Ha ha ha ha Mkuu
Kimbunga unajua tafsiri ya yote hayo ni nini?
1.Hatuko salama-Tuliowapa jukumu la kutulinda (Serikali) hawako serious.Mfano rahisi bwana kimunga,wewe uvamiwe lada na majambazi eneo la tabata nyumbani kwako usiku,ukawashtukia majambazi kabla hawajaingia ukwapiga simu polisi,kwanza aidha wasiipokee simu au wakipokea hawatakuja au waje kesho yake.Wana msaada gani sasa.
2.Hakuna wa kumwamini-Sio wanasiasa ,sio wanausalama na sio serikali na sio waandishi wa ajabu.
3.Aidha waandishi wa habari wanatumika vibaya kuilisha jamii sumu.Inawezekana kati ya haya kuna matukio ya kawaidia kabisa mfano kuibiwa laptop but Likakuzwa.Waandishi wa habari wana uwezo mkubwa wa kuiharibu jamii yetu.
Ila kiukweli;HATUKO SALAMA.