari hapa kuna walakini mkubwa? Asiye ona hilo labda mnafiki tu.

Actually wa baya wa zzk wametajwa kwenye waraka. Na ni wale waliomshauri kuwa akaembali na mambo ya chama chake na akakubali bila ya yeye kujua kuwa harakati katika chama hasa kuleta changamoto katika kusimamia utendaji wa serikali ndio kulimpa umaarufu hapo awali. Mbaya zaidi wanamshauri tena akaembali na viongozi wa juu seikalini baada ya kuona kuwa anakubalika kwao alipo onyesha umahiri wa kukihujumu chama chake.

Actually ukiwa makini utagundua kuwa kuna watu wanafanikisha mkakati wa kummaliza zzk na kukivuruga cdm, mimi na amini mpaka sasa wamefanikiwa kwa kiasi fulani.

Actually itakuwa vigumu sana kwake (kama haya mambo tunayosikia na kusoma kuhusu zzk) kuaminika si kwa cdm pekee bali kwa hao wanao mtumia. Na rudia kama haya tunayo yasikia yana ukweli wowote.

Actually, actually....!

waraka unaoutumia hauwezi kua authority ya kujengea hoja kwasababu haujathibitishwa na upande wowote kuwa kweli. Kuna kila dalili kwamba ni "hekaya" batili tu.
Hebu jaribu kujenga hoja yako kwakuonyesha evidence yoyote ya CCM kumtumia zitto.
 
waraka unaoutumia hauwezi kua authority ya kujengea hoja kwasababu haujathibitishwa na upande wowote kuwa kweli. Kuna kila dalili kwamba ni "hekaya" batili tu.
Hebu jaribu kujenga hoja yako kwakuonyesha evedence yoyote ya CCM kumtumia zitto.

Kumbe ccm wanamtumia zzk? we wasema. Soma vizuri mimi nimesema wana piga propoganda za kumtetea, kama hilo hulioni basi, huo ndio unafiki wenyewe huo. Tumeambiwa na tumeamini Dr alikiri kuujua na kuuhariri waraka.
 
Kumbe ccm wanamtumia zzk? we wasema. Soma vizuri mimi nimesema wana piga propoganda za kumtetea, kama hilo hulioni basi, huo ndio unafiki wenyewe huo. Tumeambiwa na kutumeamini Dr alikiri kuujua na kuuhariri waraka.

wanamtetea kwasababu wanamuamini. Na wanahisi anatendewa isivyo haki
 
Kumbeee! sasa unategemea cdm wafanye nini hapa? Na inajulikana kwa kila mtu rafiki wa adui yako..... malizia mwenyewe ndg.

nivigumu kufanya kazi na huo mtazamo wa rafiki ya adui yako ni adui yako., na hicho ndicho nilichokua nikieleza hapa., upinzani haumaanishi uadui.
 
kitu gani kinakufanya udhani zitto haaminiki na CCM anatumika tu.

Kwasababu kama ni hoja/mawazo/ushauri mzuri kwa serikali mbona hata wako viongozi wengi tu waadilifu wenye upeo‚ hoja‚ mawazo na hata ushauri mzuri lakini hawajalwi wala kusikilizwa‚ tena wengi wamekuwa wakipuuzwa na hata wakati mwingine kupoteza nyadhifa zao kwasababu maslahi ya viongozi yaliguswa.

Swali wanalojiuliza watanzania walio wengi hasa wana mageuzi ni kwamba huko kuaminika na serikali ni kwaajili ya nia njema ua nigeresha tu ya watawala‚ mbona wasiwaamini wataalam wao na wengine wengi waadilifu ambao kimsingi hawatetei maslahi ya watawala wenye malengo yao?
 
mleta mada umenena safi.upinzani wa siasa usikufanye rafiki na rafiki msisalimiane.

Upinzani wasiasa usikuachanishe undugu,usikugombanishe,

Vijana tuliowengi tumepokea mageuzi vibaya.tunauelewa kuwa kama mtu akiwa ccm na mwingine cdm tusipigiane simu,tusikae pamoja.siasa za uhasama hazileti tija kwa taifa bali kuleta machafuko.
 
Vigumu kwa nani wewe au mh zzk? Kwa cdm wao wamechukua hatua kwa kuwavua uongozi wanaowaita wasaliti. Sasa msaliti ni jina linalo mfaa nani, mpinzani, adui au rafiki yako. Jibu mwenyewe.
 
