ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Pia kuna Washirika Tanzania Stars Band.....

Bendi hii ilikuwa ikimilikiwa na Jumuiya ya Washirika Tanzania na iliundwa na wanamuziki wengi waliojiengua kutoka Orchestra Vijana Jazz,iliundwa mwaka 1989 na ilikuwa ikitumia mtindo wa Watunjatanjata(Watanzania tuondoe njaa Tanzania) na baadae wakajiita Njata one....

Bendi hii ilikuwa ikifanya maonesho yake katika ukumbi wa 92 Hotel pale Sinza Shekilango...Ilikuwa ni bendi kali hasa na ilikuwa ni tishio kwa bendi zilizotamba enzi zake hasa Vijana Jazz...

Bendi hii ilitamba na nyimbo kama Yaliyopita si ndwele(Nimekusamehe lakini sitokusahau),Washirika,Nelson Mandela,Julie,Penzi la ulaghai,Nimebaki nashangaa,Spare tyre,Maeliza,Gubu la wifi zako,Zuhura,Umbea,Watoto wamekuja juu,Masumanda,Kissa,Kayumba na nyingine kali....

Bendi hii iliundwa na wanamuziki wengi waliojiondo Vijana Jazz kama Hamza Kalala 'Komando',Eddy Sheggy,Mhina Panduka 'Toto Tundu',Adam Bakari 'Sauti ya Zege' bila kuwasahau Abdul Salvador 'Father Kidevu',Emma Mkelo 'Lady Champion',Robert Mabrish,Zahir Ally Zorro,Madaraka Morris 'Kiwembe' ,

Baadae mwaka 1991 baadhi ya wanamuziki wakiongozwa na Hamza Kalala na Eddy Sheggy na kwenda kuunda bendi mbili tofauti za Bantu Group Band(wana Kasimbagu Kahabuka) na MCA International(wana Munisandesa) na wengine(Eddy Sheggy na wenzake) walihamia Bima Lee Orch. wana Magnet Tingisha.....Hiii iliifanya Watunjatanjata itetereke kidogo hadi mwaka 1992 ilipompata mtaalam Zahir Ally Zorry ambaye aliifanya ikabaki imara na mtindo wa Watunjatanjata waliouboresha na kuwa Njata One wakiwa na nyimbo kama Gubu la Wifi zako,Maeliza,Zuhura na Umbea
Huu zuhura, ambao Laddy Champion, mzee Zahir alihama nao toka J.KT. Ruvu, uko vizuri mkuu.
 
Vijana wa zamani mnaojua vitu. Bado wimbo wenye maneno haya sijaupata na kama mliutuma sijaziona.
Maneno yake ni hivi
Nakwenda ilula kwa wakwe zangu wakanieleza, na maneno mengi ya kwamba yeye ana uwezo
"Leo isiwe sababu ya kunitangaza mimi eehe na kuniaharibia jina langu ehe toto tundu.
Penzi langu la kusuasua
 
Sijui unaishi wapi, ila kama unaishi dar, huo wimbo utaupata pale, temeke mwisho, zinaposhusha basi za kusini, Wale wananyimbo nyingi za zamani. nikikosa wimbo mtandaoni naenda pale, nyimbo nyingine mtandaoni huwa haziimbi mpaka mwisho.
Nisaidie namba zao,,inbox.
 
29 January 2023
Wanamuziki nguli wanaounda kundi la Maquis Original na staili yao ya Sendema ya Motoo wakitumbuiza katika onesho lao la Re-Union ukumbi wa Ngalawa katika hoteli ya Royal Village jijini Dodoma Ijumaa January 28, 2023

Vumbi Dekula Kahanga, Nkashama Kanku Kelly, Mukumbule Parash, Tshimanga Asossa, Chimbwiza Mbangu ‘Nguza Vicking’ Big Sound, Abuu Omari .....
Source : Muhidin Michuzi
 
Hii ndio Taarifa iliyotufikia hivi punde , na kwamba Mzee Hussein Jumbe amefikwa na umauti katika Hospitali ya Amana Jijini Dar es Salaam leo 10/4/2023

Enzi za Uhai wake aliwahi kutumikia bendi za DDC MLIMANI PARK na MSONDO NGOMA

Aliwahi kutamba na Kibao chake cha "Nachechemea"

Apumzike kwa Amani .
 
Mkuu SI WAZURI BINADAMU imeimbwa na BICHUKA lakini akiwa na OSS sio MLIMANI PARK. "Ninakushukuru Mungu huso mshirikae kuiponya roho yangu ilotaka toweka binadamu madhurumu ana vituko vya sumu anavituko vya sumu kali kushinda ya nyokae si wazuri binadamu usione wachekaa ooh nhon."
"si wazuri binadamu usione wafurahi"

"Mtendee la muhimu hatoridhika, akisha kusalimu moyoni akasirika"

Ooohhh.

