Zijue faida za Mmea wa Mlonge, Jitibu magonjwa 300 kwa kutumia mlonge

G.MWAKASEGE

Senior Member
Jun 29, 2007
153
15
Tulikuwa na family day na haya ndio niliyoambulia nikaona they are good news worth sharing.

View attachment The Moringa Oleifera Tree.doc

======================


 
Mapishi Mbali mbali ya mmea wa mlonge

10. MLONGE (MORINGA)



Majina ya Kiswahili Mlonge, Mzunze
Kingereza: Radish tree
Jina la Kisayansi: Moringa Oleifera


Matumizi ya Moringa

Katika nchi ya Tanzania moringa huota vyema lakini huliwi kwa wingi kwani watu hawana elimu ya kutosha kuhusu utayarishaji wake. Majani mabichi na makavu, matunda machanga, mizizi na maua yaweza kutumiwa katika upishi na dawa. Majani pia hutumiwa kama malisho kwa wanyama, chavua la maua huwavutia nyuki kwa minajili ya utoaji wa asali,hutumika katika utengenezaji wa sabuni na vyombo vingine vya urembo.

Faida yake mwilini

Majani na maua ya Moringa yanavirutubisho vingi kama vitamin A (mara tatu zaidi ya karoti), vitamin C (mara tatu zaidi ya ile ya machungwa), calcium
(mara 140 zaidi ya ile inayopatikana katika maziwa ya ngombe) na potasiamu. Umetumika katika kusaidia udhibiti wa matatanisho yanayoletwa na ugonjwa wa ukimwi.


Inakostawi

Nchi zote za joto tropics na subtropics, sana sana katika sehemu za pwani, hupendelea mwinuko wa kati ya 0-500m. Hustawi sana sehemu za Ukanda wa
Bahari ya Hindi. Asili ya mmea wa Moringa ni wenyeji wa sehemu ya Sub Himalaya kaskazini magharibi mwa nchi ya India.


Uhifadhi wa majani ya moringa Majani ya Moringa hukaushwa na kusagwa ili kutengeneza unga ambao huongezwa kwenye chakula kama viazi vilivyosetwa na uji wa mahindi ama mtama ili kuongeza ubora wake.

Mapishi mbalimbali ya Mlonge

Majani ya mlonge na maharagwe

VIAMBA UPISHI

Majani ya mlonge 2 vikombe
Nyanya 1 kubwa
Kitunguu saumu 3-4 punje
Kitunguu maji 1 kikubwa
Chumvi 1⁄2 kijiko cha chai.
Mafuta ya maji 2 vijiko vya kulia chakula
Tui la nazi 1⁄2 kikombe cha chai
Maharage 1 Kikombe
Nyama/samaki/kuku 1 kikombe cha vipande
vilivyokatwakatwa ili viwe vidogo


HATUA ZA MAPISHI

1. Chemsha maharage na kuku /nyama ya ngombe/ samaki mpaka iive.

2. Osha majani ya moringa vizuri, ondoa sehemu zisizohitajika na ukatakate.

3. Ambua, osha na ukatakate kitunguu maji na ukaange hadi kilainike.

4. Ambua, osha na uponde kitunguu saumu na uongeze kwenye kitunguuu maji.

5. Osha na ukatakate nyanya, ongeza kwenye mchanganyiko na uendelee kukaanga.

6. Ongeza majani ya moringa kwenye mchanganyiko,koroga na uendelee kukaanga.

7. Ongeza chumvi na upike hadi mboga zote ziive vizuri.

Chakula hiki cha majani kinaweza kuliwa pamoja na ugali, wali, na vyakula vinginevyo.

Mlonge na Matembele

VIAMBA UPISHI

Majani ya Mlonge 2 Vikombe
Matembele 2 Fungu
Mafuta ya kupikia 3 Vijiko vya kulia
vilivyosagwa 1 Kijiko cha chai

Kitunguu maji 1
Vitunguu saumu 3-4 punje
Nyanya 1
Karoti ndogo 1
Tui la nazi 1⁄2 kikombe cha chai
Chumvi 1⁄2 kijiko cha chai.


