Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,329
- 33,138
Chukua Majani, au maua au mizizi kiasi cha nusu kilo (Ni vizuri kama utachanganya vyote) Pondaponda na uloweke kwenye maji safi kiasi cha lita mbili (2) kwa muda wa masaa ishirini na nne au siku moja.
Chuja na uweke dawa hii mbali na jua/joto ni vizuri kama utaweka kwenye friji, kunywa kikombe kimoja Mara tatu kwa siku tatu.
TIBA
Dawa hii inaweza kutibu magonjwa yafuatayo:
1.Husaidia kuponesha vidonda.
2.Husaidia kurekebisha mzunguko wa hedhi kwa wanawake.
3.Husaidia kupunguza uvimbe.
4.Husaidia kushusha homa.
5.Huponyesha kifua na kukohoa.
6.Husafisha kibofu/njia ya mkojo.
7.Huongeza kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali