Zitto awapasua roho wabunge

FJM

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
8,081
6,198
Upinzani dhidi ya nyongeza ya posho za vikao vya wabunge, umechukua sura mpya, baada ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, kuibuka na madai mapya akiitaka serikali kuwaamuru wabunge wote waliolipwa nyongeza hiyo, kuzirejesha mara moja kwa vile bado hazijaidhinishwa na Rais.

Zitto aliibua madai hayo mapya alipokuwa akihutubia katika Harambee ya Sikukuu ya Mavuno-2011 iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Nikolao na Mashahidi wa Afrika-Ilala, la Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam. “Nadhani Mheshimiwa Rais amesikia kilio cha wananchi wake, asiidhinishe nyongeza hiyo ya posho na wale waliolipwa bila kuidhinishwa, waamrishwe kuzirejesha,” alisema Zitto.

Kwa mujibu wa Spika Makinda, posho za wabunge zilipanda mwishoni mwa Mkutano wa Nne wa Bunge, ambapo wabunge walilipwa posho hizo mpya katika vikao vya Novemba 8, 9 na 11, mwaka huu. Hata hivyo, Zitto alisema sababu ya kuongeza posho inayotolewa na serikali haina msingi. “Kwani hali gani ya Mtanzania ni nzuri,” alihoji Zitto na kushangiliwa na umati mkubwa wa waumini waliofurika katika harambee hiyo.

Alisema hapa nchini, mwalimu hulipwa mshahara usiozidi Sh. 150,000 kwa mwezi, lakini katika kikao kimoja cha siku hata kama hatazungumza kitu, mbunge analipwa Sh. 300,000.“Kama huoni kitu hapo, lazima unahitaji maombi,” alisema Zitto, ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Harambee hiyo ililenga kukusanya Sh. milioni 40 kwa ajili ya kuchangia gharama za kuezeka madarasa mawili ya shule ya awali ya Mwidu, iliyoko Chalinze, wilaya ya Bagamoyo, mkoni Pwani, ukarabati wa kanisa hilo, nyumba za watumishi na mazingira yanayolizunguka. Zitto aliahidi kuchangia Sh. milioni 13, mifuko 250 ya saruji na mabati 200 kupitia marafiki zake.

Source:IPPMedia.

Hapo kwenye red: nafurahi kwamba Zitto kawa muwazi na naamini atakubaliana na mimi nikisema wakati umefika sasa kwa bunge kuweka sheria itakayomlazimisha kiongozi yoyote wa umma including mbunge kuweka wazi kila donation wanayopata/kutoa ili kuondoa mianya ya rushwa! Pia hii itapunguza nguvu ya ma-lobbyists wanaochochea upindashaji wa sheria.
 
good to him.
Haitoshi kulalama, je wakati wa majadiliano ya kuongeza posho alipinga kwa kiasi gani?
 
Anaekerwa na posho Chadema ni Zitto Kabwe tu?

FJM
Wazo zuri, kila anatoa chochote ajieleze amezipata wapi ni muhimu kwenye kuweka rikodi ya majumuisha ya kodi ya raia mmoja mmoja pia.
 
Sijaona alichokifanya hapo zaidi ya ww kutaka kumpromote kisiasa

well said, hajamaliza habari yake na Mkulo kadandia lingine.........umelta post nae katumia lugha kali kwa issue ndogo na ilishakua wimbo shv...eti kuwapasua roho wabunge..nakujibu kwa lugha rahisi pia...kama kawapasua roho wenzake basi si mtu mzuri atawa ua...jamanii
 
Kwa upande wangu naungana na Zito kupinga ongezeko hili la posho, kwa ujumla issue sio kiasi wanachopata, issue ni utaratibu uliotumika, kwa hali hii hawatakuwa na uhalali wa kuwahoji wakina Jairo na wenzao kwani posho hizi hazikuwa kwenye bajeti ya mwaka husika na pia hazina idhini ya Raisi kama Ikulu ilivyotoa taarifa yake.
 