HATUA ZA MAPISHI

1. Osha Moringa na Matembele vizuri huku ukitoa sehemu zisizo hitajika.

2. Tayarisha tui la nazi na upashe moto kwenye sufuria tofauti.

3. Ambua kitunguu maji, vitunguu saumu na karoti na uoshe pamoja na nyanya.

4. Katakata kitunguu, nyanya na karoti na uponde vitunguu saumu.

5. Pasha mafuta moto kwenye sufuria na ukaange kitunguu maji hadi kilainike.

6. Ongeza karoti na nyanya, koroga hadi mchanganyiko uwe laini. Ongeza chumvi na kitunguu saumu na ukoroge.

7. Ongeza tui moto la nazi na ukoroge hadi kufikia kuishia tui.

Mboga hii yaweza kuliwa na ugali, mihogo, wali na vyakula vinginevyo.
 
Naomba kujua mlonge unasaidiaje kama tiba? wenye kujua naomba mtuhabarishe.

=============

MTI WA MLONGE WENYE MAAJABU NA FAIDA ZAKE ZAIDI YA KUMI.

Eileen Kasubi ni mtanazania wa kwanza mwanamke ambaye ni mjasiriamali wa kazi za mikono aliyefanikiwa kufanya utafiti juu ya mti MLONGE ambao umekuwa na faida kubwa hapa nchini na kufanikiwa kuzitambua zaidi ya faida kumi za mti huo unaopatikana kwa uchache hapa Tanzania.

Mjasiriamali huyu anaweka wazi namna ya MLONGE ulivyokuwa na faida lukuki lakini kubwa kuliko yote ni kwamba watanzania wengi bado hawajazitambua faida za mti huu ambao ni adimu kwa kiasi fulani hapa Tanzania licha ya wajasiriamali hawa kuhamasisha.

Bi. Kasubi anasema MLONGE ni mti wenye maajabu hasa katika matumizi yake kuanzia majani yake, magome,mbegu ambazozimekuwa zikitoa tiba, kinga pamoja na lishe, haya ndiyo maajabu ya mtyi MLONGE.

KAMPUNI YA Makai Moringa Enterprises inayodiri na mkakati huu wa kutafiti kwa kina zaidi juu mti Mlonge, Bi. Kasubi ambaye ni mkurugenzi wa Makai Moringa, anasema kwa miaka mingi akishirikiana na wafiti wenzake ambao ni wajasiriamali kutoka nchini Malawi na Kenya, wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuzitambua faida ya mti huo na hivi sasa wanachopigania ni mtaji mkubwa ambao utaweza kuwaendeleza wajasiriamali wanaotafiti baadhi ya matumizi ya miti hapa Tanzania.

Mkurugenzi Kasubi anasema mafanikio ambayo anajivunia kuyapata katika utafiti wake juu ya mti huo Mlonge ni pamoja na kufanikiwa kuutambua kuwa ni miongoni mwa miti ambayo inatibu baadhi ya maradhi sugu kama vile ugonjwa wa kisukari ambao umekuwa tatizo katika maisha ya jamii ya ya kitanzania.

Bi.Eileen Kasubi anazianisha bidhaa zake zitokanazo na mti huo wa MLONGE ambapo anasema mafanikio ya mti huo na faida zake ni kama ifuatavyo: Majani ya mti wa MLONGE yakisagwa unga wake hutumika kwa lishe ya mwanadamu.

Anaendelea kusema katika hayo majani pia bado yanaweza kutibu na kukinga maradhi zaidi ya magonjwa 300 kitu ambacho unaonyesha maajabu ya kutibu na kutumika kama lishe.

Si hivyo tu, unga huo wa mlonge bado unanafasi kubwa kulinda afya ya mwanadamu pamoja na kurutubisha mifumo mbalimbali ya mwili
hapo ndipo utagundua MLONGE ni mti wa maajabu.

FAIDA ZA MBEGU ZAKE

Mbegu za Mlonge hutibu maradhi kama Malaria, Saratani ya tumbo, hupunguza sonona stress, huleta hamu ya kunywa maji, huongeza kinga ya mwili CD4s,

Mbegu hizo za mti huo wa ajabu bado zinahamasisha jamii kuamka na kuutambua umuhimu wa mti MLONGE kwa mbegu hizo hutoa mafuta ya kupikia pamoja na mafuta ya kujipaka mewilini kwa nyakati tofauti.

Kwa upande wa mafuta ya kupikia chakula Bi. Kasubi anasema mafuta yake ya kupikia huua sumu kwenye chakula yaani Bacteria na huondoa cholesterol. Mafuta ya kupaka mwilini yaani (Moringa Skin Care Oil).

Mlonge unaendelea kutoa faida kemkem kwa mtanzania na jamii yote duniani kwani umeweza kuwapendelea na wanamichezo kwa kutoa mafuta ambayo yanachua pindi mchezaji anapokuwa ameshikwa na misuli wakati akiwa anacheza, Bi. Kasubi anaainisha kwamba katika utafiti wa kampuni yake amefanikiwa kutambua faida nyingine ya matumizi ya mti huo baada ya kufanikiwa kutengeneza mafuta ya kuchua na kuondoa maumivu yatokanayo na kukaza kwa misuli ya mwili yaani (MORINGA MASSEGE OIL)ambayo huondoa maumivu ya mgongo, kiuno, miguu, hutibu baridi, na hupasha misuli joto.

Bado mti huo unazidi kushika nafasi za juu kabisa hasa pale mtafiti huyu mwanamke ambaye amepigana kwa miaka minane sasa tangu aanze kufanya utafiti kabla ya kuungana na wajasiriamali wenzake, pia amefanikiwa kugundua kuwa MLONGE unao uwezo wa kutoa sabuni za aina mbalimbali zikiwemo (Toilet soap) na kutibu magonjwa mengine mbalimbali kama vile ugonjwa wa ngozi, fangazi, chunusi, mba na hulinda ngozi kwa ,muda mrefu.

Kama hiyo haitoshi, bado mti wa mlonge unaendelea kutetea miti mingine ambayo bado haijafanyiwa utafiti na kampuni hiyo, Bi. Kasubi anasema katika utafiti wake amegundua kuwa mti wa MLONGE umeweza kutoa mafuta ya kupaka kwenye nywele na huiimarisha nywele vilivyo na kuzifanya kuwa na rutuba tofauti na mafuta mengine yatumikayo hapa nchini, huu ni MTI WA MAAJABU MLONGE, amesema Eileen Kasubi Mkurugenzi wa Makai Moringa (Mlonge) anayepatikana katika jengo la Pamba House karibu na Imalaseko Posta mjini Dar es Salaam.

 
MLONGE
Unga wa majani ya Mlonge ambao ni lishe, tiba na kinga hutibu magonjwa kama shinikizo la damu,kupooza viungo au kufa ganzi,homa ya matumbo(typhoid),kuwashwa mwili,vidonda vya tumbo,malaria sugu, enia, upele n.k.

Mbegu za Mlonge hutibu Malaria, Saratani ya tumbo,hupungusa sonona stress, huleta hamu ya kunywa maji,huongeza kinga ya mwili CD4s. (Tumia mbegu 3x3 muhimu kila ukitafuna mbegu tatu kumbuka kutumia maji glass 3 au zaidi)

Maganda(magome) ya Mlonge husaidia kusafisha maji(water treatment).

Mizizi hutumika kutibu watu walio na malaria sugu au watu wanaopata homa ya usiku au wanaotiririka sana jasho wakati wa homa. Mizizi hutumika kwa kusaga unga wake na kutumia kijiko cha chai mara tatu kwa siku.

Pia mgonjwa anatakiwa kutafuna mbegu tatu mara tatu kwa muda wa siku arobaini na tano sawa na wiki sita.

Unahamasishwa na kushauriwa angalao nyumbani kwako uwe na mashina kadhaa ya mmea huu kwa matumizi yako.
 

Attachments

  • moringa.docx
    29.4 KB · Views: 961
[h=6]DRUMSTICK TREE Overview Information[/h]Drumstick tree is a plant that is native to the sub-Himalayan areas of India, Pakistan, Bangladesh, and Afghanistan. It is also grown in the tropics. The leaves, bark, flowers, fruit, seeds, and root are used to make medicine.

Drumstick tree is used for "tired blood" (anemia); arthritis and other joint pain (rheumatism); asthma; cancer; constipation; diabetes; diarrhea; epilepsy; stomach pain; stomach and intestinal ulcers; intestinal spasms; headache; heart problems; high blood pressure; kidney stones; fluid retention; thyroid disorders; and bacterial, fungal, viral, and parasitic infections.

Drumstick tree is also used to reduce swelling, increase sex drive (as an aphrodisiac), prevent pregnancy, boost the immune system, and increase breast milk production. Some people use it as a nutritional supplement or tonic.

Drumstick tree is sometimes applied directly to the skin as a germ-killer or drying agent (astringent). It is also used topically for treating pockets of infection (abscesses), athlete's foot, dandruff, gum disease (gingivitis), snakebites, warts, and wounds.

Oil from drumstick seeds is used in foods, perfume, and hair care products, and as a machine lubricant.

Drumstick tree is an important food source in some parts of the world. Because it can be grown cheaply and easily, and the leaves retain lots of vitamins and minerals when dried, the drumstick tree is used in India and Africa in feeding programs to fight malnutrition. The immature green pods (drumsticks) are prepared similarly to green beans, while the seeds are removed from more mature pods and cooked like peas or roasted like nuts. The leaves are cooked and used like spinach, and they are also dried and powdered for use as a condiment.

The seed cake remaining after oil extraction is used as a fertilizer and also to purify well water and to remove salt from seawater.


[h=4]How does it work?[/h]Drumstick tree contains proteins, vitamins, and minerals. As an antioxidant, it seems to help protect cells from damage.
TAKEN BY MOUTH
  • "Tired blood" (anemia).
  • Arthritis.
  • Asthma.
  • Cancer.
  • Constipation.
  • Birth control.
  • Diabetes.
  • Diarrhea.
  • Epilepsy.
  • Stomach pain (gastritis).
  • Stomach and intestinal ulcers.
  • Headache.
  • Heart problems.
  • High blood pressure.
  • Kidney stones.
  • Swelling (inflammation).
  • Thyroid disorders.
  • Infections.
  • Increasing breast milk production.
  • As a nutritional supplement.
  • Stimulating immunity.
  • Increasing sex drive.
  • Other conditions.
APPLIED TO THE SKIN
  • Athlete's foot.
  • Dandruff.
  • Warts.
  • Skin infections.
  • Snakebites.
  • Gum disease (gingivitis).
  • Other conditions.
More evidence is needed to rate the effectiveness of drumstick tree for these uses.


[h=6]DRUMSTICK TREE Side Effects & Safety[/h]
Drumstick tree leaves, fruit, and seeds might be safe when eaten as food. However, it's important to avoid eating the root and its extracts. These parts of the plant may contain a toxic substance that can cause paralysis and death.

There isn't enough information to know if drumstick tree is safe when used in medicinal amounts. [h=4]Special Precautions & Warnings:[/h]Pregnancy and breast-feeding: It's UNSAFE to use drumstick tree if you are pregnant. Chemicals in the root, bark, and flowers can make the uterus contract, and this might cause a miscarriage.