Bonge la Wimbo.
Hapa ni wakati wa vijembe. Baada ya kuimba wimbo huu Bitchuka akiwa OSS ndio ukawa mwisho wa vijembe kutoka Juwata.
 
"si wazuri binadamu usione wafurahi"

"Mtendee la muhimu hatoridhika, akisha kusalimu moyoni akasirika"

Ooohhh.

Bonge la Wimbo.
Hapa ni wakati wa vijembe. Baada ya kuimba wimbo huu Bitchuka akiwa OSS ndio ukawa mwisho wa vijembe kutoka Juwata.
Hana wemaa usimwone kucheka oooh

Mtendee wemaa lakini hatoridhikaaa

Apita kusalimu moyoni kakasirikaaaa
 
wakuu umoufia kwenu,naomba please anajua pa kuupata au mwenye nao huu wimbo "chaupele mpenzi"

waniambia niliwache rhumba nami sikuzoea,sitaweza kuliacha rhumba sababu yakooo..aisee mwenye nao anisaidie nimeutafuta sana,nikachoka ila jana bongo radio online wakaupiga ,nimepata mzuka wakuutafuta tena
 
Twende na wimbo wa "Mtu ni afya mwananchi elewa eeh, tusiwe wavivu kuzijenga vyema afya zetu"

Mwenye kujua ni bendi gani iliyoimba wimbo huu aniambie pliz. Na pia kama kuna mtu anao basi atuwekee hapa tafadhalini.
 
Twende na wimbo wa "Mtu ni afya mwananchi elewa eeh, tusiwe wavivu kuzijenga vyema afya zetu"

Mwenye kujua ni bendi gani iliyoimba wimbo huu aniambie pliz. Na pia kama kuna mtu anao basi atuwekee hapa tafadhalini.
Daaaah,umenikumbusha mbaaali enzi hizo RTD tu akina Juma ngondae.
 
We acha tu ndugu yangu, kuna nyimbo mtu ukizisikia lazima utoe chozi bila kujijua.
Nautafuta sana mwimbo huu.
Na hisi na huu utakua unaujua[emoji1787]

"Na vijijini oooh ni kiswahili chatumika×2

Kiswahili lughaaa ya Taifaaaa.

[emoji13][emoji13]
Mwingine,,,,Tusilime tulivyozoea,tutumie mbolea,Kwa maagizo ya wataalamuu,njaa haitatokea.
 
Vijana wa zamani mnaojua vitu. Bado wimbo wenye maneno haya sijaupata na kama mliutuma sijaziona.
Maneno yake ni hivi
Nakwenda ilula kwa wakwe zangu wakanieleza, na maneno mengi ya kwamba yeye ana uwezo
"Leo isiwe sababu ya kunitangaza mimi eehe na kuniaharibia jina langu ehe toto tundu.
Penzi langu la kusuasua
Huu wimbo kama sikosei umeimbwa na Washirika Tanzania Stars, Njata one,
waimbaji Muhina Panduka 'Toto Tundu', Mohamed Shaweji, Adam Bakar, Madaraka Moris 'Kiwembe' na wengineo.

Naweza kurekebishwa.
 
Habari
Naomba kufaham jina la nyimbo ya jagwa music kuna mistar kadhaa naikumbuka
"Habar za saahiz kwanza nakusalimia
Kusahau mi siwez,sababu nazingatia
Siyo wewe mpuuz
Ahsante
 
wakuu umoufia kwenu,naomba please anajua pa kuupata au mwenye nao huu wimbo "chaupele mpenzi"

waniambia niliwache rhumba nami sikuzoea,sitaweza kuliacha rhumba sababu yakooo..aisee mwenye nao anisaidie nimeutafuta sana,nikachoka ila jana bongo radio online wakaupiga ,nimepata mzuka wakuutafuta tena

Wanaitwa Them Mushrooms - Itawezakanaje
 
Mwenye Audio_Kisiki cha mpingo_ wa Mchinga sound band
Au wimbo wowote ule wa mchinga Sound kuanzia miaka ile 2000....
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Mwenye anafaham jina la hii mp3/beat anisaidie, Na kama unayo full ukaitupia hapa itakua makini zaidi.
 
Atakayenipatia wimbo wa tofii mvambe chini ya mokibo sound unoitwa mosesengo zawadi yake no no sana
 
Back
Top Bottom