Zitto & Dr. Slaa Kaeni kitako katika hili

Zitto & Dr. Slaa Kaeni kitako katika hili

WABHEJASANA

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2011
Posts
4,225
Reaction score
869
Wakuu Habari za Krismas jana?,najua kwa sasa wengi wanfungua zile zawadi za jana!!!!!!!!

Kuna jambo ambalo nimelifikiria kwa muda mrefu sana tangu yalipoanza malumbano humu Jamvini juu ya Zitto na masalia yanavyofanya mkakati wa kumchafua Dr.Slaa Thread nyingi nilizosoma juu ya kilichoibuka nikabaini kuna kushambuliana kwa hali ya juu na inavyoonekana ni jambo ambalo watu walik na kujipanga namna ya kufanya mashambulizi.

Maoni ya wachangiaji wengi ambao wamekuwa wakichangia kwenye Thread hizo wamekuwa wakizungumzia sual la ukabila wakifikia hadi hatua ya kulitaja kabila la wachaga kwamba ndilo linalomsakama Zitto eti kwa sababu Muasisi wa CHADEMA anatokana na kabila hilo hivyo wanamhitaji Dr Slaa kwa sababu naye anatokea ukanda huo pamoja na kwamba yeye si Mchaga.

Kwanza sitaki kuamini saana hili suala la ukabila na hata kama lipo kwa namna yoyote ile binfasi kwa maoni yangu naona haliwezi kuathiri utendaji kazi wa Zitto wala Dr.Slaa kwa sababu siku zote naamini kwamba unapoona unaandamwa na matatizo utambue kwamba kuna furaha mbeleni kwa hiyo binafsi naichukulia kama sehemu ya mapito ya zitto pamoja na Dr Slaa katika mafanikio.

Anayoyapata Zitto hivi sasa ndani ya chama chake hayana tofauti na anayoyapata Dr Slaa kutoka ndani ya CCM na ndiyo maana utaona kila siku kunakuwepo na hoja zinazojaribu kumchafua Slaa ama aonekane hafi katika jamii,ama basi wajaribu kupunguza mvuto wake kwa jamii.

Kwa maoni yangu na kwa mujibu wa uchunguzi wangu,CCM inamuhofia sana Dr Slaa na hasa endapo atawania Urais mwaka 2015 na hili halina ubishi kwamba Slaa ni mtu ambaye anapendwa na watanzania walio wengi na hii inatokana na hazina kubwa aliyoiweka miaka mingi katika kutetea rasilimali za watanzania ndiyo maana leo hata ukisema nini watu hawawezi kukuelewa juu ya Slaa na pamoja na kwamba kuna mambo yanyogusa lakini watu wanachukulia kama sehemu ya ubinadamu kwa sababu na yeye ni binadamu anayetumia Damu,maji na Nyama.

Kinachonishangaza na kuniumiza ni hili ambalo linaonekana kuibuka ndani ya CHADEMA yenyewe ambayo sasa imeanza kuchafuana wao kwa wao,kwa sababu ni uwazi wa kweli kwamba ndani ya CHADEMA hivi sasa kuna makundi mawili kundi la kwanza likiwa ni la Zitto na la pili likiwa ni la Dr Slaa ambalo kila moja linahofia mwenzake katika suala la Urais na ndiyo maana utaona kuna mambo ya ajabu ajabu ambayo yanaendelea kutokea kama ambavyo tunashuhudia mengine humu JF.

Yawezekana kweli kundi la Dr Slaa linafanya kila jitihada za kuhakikisha kwamba linalidhoofisha kundi la Zitto lakini pia huenda kundi la Zitto nalo linafanya jitihada za kulidhoofisha kundi la Dr Slaa ili liweze kupata nafasi,lakini ukweli ulio wazi ni kwamba hili jambo ni la hatari sana na hapa napenda niseme wazi kwamba huu ndio mwanzo wa chama kugawanyika na mwisho wa siku hata kama kilikua na asilimia kubwa ya kuing'oa CCM madarakani lazima asilimia hizo zitapungua tena kwa kiwango kikubwa jambo ambalo naona kwamba linaweza kuipa nafasi tena CCM kuitawala nchi hii.

