MREKEBISHARIKA
Member
- Dec 4, 2006
- 18
- 33
Leo majira ya mchana ndani ya maeneo ya Musoma mjini mkoa wa Mara tulipata ugeni.Na mgeni huyu sio mwengine ni Edward Ngoyai Lowassa.ilikuwa ni ugeni wa ghafla na kwa kweli kwa ughafla wake tumejionea mengi.Kuanzia afya yake aliposaidia kushushwa na kupandishwa kwenye ndege na pili jinsi hela zilizochangwa juzi viwanja vya Hekima,Mikocheno Dar es salaam zilivyoanza kutumiwa.Mie ninawaletea safari nzima.
Baada ya kutua uwanja wa ndege majira hayo, Ndg.Lowasa alipokelewa na Ndg.Veda Mathayo ambaye alimchukua hadi kwenye shamba lake huko Bunda ambapo alifanya naye mazungumzo alimkabidhi taarifa ya hali ya kisiasa ilivyo na ilivyobadilika ikiwemo kuwa Mwenyekiti na Mjumbe wa Nec toka Bunda amekimbia Kambi na sasa anamuunga mkono Mh.Wassira pamoja na wao ni Mnec na Mwenyekiti wa Butiama pia.
Lowasa ambaye alionekana kuchoka sana kiafya na nguvu za kutembea aliamua kuwatafuta wajumbe hawa.Akiwa njiani alisimama Bunda na kuongea na viongozi hao wa Bunda.Baada ya kumaliza Viongozi hao wawili waliongozana na Mh. Lowasa kuelekea Musoma mjini. Msafara huo ulisimama tena Butiama na kufanya hivyo wakaenda na viongozi hao wote hadi mjini.
Walipofika mjini walijumuishwa na viongozi wa mjini akiwemo Mwenyekiti wa wilaya ya Mjini na mwengine aliyetambulishwa kama ndg. Mathayo ambaye ni kiongozi wa Ccm mkoa wa Mara.
Kikao kilifanyika katika hotel ya Matvilla ambayo inamilikiwa na Ndg.Mathayo (Mnec).katika kikao hicho wenyeviti wa wilaya kila mmoja alipewa maagizo ya kuonana na wajumbe wake na kuwapatia kiasi cha shilingi laki moja ikiwa ni sehemu ya kuwapa salamu za Ndg.Mgombea.Wao wenyewe wenyeviti na Wanec wakiondoka na shilingi Laki Tano kila mmoja.
Kikao hicho kilichochukua zaidi ya Lisaa kilijazwa na Jazba toka kwa Bwana Veda na Ndg.Mathayo wakiwalaumu wenyeviti na Wanec wao kulwa kuwa Vigeugeu kwa kubadilikabadilika jambo ambalo walipotoka walikuwa wanasema vipembeni kuwa ..huyu bwana hata Afya hana tutamsaidiaje."
Mimi nipo safarini naye.Ninaendelea wajuza kinachoendelea.Nifuate......
Baada ya kutua uwanja wa ndege majira hayo, Ndg.Lowasa alipokelewa na Ndg.Veda Mathayo ambaye alimchukua hadi kwenye shamba lake huko Bunda ambapo alifanya naye mazungumzo alimkabidhi taarifa ya hali ya kisiasa ilivyo na ilivyobadilika ikiwemo kuwa Mwenyekiti na Mjumbe wa Nec toka Bunda amekimbia Kambi na sasa anamuunga mkono Mh.Wassira pamoja na wao ni Mnec na Mwenyekiti wa Butiama pia.
Lowasa ambaye alionekana kuchoka sana kiafya na nguvu za kutembea aliamua kuwatafuta wajumbe hawa.Akiwa njiani alisimama Bunda na kuongea na viongozi hao wa Bunda.Baada ya kumaliza Viongozi hao wawili waliongozana na Mh. Lowasa kuelekea Musoma mjini. Msafara huo ulisimama tena Butiama na kufanya hivyo wakaenda na viongozi hao wote hadi mjini.
Walipofika mjini walijumuishwa na viongozi wa mjini akiwemo Mwenyekiti wa wilaya ya Mjini na mwengine aliyetambulishwa kama ndg. Mathayo ambaye ni kiongozi wa Ccm mkoa wa Mara.
Kikao kilifanyika katika hotel ya Matvilla ambayo inamilikiwa na Ndg.Mathayo (Mnec).katika kikao hicho wenyeviti wa wilaya kila mmoja alipewa maagizo ya kuonana na wajumbe wake na kuwapatia kiasi cha shilingi laki moja ikiwa ni sehemu ya kuwapa salamu za Ndg.Mgombea.Wao wenyewe wenyeviti na Wanec wakiondoka na shilingi Laki Tano kila mmoja.
Kikao hicho kilichochukua zaidi ya Lisaa kilijazwa na Jazba toka kwa Bwana Veda na Ndg.Mathayo wakiwalaumu wenyeviti na Wanec wao kulwa kuwa Vigeugeu kwa kubadilikabadilika jambo ambalo walipotoka walikuwa wanasema vipembeni kuwa ..huyu bwana hata Afya hana tutamsaidiaje."
Mimi nipo safarini naye.Ninaendelea wajuza kinachoendelea.Nifuate......