It's also best to avoid drumstick tree if you are breast-feeding. There isn't enough information to know whether it is safe for a nursing infant.
[h=6]DRUMSTICK TREE Interactions [/h]We currently have no information for DRUMSTICK TREE Interactions

[h=6]DRUMSTICK TREE Dosing[/h]The appropriate dose of drumstick tree depends on several factors such as the user's age, health, and several other conditions. At this time there is not enough scientific information to determine an appropriate range of doses for drumstick tree. Keep in mind that natural products are not always necessarily safe and dosages can be important. Be sure to follow relevant directions on product labels and consult your pharmacist or physician or other healthcare professional before using.

READ ALSO Trees for Life Journal - Moringa oleifera: A Review of the Medical Evidence for Its Nutritional, Therapeutic, and Prophylactic Properties. Part 1.
 
hi!i kindly request NGOSHWE to put in swahili the uses of Moriga oliefera so that most tanzanian can understand its usefulness.its a movolous lecture i benefited alot.
its true that this forums is of great thinkers...pull it up
 
hi!i kindly request NGOSHWE to put in swahili the uses of Moriga oliefera so that most tanzanian can understand its usefulness.its a movolous lecture i benefited alot.
its true that this forums is of great thinkers...pull it up

Sasa unamshauri mwenzako atumie kiswahili wakati huo huo wewe mwenyewe umetumia kiingereza.
 
Nimesikia mengi kuhusiana na mti wa Mlonge lakini hii ni kali zaidi
CAPE TOWN, (IPS). Wakati tatizo linalipolikabili Bara la Afrika, watu wanaangalia uwezekano wa kupata misaada kutoka kwenye mashirika ya kimataifa kutoka nje ya bara hilo.

Lakini hali ya ukame inayoongezeka kwa kasi, miti yenye kuhimili ukame huku ikiwa na majani yenye viini lishe vingi inaweza kuwasaidia watu maskini, pia maeneo ya usalama wa chakula na utapiamlo, wao wenyewe.

Shamba lenye hekta 15 lilipandwa miti ya Mlonge au wengine huuita mti wa miujiza ambao kwa Kiingereza unaitwa Moringa Oleifera, tayari umeshaanza kuleta mabadiliko katika jimbo moja maskini zaidi la Afrika Kusini la Limpopo.

Majani ya Mlonge yamepachikwa jina la chakula chenye viwango kwasababu wanasayansi waligundua yana kiasi cha madini ya Kalisium yanayoweza kupatiakana katika glasi nne za maziwa, kiasi cha vitamini c inayopatikana kwenye machungwa saba, Potasium ya kwenye ndizi mbivu tatu. Pia unapata kiasi cha madini ya chuma mara nne zaidi ya kiasi kile kinachopatikana kwenye spinachi. kiasi cha vitamani A mara nne zaidi ya kile kinachopatikana kwenye karoti na kiasi cha protini mara mbili zaidi ya kile kinachopatikana kwenye maziwa. Ukiwa na mti wa Mlonge ni sawa na kuwa na Supermarket kwenye mti.
Mavis Mathabatha aliyewahi kuwa mwalimu kutoka Tooseng, amekuwa akifanya bidii ya kufungua mashamba ya Mlonge kwa kipindi cha miaka mitatu sasa ambalo litamuwezesha kuzalisha majani ya kutosha ya Mlonge ili kusaidia kuleta mabadiliko katika jamii yake.
"Nataka kuleta mabadiliko katika jimbo langu na nchi nzima kupitia mradi huu," alisema.
Mwaka 2009, alianza kuvuna na kuyakausha na kisha kuyasaga majini ya Mlonge kutoka kwenye miti michache aliyokuwa ameipabnda.
Unga huo wa Mlonge alikuwa ukiwachanganyia watoto 400 kutoka katika familia masikini waliokuwa wakipata chakula kutoka kwenye kituo maalum.
Kituo hicho kinalisha watoto wanaotoka katika familia zenye kipato kidogo ambacho kiko chini ya dola 250 kwa mwezi.
Hii inahusuisha watoto wote wa kike na kiume kutoka kwenye jamii hiyo ambayo ina tatizo la ukosefu wa ajira, umasikini na utapiamlo, wengine wana maambukizi ya UKIMWI.