Vigumu kwa nani wewe au mh zzk? Kwa cdm wao wamechukua hatua kwa kuwavua uongozi wanaowaita wasaliti. Sasa msaliti ni jina linalo mfaa nani, mpinzani, adui au rafiki yako. Jibu mwenyewe.

unajua swala sio kuitwa tu msaliti, swala ni kuthibitisha usaliti., nashindwa kumuita mh. Zitto msaliti kwakua hakuna aliye weza kuthibitisha usaliti wake., swala la yeye kuwa karibu na watu wa serikali haitoshi kumuita msaliti., ila nasema kwa habari ya waraka ule wa ushindi lile ndio kosa la zitto na ndomaana na sema kwalile CC imefanya uamuzi sahihi.
 
unajua swala sio kuitwa tu msaliti, swala ni kuthibitisha usaliti., nashindwa kumuita mh. Zitto msaliti kwakua hakuna aliye weza kuthibitisha usaliti wake., swala la yeye kuwa karibu na watu wa serikali haitoshi kumuita msaliti., ila nasema kwa habari ya waraka ule wa ushindi lile ndio kosa la zitto na ndomaana na sema kwalile CC imefanya uamuzi sahihi.

Kama umekubali waraka mm ni kosa inamana una kubaliana na cc cdm. Wewe ungekuwa na maoni gani kuhusu jina la hili kosa. Cc cdm wameliita kosa hili usaliti na pengine uhaini wote tumesikia. Labda wewe pendekeza jina tofauti na utushawishi tulitumie.
 
Mleta uzi nimependa sana mtazamo wako. Zaidi umeyaamini mawazo yako na kukaribisha watu kukosoa ila waliowengi wameshindwa kutoa hoja ambazo zina mashiko bali wameendelea kuunga maamuzi ya cc bila kutoa hoja za kuunga maamuzi hayo.
Mi ningependa kuona watu wanatoa makosa ya zzk waziwazi ili kila mtu mwenye upeo wa kutafakali nae achambue na kuona uhalali wa usaliti wa huyo jamaa. Kwa waraka wa mabasdiliko 2013 wa kitila na wenzie zzk hausiki ila amependwa na hao wasaka mabadiliko na kuona kwamba kwa wanavyotaka wao zzk ndio angefaa kukiongoza chama na kikatimiza lengo lake la kuing'oa
ccm madarakani. Labda tungejua hayo makosa 11 waliyopewa ndio tungeweza kujadili uhaini wa zzk, kinachofanyika sasa ni ushabiki wa mtu au kundi fulani bila hata kuwa na sababu za msingi. KWA MNAO JARIBU KUKOSOA UZI HUU wekeni hoja zenye mashiko angalau
zimuumize kichwa mleta uzi. So far upinzani si uadui mpaka watu msizungumze pamoja kwa furaha bali upinzani wa siasa ni kutoa hoja zenye nguvu ambazo mnaona wapinzani wenu hawazitumii kuboresha maisha ya watu na kama hayataki kuzitumia kwa masilai yao binafsi basi ombeni kuungwa mkono na wenyenchi ili wawape ruhusa ya kuwaongoza. Si kuamisha upinzani wa hoja za siasa mpaka kwenye maisha ya kawaida nje ya siasa.
 
Actually umemtaja na kuelezea kuhusu Mandela kwenye huu ujumbe wako, vema. Umeshindwa kuonyesha wapi makaburu wa iliyo kuwa SA ya ubaguzi wa rangi walisimama kidedea, tena kwa juhudi na maarifa kutumia propaganda kumtetea Mandela, kama tunavyo ona leo hii ccm wanavyofanya kwa zzk. Je wewe kama ni mkweli kwa nafsi yako huoni tayari hapa kuna walakini mkubwa? Asiye ona hilo labda mnafiki tu.

Actually wa baya wa zzk wametajwa kwenye waraka. Na ni wale waliomshauri kuwa akaembali na mambo ya chama chake na akakubali bila ya yeye kujua kuwa harakati katika chama hasa kuleta changamoto katika kusimamia utendaji wa serikali ndio kulimpa umaarufu hapo awali. Mbaya zaidi wanamshauri tena akaembali na viongozi wa juu seikalini baada ya kuona kuwa anakubalika kwao alipo onyesha umahiri wa kukihujumu chama chake.

Actually ukiwa makini utagundua kuwa kuna watu wanafanikisha mkakati wa kummaliza zzk na kukivuruga cdm, mimi na amini mpaka sasa wamefanikiwa kwa kiasi fulani.

Actually itakuwa vigumu sana kwake (kama haya mambo tunayosikia na kusoma kuhusu zzk) kuaminika si kwa cdm pekee bali kwa hao wanao mtumia. Na rudia kama haya tunayo yasikia yana ukweli wowote.

Actually, actually....!

Viroba at work
 
Back
Top Bottom