Hakuna ubishi kwamba Zitto anakubalika na anao wafuasi wengi na hasa ukanda wa Ziwa ambao hakuna ubishi kwamba una watu wengi,lakini Slaa naye ana kundi kubwa ingawa kwa kiwango kikubwa anaonekana kuungwa mkono zaidi na watu kutoka kaskazini ambao ukiangalia idadi yake si kubwa kama ile ya Ziwa,kwa hiyo kinachokuja kutokea hapa ni kwamba zitabaki zile kanda za kusini,kati na mashariki ambapo huko itategemea nani mwenye mvuto zaidi na kwa vyovyote ni lazima watagawana ingawa kuna mshindi lazima tapatikana bila kujali ni Zitto ama Dr Slaa.

OMBI LANGU:Kuna kila sababu ya hizi pande mbili kukaa chini na kuumaliza huu mgogoro na aina yoyote ya kuwatimua ama kuwasimamisha watu wa kundi fulani ni kutengeneza bomu lingine kubwa ambalo linaweza kuwalipua watu wengi zaidi,jamani tukumbuke hii ni vita ambayo inahitaji umakini wa hali ya juu,vinginevyo mnaweza kukaa mnapigana ndani kwa ndani mwisho linakuja jamaa linanawateka wote na kuwa baba wa mji na ninyi mnabaki kuwa wajakazi wake.

Tukumbuke kwamba waswahili walisema "Vita vya Panzi,furaha ya Kunguru" Msemo huu una maana kubwa sana.

Naomba kuwasilisha na Tudadavue kwa nia ya kujenga.
 
Mkuu nakuunga mkono, suluhu ipatikane mapema. hili suala likiachiwa liendelee litakivuruga chama na wanachama kwa ujumla.
 
Ushauli wako ni mzurh pia ni vema wakae chini wamalize tofauti zao kwa masilah ya chama na watanzania kwa ujumla
 
Kilichonifurahisha ni kwamba hawa watu wako makini sana,wote wawili wamewatumia wafuasi wao kutoa hoja na maelezo lakini wao hawajajitokeza kujibu chochote,hii inaonesha ni namn gani ni wakomavu katika siasa za nchi hii,na kwa sababu hawajafanya hivyo humu jukwaani basi wakae chini,hiki chama kinapendwa na watu na kimekua kimbilio la wanyonge hili halina ubishi,lakini vurugu na kelele zinazoendelea hizi zitawafanya watu kuwa na taharuki mwisho watakata tamaa,na ukweli ni kwamba chama bana ni watu asikudanganye mtu.
 
