Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Kiongozi mstaafu wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, leo Jumapili amechukua rasmi fomu ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini kupitia chama hicho.
Zitto amekabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa Jimbo, Ndugu Idd Adam, katika tukio lililoshuhudiwa na wafuasi na viongozi wa chama hicho.
Tukio hili linakuja siku moja baada ya kufanyiwa maombi maalumu na wanakwaya wa Kanisa la Moravian Kigoma, na leo asubuhi alifanya ziara ya kimya kimya katika makaburi ya Rubengela ambako mama yake mzazi, Hajjat Shida Salum, amezikwa. Aidha, kinamama wa Kigoma mjini walimfanyia dua maalum katika Zawiya za wanawake kama sehemu ya kumuombea baraka katika safari yake ya kisiasa.
Katika kuonesha mshikamano na hamasa, zaidi ya wanawake 600 kutoka matawi yote 72 ya ACT Wazalendo Kigoma Mjini walitembea naye kwa umbali wa kilomita mbili kutoka Ofisi ya ACT Wazalendo Mkoa iliyoko Rubuga Ujiji hadi Ofisi za Jimbo Buzebazeba.
Akizungumza baada ya tukio hilo, Zitto alisema, "Ilikuwa ni shughuli ya Wanawake wa Mji kwa heshima ya mwenzao ‘Da Shida’. Ninaukabidhi mchakato mzima wa mimi kurejea Bungeni kwa Wanawake wa Mji wa Kigoma Ujiji. TUTASHINDA KWA KUPAMBANA!"
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Zitto Kabwe aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo hilo kwa vipindi viwili na sasa anarejea kwenye kinyang’anyiro akijivunia sapoti kubwa ya wanawake wa Kigoma.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Zitto Kabwe aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo hilo kwa vipindi viwili na sasa anarejea kwenye kinyang’anyiro akijivunia sapoti kubwa ya wanawake wa Kigoma.