"Matokeo yake yalikuwa dhahiri kwa muda mfupi sana, Afya za watoto ziliboreka kwa muda mfupi.
Anasema Elizabeth Serogole, meneja wa kituo hicho cha kulisha watoto ambaye anafanya kazi kwa kushirikiana na Mathabatha.
Anasema watoto wengi waliokuwa wakionesha kuwa na utapiamlo, kama vile vidonda kwenye ngozi walianza kupona mara baada ya kula mlo huo uliochanganywa na unga wa Mlonge.

Nyongeza hiyo ya Mlonge kwenye chakula chao iliwasaidia kupambana na magonjwa mengine yaliyojitokeza, pia iliwasaidia kuboresha uwezo wao wa kiakili," anasema Seregole.

"Wengi sasa wanaweza kusoma vizuri shuleni," anasema. Walichokuwa wanahitaji ni kjiko kimoja cha unga wa molonge katika chakula chao kwa siku. Dk.Samson Tesfay anayseoma Afrika Kusini kwenye chuo kikuu cha Zulu Natal idara inayohusika na masuala ya mbogamboga na matunda,alisema Mlonge ni mmea wenye kutenda maajabu kwenye lishe.

"Mlonge ni mmea wa kipekeeunaoweza kuutumia kwa faida nyingi, kama vile dawa, chakula, kuponyesha viungo mwilini na kusaidia kupambana na utapiamlo," anasema.

Source-Gazeti la Nipashe Ijumaa Februari 24, 2012

Binafsi nimeshasikia kuwa Mlonge unatibu magonjwa 300, bila ya kusahau kansa,maralia,vidonda vya tumbo,kuondoa sumu mwilini na hata kuongeza nguvu za kiume. Maderava wengi wa safari ndefu hutumia Mlonge kuondoa uchovu. Mlonge watu wa kule Tanga wanatumia kama mti wa kujengea fensi, Uzaramoni umepandwa karibu kabisa na vyoo vyao, Dodoma na Morogoro umejaaa tele. Dar mbegu zake zinauzwa kwa Shilingi 1000 kwa pakti.

Mbegu hizo zina dozi ya 3x3x3 na ukizila kwa wingi huweza kukufanya kuhalisha na kutoa uchafu mwilini. Tafakari ndugu yangu dawa tunazo tunatimia madawa yenye sumu yaliyotayalishwa na wazungu.... Tafakari.
 
Hii ni thread educative, hongera sana.These are the kind of threads one would like to read,sio thread za kijinga jinga tu.Okay,ninayo Milongelonge shambani kwangu.

Lakini taste ya mbegu zake au unga wake mm, inahitaji moyo.Sijawahi kula majani yake kama mboga,lakini nasikia nayo ni extremely nutritious.Kwa wale wanaoweza kula unga wake while mixed with warm water,nasikia ni dawa nzuri ya kisukari pia.
 
Huwa natumia moringa powder kwa kutibu malaria, inakinga malaria pia kama ukijizoesha kunywa kama chai, jaribu na hakika malaria utaisikia redioni..,.

Inatibu na sukari, iwe ya kupanda au kushuka..

pia ikichanganywa na asali ya nyuki wadogo ni dawa nzuri sana kwa kifua/kikohozi na mafua!
 
Mkuu , mlonge nimeupanda hapa home yaani ndani ya miezi nane limekuwa ni bonge la mti inabidi kukata matawi. Yaani kila kitu kuanzia majani, maua, mbegu n.k kina virubisho vingi. Mimi huwa nayatafuna majani kama mbuzi. Bado najiuliza kwanini huu mmea hautangazwi sana hapa tanzania.
 

ila asali za town hapo mmm unawza kukupa molasense!
 
Duh! Yaani pamoja na sifa zote hizo lakini bado wala sifahamu huo mti unafananaje!! Kwa wakazi wa dar, je kuna mtu anaweza kunijuza unapatikana sehemu zipi ili angalau nikauone ulivyo?!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…