mgogoro ktk jamii ni mzuri, endapo jamii hiyo haitaona kuwa mgogoro wao ni uadui. binafsi nikiutazama mgogoro huu nauona kuwa ZZK amejitenga akijiepusha na mgogoro wenye UADUI ,ambao ni hatari kwa ustawi wa chama. ndo maana ktk maelezo yake amesisitiza ktk ustawi wa chama kuna jasho na damu yake. hivyo atakuwa wa mwisho kukisaliti. kuna Huyu BEN sijui ni yy mwenyewe au kuna REMOTE, sehemu fulani . yy huyu anaendesha mgogoro huu, kwa maana ya UADUI, lengo na madhumuni yake kuwa mgombea wake anayemtaka ndiye apewe nafasi ya kuteuliwa bila kipingamizi na kwake anaona PINGAMIZI ni ZZKz, hivyo anapaswa adhibitiwe kwa udi na uvumba asifurukute, hivyo amejipanga/ wamejipanga, kuhakikisha ukweli na uongo vinawekwa pamoja kumuangamiza. naandika haya kwa sababu mara nyingi kabla ya sakata hili kuibuka, nilikuwa namsifia saana ZZK, kama mwanasiasa kijana mzalendo, asiyependa kujinasibu kichama mwenye kusimamia UZALENDO kwa nchi yake, anafaa kuwa rais , hakika nilishambuliwa saana na mtu huyu BEN, hivyo kwangu mimi sishangai leo hii, yy akisimama na kuuuuunda uuuuuunda kashfa kwa ZZK zenye muono wa UADUI. kuna hawa wengine BI JULIANA na KIKUNDI CHAKE, hawa nao wameeleza mengi ,yenye kuonesha mgogoro wa kiuadui wkijinasibu kumuunga mkono ZZK, hapo ndipo MGOGORO huu unapokuwa si mzuri kwa ustawi wa chama. ninavyoamini kila mwana CDM, anahaki ya kuomba kupitia chama chake haki ya kuteuliwa kugombea nafasi ya urais , ubunge ,udiwani na nafasi zingine zinazotambuliwa kikatiba. na kila mwana CDM anapaswa kuridhia maamuzi yanayopitishwa na vikao vya juu vya chama chao. sasa kuna kosa gani? kutengeneza mgogoro wenye kujenga ktk kumtafuta mgombea wenu, kisha mkazika tofauti zenu na kujenga chama. kauli hii, mimi sikutaki ZZK namtaka SLAA au MBOWE au MNYIKA si uadui ni DEMOKRASIA ktk chama. mwisho wa siku huyu ndo mgombea wetu tukiulizwa na wananchi anafaa sote tuwe na kauli moja. mkiendeleza mgogoro adui mtasikia NAMBARI WANI EEEEEEEEH <NAMBARI WANI NI CCM, mtabakia tumeibiwa kura.
 
Pamoja sana mkuu umeongeza mambo ya msingi sana.
 
By Wabhejasana

"Hakuna ubishi kwamba Zitto anakubalika na anao wafuasi wengi na hasa ukanda wa Ziwa ambao hakuna ubishi kwamba una watu wengi,lakini Slaa naye ana kundi kubwa ingawa kwa kiwango kikubwa anaonekana kuungwa mkono zaidi na watu kutoka kaskazini ambao ukiangalia idadi yake si kubwa kama ile ya Ziwa,kwa hiyo kinachokuja kutokea hapa ni kwamba zitabaki zile kanda za kusini,kati na mashariki ambapo huko itategemea nani mwenye mvuto zaidi na kwa vyovyote ni lazima watagawana ingawa kuna mshindi lazima tapatikana bila kujali ni Zitto ama Dr Slaa"



Huku ni Uongo mkuu. kukubalika kwa Zitto kulitokana na Juhudi za DR. Slaaa,

Wabunge wengi wa Chadema wameongezeka bungezi ni juhudi za DR. Slaa


kanda ya ziwa DR. Slaa anakubalika kuliko mtu yeyote : wazeee kwa vijana , zitto labda akubalike kigoma peke yake na Tena kwenye jimbo lake.


Baada ya DR. Slaa kanda ziwa anayefuata kukubalika ni Maghufuli, ambaye sasa umaarufu wake umeanza kupungua.

Kwa kanda ya ziwa List ya wtu wanokubalika.


DR. Slaaa....60%
Maghufuli........15%
Sitta.............12.5%
Zitto..............12.5%

Nyanda za Juu kusini.

DR. Slaaa.........54%
Mwandosya.......30%
Mwakyembe.......11%
Zitto.................05%


Kusini(Lindi,Mtwara)

Membe..........54%
DR. Slaa..........36%
Zitto..............10%

Nyanda za Juu kaskazini
DR. Slaa..........70%

Lowasa...........26%

Zitto............04%

Dar + Pwani

Kikwete......48%

Dr. slaaa......42%

Zitto...........10%
 
Ndani ya chama, Slaa anakubalika makao makuu, Zitto anakubalika matawini.
Slaa anashindwa kusoma alama za nyakati, kushindana na Zitto kunamshusha daraja kila siku hasahasa ndani ya chama.
 
