Giro
JF-Expert Member
- Feb 9, 2009
- 359
- 22
Theopista Nsanzugwanko
Daily News; Monday,March 16, 2009 @18:50
Polisi leo inaanza operesheni maalumu ya kukagua na kukamata daladala, kubaini watakaotoza nauli kinyume na utaratibu ili wachukuliwe hatua za kisheria. Operesheni hiyo ya wiki mbili, inaendeshwa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), Kanda ya Mashariki na Pwani.
Katika mkutano na waandishi wa habari leo, Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda ya Dar es Salaam, Mohamed Mpinga, alisema miongoni mwa adhabu zitakazotolewa kwa watakaobainika, ni pamoja na kunyang'anya leseni za biashara kwa siku 15.
Mpinga alisema kutoza nauli kubwa au kujaribu kufanya mgomo baridi kwa baadhi ya wamiliki wa daladala kwa kisingizio cha kushuka nauli, ni kinyume na sheria ya leseni zao. Kutokana na kuwapo taarifa za baadhi ya madereva na makondakta kukaidi kutoza nauli mpya, Mpinga alitoa namba za simu yake ya mkononi akiwataka wananchi kuwasiliana naye kutoa taarifa ya gari linalohusika.
Namba hizo ni 0754 360046 na 0713 635799. Vilevile alitoa namba za wakuu wa Usalama Barabarani katika Mikoa ya Kipolisi ambazo ni Ilala 0784 304158, Kinondoni 0755624243 na Temeke 0713 260888.
Ofisa Mfawidhi wa SUMATRA, Kanda ya Mashariki na Pwani, Walukani Luhamba, alisema wameamua kunyang'anya leseni kwa watakaokutwa na makosa hayo kutokana na uzoefu uliopo kwamba wakitozwa faini, huendelea kutenda makosa.
Alisema Sumatra imekuwa ikifanya ukaguzi mara kwa mara tangu kushuka kwa nauli na kukamata baadhi ya mabasi ambayo wamiliki walilipa faini kwa kuwatoza abiria nauli kubwa lakini sasa watawanyang'anya leseni. Alisisitiza kupelekwa kwa mabasi hayo katika Chuo cha Ufundi VETA kuandikiwa nauli mpya ubavuni, akisema mabasi machache ndiyo yalitekeleza hilo. Hivi karibuni, Sumatra ilishusha nauli za mabasi ya mikoani na daladala. Kwa upande wa Dar es Salaam, ilishusha nauli ya daladala kwa asilimia 12 ambayo ni sawa na Sh 50.
...................................
Ila kwa tabia ya wadanganyika watakubali vitisho vya makonda hata kama ni haki yao.
Daily News; Monday,March 16, 2009 @18:50
Polisi leo inaanza operesheni maalumu ya kukagua na kukamata daladala, kubaini watakaotoza nauli kinyume na utaratibu ili wachukuliwe hatua za kisheria. Operesheni hiyo ya wiki mbili, inaendeshwa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), Kanda ya Mashariki na Pwani.
Katika mkutano na waandishi wa habari leo, Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda ya Dar es Salaam, Mohamed Mpinga, alisema miongoni mwa adhabu zitakazotolewa kwa watakaobainika, ni pamoja na kunyang'anya leseni za biashara kwa siku 15.
Mpinga alisema kutoza nauli kubwa au kujaribu kufanya mgomo baridi kwa baadhi ya wamiliki wa daladala kwa kisingizio cha kushuka nauli, ni kinyume na sheria ya leseni zao. Kutokana na kuwapo taarifa za baadhi ya madereva na makondakta kukaidi kutoza nauli mpya, Mpinga alitoa namba za simu yake ya mkononi akiwataka wananchi kuwasiliana naye kutoa taarifa ya gari linalohusika.
Namba hizo ni 0754 360046 na 0713 635799. Vilevile alitoa namba za wakuu wa Usalama Barabarani katika Mikoa ya Kipolisi ambazo ni Ilala 0784 304158, Kinondoni 0755624243 na Temeke 0713 260888.
Ofisa Mfawidhi wa SUMATRA, Kanda ya Mashariki na Pwani, Walukani Luhamba, alisema wameamua kunyang'anya leseni kwa watakaokutwa na makosa hayo kutokana na uzoefu uliopo kwamba wakitozwa faini, huendelea kutenda makosa.
Alisema Sumatra imekuwa ikifanya ukaguzi mara kwa mara tangu kushuka kwa nauli na kukamata baadhi ya mabasi ambayo wamiliki walilipa faini kwa kuwatoza abiria nauli kubwa lakini sasa watawanyang'anya leseni. Alisisitiza kupelekwa kwa mabasi hayo katika Chuo cha Ufundi VETA kuandikiwa nauli mpya ubavuni, akisema mabasi machache ndiyo yalitekeleza hilo. Hivi karibuni, Sumatra ilishusha nauli za mabasi ya mikoani na daladala. Kwa upande wa Dar es Salaam, ilishusha nauli ya daladala kwa asilimia 12 ambayo ni sawa na Sh 50.
...................................
Ila kwa tabia ya wadanganyika watakubali vitisho vya makonda hata kama ni haki yao.