EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe alisema mabadiliko hayo ya baraza la mawaziri hayatoi uhalali wa wao kutoa hoja yao ya kutaka waziri mkuu awajibike, bali uamuzi wa pamoja wa wabunge waliotia saini kutaka kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu ndiyo utakaofuatwa.
Alisema kutokana na mabadiliko hayo Bunge limekuwa imara na limeonyesha dhamira ya kweli ya kuisimamia serikali kwa ajili ya maslahi ya wananchi na kwamba sasa taarifa ya CAG itakuwa inathaminiwa kwa kiwango kikubwa.
Ile dharau inayoonyeshwa na mawaziri katika ripoti mbali mbali juu ya wizara zao sasa tunaamini haitakuwepo na wataheshimu maamuzi ya kamati mbali mbali pamoja na taarifa ya CAG, alisema Zitto.
Aliongeza kuwa hatua hiyo ni kuelekea kujenga Bunge imara la kuweza kuwawajibisha watendaji wanaokiuka maadili na kushindwa kulinda mali ya umma.
Filikunjombe aunga mkono
Naye Mbunge wa Ludewa, Deo Fillikunjombe, ambaye katika Bunge lililopita alikuwa miongoni mwa vinara waliotaka mawaziri wawajibishwe kwa maslahi ya taifa alisema hatua hiyo ni nuru njema kwa Watanzania.
Alirejea kauli yake kuwa maamuzi hayo ya kubadilishwa mawaziri ni kutokana na nguvu ya Bunge na kwamba wao walisimamia maslahi ya wananchi.
Alisema ilikuwa ni kawaida kwa serikali kutofanyia kazi maazimio mbalimbali yanayotolewa bungeni na kwamba huo ni mwanzo wa kuhakikisha serikali inatambua kuwa Bunge lipo.
CHANZO: Tanzania Daima
Alisema kutokana na mabadiliko hayo Bunge limekuwa imara na limeonyesha dhamira ya kweli ya kuisimamia serikali kwa ajili ya maslahi ya wananchi na kwamba sasa taarifa ya CAG itakuwa inathaminiwa kwa kiwango kikubwa.
Ile dharau inayoonyeshwa na mawaziri katika ripoti mbali mbali juu ya wizara zao sasa tunaamini haitakuwepo na wataheshimu maamuzi ya kamati mbali mbali pamoja na taarifa ya CAG, alisema Zitto.
Aliongeza kuwa hatua hiyo ni kuelekea kujenga Bunge imara la kuweza kuwawajibisha watendaji wanaokiuka maadili na kushindwa kulinda mali ya umma.
Filikunjombe aunga mkono
Naye Mbunge wa Ludewa, Deo Fillikunjombe, ambaye katika Bunge lililopita alikuwa miongoni mwa vinara waliotaka mawaziri wawajibishwe kwa maslahi ya taifa alisema hatua hiyo ni nuru njema kwa Watanzania.
Alirejea kauli yake kuwa maamuzi hayo ya kubadilishwa mawaziri ni kutokana na nguvu ya Bunge na kwamba wao walisimamia maslahi ya wananchi.
Alisema ilikuwa ni kawaida kwa serikali kutofanyia kazi maazimio mbalimbali yanayotolewa bungeni na kwamba huo ni mwanzo wa kuhakikisha serikali inatambua kuwa Bunge lipo.
CHANZO: Tanzania Daima