Ze komedi...

-Vijana wabunifu sana, wasanii wa kweli! Walianzia EATV-walifanya vizuri, wakawa maarufu wakaitwa Bungeni mpaka Ikulu wakajisahau wakadhani ni maarufu kuliko EATV yenyewe, wakatemwa!
-Wakaja TBC wakaanza vizuri, wakapata tenda nono, wakajiona wako juu ya DUNIA, matanuzi kwa sana, wakaanza kutukana watu (kwamba wamefulia)!
-Sasa, hawana mvuto, hawaeleweki wanafanya nini, wanaburudisha au wanaganga njaa tu! mashabiki hakuna tena, Wapo TBC tu kwa sababu ya Contract ya Vodacom, Ikiisha-KAZI BASI! Warudi kijiweni...

Tuwaite nao wamefulia kama walivyowaita wenzao??
Message;
Ukiwa Juu usijishau na usione wengine ni wapumbavu badala yake ongeza juhudi zaidi na heshimu watu wote!

Mkuu inaonekana una bifu kubwa na hawa "The original Comedy" lazima kuna mahali mlikwaruzana tu pole sana. Ukweli ni kwamba hawa jamaa wamefulia na wamebakia kunywa bia mpaka wanashindwa kuwa wabunifu. Kwa sasa tunaopenda kucheka tumeamia EATV kwa akina Bambo, Kiwewe na Wenzake wale wako vizuri na ni wabunifu.
Kwa sasa hivi husikii mtu anakimbia home kuwahi the comedy kwani wanachofanya ni pumba tupu. Mfano jana alhamis hakuna walichofanya cha kuchekesha bali wameshindwa kutofautisha maigizo na vichekesho. wanatakiwa waende Kenya wakajifunze kwa kipindi cha "PASUA SHOW" kinachorushwa na KBC1 siku za Jumamosi kuanzia saa 2:30 usiku. wale vijana ni wabunifu ile mbaya hawaongei lakini wanachekesha sana.

Pia wakajifunze kwa akina Bambo kwani hata FUTUI siku hizi wamefulia baada ya Mkombe kuondoka.

Matangazaji wa the original Comedy' Masanja jana aliniboa sana kwani amepoteza mwelekeo kabisa anafanya mambo ya kitaahira badala ya kuchekesha.
 
-Vijana wabunifu sana, wasanii wa kweli! Walianzia EATV-walifanya vizuri, wakawa maarufu wakaitwa Bungeni mpaka Ikulu wakajisahau wakadhani ni maarufu kuliko EATV yenyewe, wakatemwa!-Wakaja TBC wakaanza vizuri, wakapata tenda nono, wakajiona wako juu ya DUNIA, matanuzi kwa sana, wakaanza kutukana watu (kwamba wamefulia)! -Sasa, hawana mvuto, hawaeleweki wanafanya nini, wanaburudisha au wanaganga njaa tu! mashabiki hakuna tena, Wapo TBC tu kwa sababu ya Contract ya Vodacom, Ikiisha-KAZI BASI! Warudi kijiweni... Tuwaite nao wamefulia kama walivyowaita wenzao??Message;Ukiwa Juu usijishau na usione wengine ni wapumbavu badala yake ongeza juhudi zaidi na heshimu watu wote!
hapo kwenye nyekundu na wewe walikutoa nini?
 
usipate shida mkuu katazame MIZENGWE pale ITV utafurahi na nafsi yako.
Laaa..hh i never miss mizengwe esp when am at home during sundays,lkn i hate style ya hao akija joti...honestly jamaa wako creative ila wana lugha ya mtaro wa kutiririsha kinyesi.
 
du jamaaa wamelewa umaalufu watu wengi tuliacha kuwatazama.
wamejaa majigambo aswa aswa huyo masanja ndo anaboha kujifanya anaujua mji wakati alikuwa fuka tu.
 
Haters mna chuki binafsi mbona vijana wanafanya vizuri tu, nia ya kuchekesha kwao ni kuingiza kipato na ni sehemu ya ajira kwa vijana ambao kama wasingepata kazi hiyo wangekuwa sehemu mbaya ila kwa sasa wanaongeza kipato chao na pato la taifa kwa kulipa kodi na kutoa ajira kwa watanzania wengine<br><br>Halafu ucheshi unamsahidia mwanadamu kuongeza siku za kuishi na kumpunguzia stress mbalimbali za maisha. Sasa nyinyi badala ya kufurahi kwa maendeleo ya watanzania wenzetu mnaanza kuwaponda. Ule ni ucheshi tu na nia ni kutufuraisha baada ya shughuli za kujenga uchumi<br><br>Wa tz tuache chuki binafsi tumekuwa sijui jamii ya aina gani kila kitu kinachofanywa na watz wenzetu tunaponda, mtu ukivaa vizuri unapondwa acheni hizo na sitaki majibu ila habari ndio hiyo<br><br>Kwa maendeleo ya Origino komedi fuata link hii &nbsp; http://www.mkandamizaji.blogspot.com/<br>