Ndani ya chama, Slaa anakubalika makao makuu, Zitto anakubalika matawini.
Slaa anashindwa kusoma alama za nyakati, kushindana na Zitto kunamshusha daraja kila siku hasahasa ndani ya chama.

Hayo mawazo yako mkuu
 
Hallo mwanzisha thread,
Usijaribu kucheza na akili za makachero kama mimi. Wewe uliyeanzisha thread ama ni mkuu wa kikundi cha masalia au ni mfuasi wake. Na nia ya kuanzisha hii thread ni kuomba msamaha kwa njia ya ku-blackmail kama ambavyo mmekuwa mnafanya siku zote. Na wachangiaji wote wa mwanzo mwanzo wanaokuunga mkono ni wewe/nyie wenyewe kwa wenyewe, mtindo ambao nao mmezoea kuutumia. Unasema Dr Slaa wakae na Zitto eti Chadema imegawanyika vipande viwili? Hebu acheni kucheza na akili za watu bwana. Mlikubali kutumiwa na CCM na mtavuna mlichopanda. Kama kweli mna nia ya kuomba msamaha jitokezeni muungame mbele ya umma na wacheni hizi njia za ku-blackmail eti Zitto akiondoka Chadema itakufa.
 
By Wabhejasana

"Hakuna ubishi kwamba Zitto anakubalika na anao wafuasi wengi na hasa ukanda wa Ziwa ambao hakuna ubishi kwamba una watu wengi,lakini Slaa naye ana kundi kubwa ingawa kwa kiwango kikubwa anaonekana kuungwa mkono zaidi na watu kutoka kaskazini ambao ukiangalia idadi yake si kubwa kama ile ya Ziwa,kwa hiyo kinachokuja kutokea hapa ni kwamba zitabaki zile kanda za kusini,kati na mashariki ambapo huko itategemea nani mwenye mvuto zaidi na kwa vyovyote ni lazima watagawana ingawa kuna mshindi lazima tapatikana bila kujali ni Zitto ama Dr Slaa"



Huku ni Uongo mkuu. kukubalika kwa Zitto kulitokana na Juhudi za DR. Slaaa,

Wabunge wengi wa Chadema wameongezeka bungezi ni juhudi za DR. Slaa


kanda ya ziwa DR. Slaa anakubalika kuliko mtu yeyote : wazeee kwa vijana , zitto labda akubalike kigoma peke yake na Tena kwenye jimbo lake.


Baada ya DR. Slaa kanda ziwa anayefuata kukubalika ni Maghufuli, ambaye sasa umaarufu wake umeanza kupungua.

Kwa kanda ya ziwa List ya wtu wanokubalika.


DR. Slaaa....60%
Maghuli........15%
Sitta.............12.5%
Zitto..............12.5%

Nyanda za Juu kusini.

DR. Slaaa.........54%
Mwandosya.......30%
Mwakyembe.......11%
Zitto.................05%


Kusini(Lindi,Mtwara)

Membe..........54%
DR. Slaa..........36%
Zitto..............10%

Nyanda za Juu kaskazini
DR. Slaa..........70%

Lowasa...........26%

Zitto............04%

Dar + Pwani

Kikwete......48%

Dr. slaaa......42%

Zitto...........10%

labda unamaanisha kando ya ziwa tanganyika sio kanda ya ziwa ninyoijua mimi , your analysis is raw rubbish
 
Join Date : 9th September 2012
Posts : 1,092
Rep Power : 534

Joined with 17 days 1092 post ??????? 65 per day 3post per day

Sorry mkuu inawezekana umetuma under a certain mission na prezee aka Zitto

We do not buy this RUBBISH
 
Last edited by a moderator:
Huu up.upu ulioandika hapa mtumie Zitto kwenye account yake ya twitter John Mnyika ameshatoa maelezo ya taatibu za chama na Kwamba suala hili linashughulikiwa . Nyie wafuasi wa zitto siku zote ndio mnaomuharibia .Pia inaelekea Zitto kwa tabia yake ya kutokukubali kushindwa ndio anaandika haya na kuwapa m-post .
 
