Ungejibu ndio au hapana. Naomba usome hapa halafu unieleweshe
The Quran in Sura 23:5-6 says:
5 [Most certainly true believers] . . . guard their private parts scrupulously, 6 except with regard to their wives and those who are legally in their possession, for in that case they shall not be blameworthy. (Sayyid Abul A’La Maududi, The Meaning of the Quran, vol. 3, p. 237)
The key words are "those who are legally in their possession." Maududi (d. 1979) is a highly respected commentator on the Quran, and he interprets the plain meaning of the clause, saying that sex with slave-girls is lawful.
Maududi writes:
Two categories of women have been excluded from the general command of guarding the private parts: (a) wives, (b) women who are legally in one’s possession, i.e. slave-girls. Thus the verse clearly lays down the law that one is allowed to have sexual relation with one’s slave-girl as with one’s wife, the basis being possession and not marriage. If marriage had been the condition, the slave-girl also would have been included among the wives, and there was no need to mention them separately. (Ibid. p. 241, note 7)
The
Mbona umetoka nje ya mada?! Nimekuomba unipe full verse ya hii uliyoita Quran 4:24 na kudai inasema:
'So those of them [women] whom you enjoy, give to them their appointed wages' (4:24).
Hiyo uliyoweka haizungumzii na wala haina uhusiano na mada yako ya Mut'ah marriage au aya niliyokuuliza! Lakini kwavile lengo lako ni issue ya Uislamu na ngono na watumwa, ngoja nikusaidie!
Awali ya yote, Muhammad alishushiwa Quran wakati hao watumwa waemeenea sehemu nyingi tu duniani, na ndio maana, Kutoka 21:20-21 inasema:
Mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na kumwua papo hapo, ni lazima aadhibiwe. Lakini mtumwa huyo akibaki hai siku moja au mbili, bwana wake hataadhibiwa, kwani huyo alikuwa ni mali yake.
Kama ni kushushwa, hiyo Kutoka (Exodus) ilishushwa hata kabla ya Babu ya babu ya babu ya babu yake Mume Muhammada hajazaliwa!!
Hiyo ni kuonesha haya masuala ya watumwa yalikuwepo na yalishadadiwa vile vile na wateule wa Mungu!!!
Na wala usidhani hayo ni ya zama za Taurati na Nabii Musa peke yake, manake hata Mtume Paulo, kupitia Wakolosai 3:22-25 anatuambia:
Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana. Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu. Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana! Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.
Watumwa hao zama hizo za Kristo!!!!
Na hayo yakaendelea hata zama za Muhammad, at least kwa wale wanaomuamini Muhammad na ndipo hapo unapokutana na aya kama hiyo ya 23:5-6!!
Na ilivyo ni kwamba, Quran haikushuka mara moja bali ilishuka kidogo kidogo kwa miaka 23, na ndio maana wakati unaona hiyo aya hapo juu inatoa ruhusa ya Master kumwingilia Mtumwa wake, ukirudi kwenye ile sura niliyokuambia awali, yaani Q 4:25 inasema
Na miongoni mwenu asiyeweza kupata mali ya kuoa wanawake waungwana, waaminio, basi (aoe) katika wajakazi waaminio iliyowamiliki mikono yenu ya kuume, na Mwenyezi Mungu Anajua sana imani yenu...
Na English version yake inasema:
And whoever among you cannot [find] the means to marry free, believing women, then [he may marry] from those whom your right hands possess of believing slave girls. And Allah is most knowing about your faith.
Na kadri Quran ilivyokuwa inashuka, ikafika hapa kupitia Quran 24:32-33:
Na waozeni wajane miongoni mwenu, na walio wema katika watumwa wenu, na wajakazi wenu; kama mtakuwa mafakiri Mwenyezi Mungu Atawatajirisheni katika fadhili Zake; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa, Mwenye kujua.
Na washike utawa wale wasiopata kuoa mpaka Mwenyezi Mungu Awatajirishe katika fadhili Zake. Na wale wanaotaka hati katika wale inayowamiliki mikono yenu ya kuume, basi waandikieni, kama mkiona wema kwao. Na wapeni katika mali ya Mwenyezi Mungu Aliyowapeni. Wala msiwashurutishe vijana wenu wa kike kufanya ukahaba kama wakitaka kukaa utawani, ili kutafuta vifaa vya maisha ya dunia. Na Atakayewashurutisha, basi hakika Mwenyezi Mungu baada ya kushurutishwa kwao ni Msamehevu, Mrehemevu.
Kwamba, watumwa wale wale ambao hawakuwa na haki yoyote, hatimae Quran inashusha aya kwa kuwataka Masters wawaoze watumwa wao, na kwa wale watumwa ambao hawatadondokewa na ngekewa hii ya ndoa, basi wa-abstain!
Na ikiwa miongoni mwa hao watumwa, watatokea wengine wa kutaka kuwa huru (wanaotaka hati), basi mkiona kwa wema waliowafanyia, wapeni hati (mkataba wa kuachiwa huru)!
Kwahiyo funzo lingine hapo, unaposoma Quran ni lazima pia ufahamu Quran haikushuka mara moja! Na usipofahamu aya ipi ilishuka wakati gani na kwa dhima ipi, basi mtu ataishia kupotosha tu! Na ukweli ni kwamba, Waislamu wengi huwa hatufahamu hili na ndio maana inakuwa rahisi sana ku-brainwash watu kiasi cha kukubali kwenda kujilipua na kuua baada ya kushuhudiwa Aya za kwenye Quran bila kufahamu aya husika ilishuka lini na kwa madhumuni gani!!!
Hatulifahamu kwa sababu majority ya Waislamu Quran hatuijui, na wanaoijua wameipitia juu juu tu kwa kumaliza Juzuu mbili tatu lakini na hata wale waliokung'uta Juzuu zote 30, majority hawajasoma Theology!
Whether you're a Muslim or Christian, usiposoma theology utaishia kukariri tu maandiko bila kufahamu dhima ya kile neno!!! Mkristo atadhani Bible anaijua, kumbe haijui sawa sawa na hali kadhalika Mwislamu atadhani Quran anaijua kumbe anachojua ni kuisoma/kuikariri tu na kuitafsiri!