Upinzani dhidi ya nyongeza ya posho za vikao vya wabunge, umechukua sura mpya, baada ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, kuibuka na madai mapya akiitaka serikali kuwaamuru wabunge wote waliolipwa nyongeza hiyo, kuzirejesha mara moja kwa vile bado hazijaidhinishwa na Rais.

Zitto aliibua madai hayo mapya alipokuwa akihutubia katika Harambee ya Sikukuu ya Mavuno-2011 iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Nikolao na Mashahidi wa Afrika-Ilala, la Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam. "Nadhani Mheshimiwa Rais amesikia kilio cha wananchi wake, asiidhinishe nyongeza hiyo ya posho na wale waliolipwa bila kuidhinishwa, waamrishwe kuzirejesha," alisema Zitto.

Kwa mujibu wa Spika Makinda, posho za wabunge zilipanda mwishoni mwa Mkutano wa Nne wa Bunge, ambapo wabunge walilipwa posho hizo mpya katika vikao vya Novemba 8, 9 na 11, mwaka huu. Hata hivyo, Zitto alisema sababu ya kuongeza posho inayotolewa na serikali haina msingi. "Kwani hali gani ya Mtanzania ni nzuri," alihoji Zitto na kushangiliwa na umati mkubwa wa waumini waliofurika katika harambee hiyo.

Alisema hapa nchini, mwalimu hulipwa mshahara usiozidi Sh. 150,000 kwa mwezi, lakini katika kikao kimoja cha siku hata kama hatazungumza kitu, mbunge analipwa Sh. 300,000."Kama huoni kitu hapo, lazima unahitaji maombi," alisema Zitto, ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Harambee hiyo ililenga kukusanya Sh. milioni 40 kwa ajili ya kuchangia gharama za kuezeka madarasa mawili ya shule ya awali ya Mwidu, iliyoko Chalinze, wilaya ya Bagamoyo, mkoni Pwani, ukarabati wa kanisa hilo, nyumba za watumishi na mazingira yanayolizunguka. Zitto aliahidi kuchangia Sh. milioni 13, mifuko 250 ya saruji na mabati 200 kupitia marafiki zake.

Source:IPPMedia.

Hapo kwenye red: nafurahi kwamba Zitto kawa muwazi na naamini atakubaliana na mimi nikisema wakati umefika sasa kwa bunge kuweka sheria itakayomlazimisha kiongozi yoyote wa umma including mbunge kuweka wazi kila donation wanayopata/kutoa ili kuondoa mianya ya rushwa! Pia hii itapunguza nguvu ya ma-lobbyists wanaochochea upindashaji wa sheria.

iundwe tume ya wananchi na majaji kuchunguze iweje pesa imetolewa bila kuidhinishwa. nini maana ya kuidhinisha au wabunge walitakiwa waionje posho kwanza halafu walete feedback kwa raisi kwamba posho tamu
 
Anaekerwa na posho Chadema ni Zitto Kabwe tu?

FJM
Wazo zuri, kila anatoa chochote ajieleze amezipata wapi ni muhimu kwenye kuweka rikodi ya majumuisha ya kodi ya raia mmoja mmoja pia.
Gaijin hujui siasa wewe..........ulikuwa unataka wabunge wote wa cdm watoe matamko?

we fanya kazi ulopewa na max bana. achana na siasa, huziwezi, siasa zinataka majibu, sio maswali, and you are full of questions.
 
Warudishe hizo fedha tena haraka sana wevi wakubwa...wanapokeaje bila ya kutafiti kama zimeidhinishwa au la?
 
Hongera Mh. Zito,.lakini hii inchi kumbe haina uongozi kabisa,.Makinda anaruhusu vipi kulipwa posho hawa wabunge wakati hata boss wake JK hajaruhusu?,au ndo kujichukulia sheria mkononi kama polisi wanavyotuzui kila siku? :lol:.
 
We naona umetoka kuzimu! au huu mjadala wa posho tangu umeanza naona haukuwa ndani ya Tanganyika yetu.

Ungeiacha tu sentensi ya kwanza kwamba ametoka kuzimu! Yaani hakuwepo kabisaa duniani kwa kipindi fulani!
 
Back
Top Bottom