Last edited by a moderator:
By Wabhejasana

"Hakuna ubishi kwamba Zitto anakubalika na anao wafuasi wengi na hasa ukanda wa Ziwa ambao hakuna ubishi kwamba una watu wengi,lakini Slaa naye ana kundi kubwa ingawa kwa kiwango kikubwa anaonekana kuungwa mkono zaidi na watu kutoka kaskazini ambao ukiangalia idadi yake si kubwa kama ile ya Ziwa,kwa hiyo kinachokuja kutokea hapa ni kwamba zitabaki zile kanda za kusini,kati na mashariki ambapo huko itategemea nani mwenye mvuto zaidi na kwa vyovyote ni lazima watagawana ingawa kuna mshindi lazima tapatikana bila kujali ni Zitto ama Dr Slaa"



Huku ni Uongo mkuu. kukubalika kwa Zitto kulitokana na Juhudi za DR. Slaaa,

Wabunge wengi wa Chadema wameongezeka bungezi ni juhudi za DR. Slaa


kanda ya ziwa DR. Slaa anakubalika kuliko mtu yeyote : wazeee kwa vijana , zitto labda akubalike kigoma peke yake na Tena kwenye jimbo lake.


Baada ya DR. Slaa kanda ziwa anayefuata kukubalika ni Maghufuli, ambaye sasa umaarufu wake umeanza kupungua.

Kwa kanda ya ziwa List ya wtu wanokubalika.


DR. Slaaa....60%
Maghuli........15%
Sitta.............12.5%
Zitto..............12.5%

Nyanda za Juu kusini.

DR. Slaaa.........54%
Mwandosya.......30%
Mwakyembe.......11%
Zitto.................05%


Kusini(Lindi,Mtwara)

Membe..........54%
DR. Slaa..........36%
Zitto..............10%

Nyanda za Juu kaskazini
DR. Slaa..........70%

Lowasa...........26%

Zitto............04%

Dar + Pwani

Kikwete......48%

Dr. slaaa......42%

Zitto...........10%

Nyie ndio mnaleta migogoro ya Takwimu nchini, Source yako ni ipi? au unaamka tu na kumwaga data za kichwani mwako apo.
 
Ndani ya chama, Slaa anakubalika makao makuu, Zitto anakubalika matawini.
Slaa anashindwa kusoma alama za nyakati, kushindana na Zitto kunamshusha daraja kila siku hasahasa ndani ya chama.
Kikagula at work this is nasty no one will ever buy this rubbish too late for damage control musitutoshe na ID zenu za kulemba the same Zitto na ID 100 kama Zitto wewe ni mwamba unapanic nini na propaganda za eti unakubalika hapa tuu JF penye wasomi kura ilipitishwa na DR Slaa hata 20 percent hukuipata halafu utuambie kanda ya ziwa unakubalika wapi bwana ,hivi wewe unadhani hii vita ya ushenzi wako utaiweza, huiwezi umerikoroga si kila jambo unalohujumu chama litapita kama unadhani ni upepo huu haupiti ng,o
 
Hamtaki kukubari eheee Mtakubali Subiri muje kuona

Panic panic panic hadi raha i love this the so called Zitto aka Kigagula on run good learn through mistake may be one day you will turn to be a responsible politician not a surpent
 
Sahihisho Dr. Slaa hana kundi, hajawahi kuunda kundi ndiyo maana hakuomba kugombea urais ila aliombwa. Kinyume ni kweli kwa ZZK. Hakuna cha kudadavua ukweli utajitenga
 
Ndani ya chama, Slaa anakubalika makao makuu, Zitto anakubalika matawini.
Slaa anashindwa kusoma alama za nyakati, kushindana na Zitto kunamshusha daraja kila siku hasahasa ndani ya chama.

Mimi huku Arusha Dr. Slaa is the only Presidential Material, au Arusha ni makao makuu ya Chadema.
 
Back
Top Bottom