GE2025 ZItto Kabwe ameanza mbwembwe ACT mnajulikana!!

GE2025 ZItto Kabwe ameanza mbwembwe ACT mnajulikana!!

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

jindundu

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2025
Posts
679
Reaction score
580
Akiwa Zanzibar' kumtambulisha Mgombea Urais wa Chama chake Luhaga Mpina, Kiongozi wa zamani.wa ACT wazalendo ZItto Kabwe amejiapiza kwamba kama Luhaga Mpina atashinda kwenye Uchaguzi huo, kama atatangazwa au kama hatatangazwa, atakuwa Rais.

Amesema vivyo hivyo kwa wagombea Ubunge na Udiwani kupitia Chama hicho kwamba wakishinda kama hawatatangazwa, watakalia nafasi zao.

Kwamba CCM wasitumie vyombo vya dola kupoka matokeo hayo ya Uchaguzi maana hawatakubali.

ZItto anatamka haya maneno kwetu wengine ni kichekesho na tunaona ni kejeli tu kwa wapiga kura. Kila mtu anajua fika kuwa hakuna uwiano wa kiushindani kati ya Luhaga Mpina na Mgombea wa CCM mama Samia Suluhu Hassan.

Tukija kwenye Uchaguzi wa Wabunge na Madiwani hapo political Strategy iliyopo inajulikana wazi kuwa, " tuwape majimbo kadhaa wachukue Ubunge na Kata kadhaa wachukue Udiwani". Lengo ni kuonyesha Dunia kuwa Demokrasia ipo tena ya kumwaga. Lengo ni kuwapoteza maboya kule ambako huwa tunakimbilia kuomba misaada na mikopo. Maana macho na masikio yao ni kwenye hili zoezi la Uchaguzi. Wana tu zoom tu waone Nini kitatokea ili wajue watabonyeza wapi ili kutukomesha.

Kwa hiyo Ndg ZItto Kabwe tunamwelewa vizuri na project yake. Hongera!!
 
ZK na LM wana Hoja kwenye chama chao tuwasikilize vizuri wakija kujinadi na sera zao. Luhaga mbona hata kabla ya kuja ACT tulikuwa tunamkubali kwa hoja na misimamo yake ya kuikemea hata Serikali ya chama chake mwenyewe? So tusimuhukumu kabla ya kumpa nafasi ya kumsikiliza mipango na sera zao.
 
Back
Top Bottom