Zitto azidi kuwakalia kooni viongozi TPDC

Zitto azidi kuwakalia kooni viongozi TPDC

Donatila

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
8,273
Reaction score
25,297
Zitto-Kabwe--November7-2014.jpg

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe, amesema wanafuatilia kwa Spika wa Bunge ili asaini nyaraka zitakazowezesha kufikishwa mahakamani viongozi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa kukaidi agizo lililowataka wawasilishe mikataba 26 ya gesi asilia mbele ya kamari hiyo ili ikaguliwe.

Wakati Zitto akisema hayo, kuna taarifa kwamba Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), ina mpango wa kuzishughulikia halmashauri zinazotuhumiwa kwa matumizi mabaya ya fedha za umma kwa mtindo unaoendeshwa na PAC.

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), aliyasema hayo alipozungumza na NIPASHE katika viwanja vya Bunge, mjini hapa jana.

Alisema hatua yao hiyo inalenga kudai taarifa za mapitio na mikataba 26 iliyoingiwa kati ya serikali na wawekezaji katika nishati hiyo.

Zitto alisema agizo la PAC kwa TPDC lilitolewa tangu Januari 26 mwaka 2012, lakini hadi sasa halijatekelezwa.

Jumatatu wiki hii, PAC iliamuru polisi kuwaweka rumande Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, James Andilile na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo, Michael Mwanda, kwa kukaidi agizo hilo la PAC.

Andilile na Mwanda walikaa rumande katika Kituo Kikuu cha Polisi jijinu Dar es Salaam kwa saa kadhaa kabla ya kuachiwa bila sharti lolote.

"Kwa sasa tunafuatilia Spika asaini hati ili tuwafikishe mahakamani. Mikataba lazima wataitoa tu," alisisitiza Zitto.


CHANZO:
NIPASHE

http://www.ippmedia.com/frontend/index.php?l=73933
 
Tapeli eliakim maswi akisoma hii mapovu yanamtoka kama nini
 
kwa nini waliachiwa bila masharti kama ni watu wenye hatia? mtuhumiwa ni kunakuwa na masharti fulani ndio unaondoka kituoni kusuburi kitwa mahakamani? hili jambo lina walakinieg. Pr. Muhongo alishawahi kumita zito mlafi wa rushwa, au ndio kitu kinamfanya zito kufuatilia hili jambo kwa nguvu kwa kuwa kuna kitu alinyimwa? kwa nini wizara husika ilishindwa miaka yote hiyo kuchukua mikataba hiyo na Kuiwakilisha bungeni kwa sababu mawaziri wote hawa ni wabunge na wanakutana bungeni, Maswi na zito ni paka na panya. Hawa TPDC wanataka watolewe kafara tu kuna kubwa nyuma ya hili. Ina maana mikataba min gine yote iliwakilishwa kwa kamati kasoro hii tu ya gesi, na kama kuna hitilafu watasitisha hiyo mikataba? sielewi.
 
Mikataba anayo Jk, kwanini kuhangaika na wafuga mbwa wakati mwenye Mbwa yupo? Kila mwenye akili anajua kuwa hakuna mwenye ubavu wa kuzuia mikataba isitoke ila amri ya Raisi kwa watendeji wake. hao akina Andilile kwa ukweli watasumbuliwa tu ila bila ya Boss wao kukubali mikataba itoke tunachezeana akili tu, ndio maana hata kabla ya kufika polisi amri ilitoka ikulu waachiwe mara moja.


"Andilile na Mwanda walikaa rumande katika Kituo Kikuu cha Polisi jijinu Dar es Salaam kwa saa kadhaa kabla ya kuachiwa bila sharti lolote.

“Kwa sasa tunafuatilia Spika asaini hati ili tuwafikishe mahakamani. Mikataba lazima wataitoa tu,” alisisitiza Zitto."


CHANZO: NIPASHE






 
It will take the wind out of everyone's sails. This country is a tragedy, I tell you
 
Na katiba ndio hiyo inarushwa kama tiara....................pathetic
 
Na hizi danadana za mambo kama haya ndio sababu ya kuchakachuliwa kwa katiba ya warioba.
 
Mambo ya kisiasa kuingilia mikataba ya uzalishaji wa gesi asilia, hususan kukamatwa hivi karibuni kwa viongozi wawili wa TPDC baada ya kushindwa kuwasilisha details za mikataba 26 ya Production Sharing Agreements kumeathiri na kuchelewesha kwa uwekezaji wa mabilioni ya Dola za Marekani nchini Tanzania.

Kuna uwezekano wa Kampuni kuahirisha uamuzi wao wa mwisho wa uwekezaji hadi hapo baadaye hali ambayo itaifanya Tanzania kubaki nyuma zaidi ikilinganishwa na Msumbiji ambayo inategemea kuanza kuuza nje ya nchi gesi asilia ifikapo Mwaka 2018.
 
gas haitoki au mkataba hautoki ? ni nini kinachotakiwa kutoka sijaipata kwenye kichwa cha uzi
 
Back
Top Bottom