Watu wanacholalamika ni kwamba siku hizi hawatuchekeshi kama tulivyowazoea,
Nakumbuka enzi zile za EATV watu wengi tulikuwa tunatoka ofisini mapema siku ya Alhamis kuwahi Ze Comed, vyuoni watu lecture za mida ile watu wanakacha kwenda kuisikiliza Ze Comed.

Kama uliiona Ze Comed ya siku zile hakika ungesema ilikuwa zaidi ya kuchekesha hasa pale walipokuwa wanatupa taarifa za Rais (au waziri f'lani) kwenda safari nyingi za nje ikiwemo na za kutazama kilimo cha mboga mboga.

Nakumbuka ni kupitia Ze Comed waliwahi kuainisha hasara serikali ilipata kwa issue ya Epa (wakawa wanasema ile fedha ukiitandandaza chini itafika mpaka Lujewa na mifano mingine mingi ya ingejenga shule ngapi, ingelipa mishahara kwa walimu wangapi), na hii waliipresent kikomedi komedi.

Leo hii wamebaki kutulazimisha kucheka, na kubaki tunawaona laini tu, hawatupi taarifa za ukweli juu ya serikali yetu kama walivyozoea kutupa taarifa huku wakituchekesha.
 
Shule nayo inasaidia,kujipanga na kependa kujifunza kutoka kwa watu,mimi naona wanathink inside the box,Wamwangalie mwenzao churchill wa Kenya anafanya nini,comedy anaalika hadi makamu wa rais(odinga)Martha Karua ETC,Comedy wanaalikwa bussiness people na kutoa advice kwa vijana jinsi ya kujiendeleza!Kwa kweli they need to learn from others and be creative!
 
Watu wanacholalamika ni kwamba siku hizi hawatuchekeshi kama tulivyowazoea,
Nakumbuka enzi zile za EATV watu wengi tulikuwa tunatoka ofisini mapema siku ya Alhamis kuwahi Ze Comed, vyuoni watu lecture za mida ile watu wanakacha kwenda kuisikiliza Ze Comed.

Kama uliiona Ze Comed ya siku zile hakika ungesema ilikuwa zaidi ya kuchekesha hasa pale walipokuwa wanatupa taarifa za Rais (au waziri f'lani) kwenda safari nyingi za nje ikiwemo na za kutazama kilimo cha mboga mboga.

Nakumbuka ni kupitia Ze Comed waliwahi kuainisha hasara serikali ilipata kwa issue ya Epa (wakawa wanasema ile fedha ukiitandandaza chini itafika mpaka Lujewa na mifano mingine mingi ya ingejenga shule ngapi, ingelipa mishahara kwa walimu wangapi), na hii waliipresent kikomedi komedi.

Leo hii wamebaki kutulazimisha kucheka, na kubaki tunawaona laini tu, hawatupi taarifa za ukweli juu ya serikali yetu kama walivyozoea kutupa taarifa huku wakituchekesha.

Wamemezwa na kundi la mafisadi, mwanzoni walikuwa wapambanaji ndio maana walikuwa huru hata kuwasema viongozi wa nchi ki comedy, sasa hivi hata Komba mwenyewe hawamwongelei na issue za wabunge au mawaziri ndo kabisa. Walitegwa kwenye chambo na wakanaswa.
 
wabongo bwana yahani wakisha kususa utatamani kujikojolea, nakumbuka walikuwa wanawatukana sana wasanii wengine kwamba wao wanafedha nyingi! waaaaapi bwana sikio halizidi kichwa bwana wako wengi wazuri kina mtanga, kingwendu bambo, mzee majuto, small nk wote wakongwe katika sanaa na wanafanya vizuri. sasa hivi wao so issue tena maana eatv, channel nk kuna makomedi ya kusisimua. ukivungua tbc1 utasikia unaambiawa toa weka eatv/channel ten hao hawana mpya hao tumeshawazoea.
 
Mie nishawasahau kwa kweli!sasa hivi comedy kali ni channel 10 Vituko show na ITV Mizengwe.Mie niliacha kuwaangalia walipo anza kumdhihaki mzee Mengi,ni utivu wa nidhamu wa hali ya juu sana na wala sinta shangaa wakiporomoka tu ziro. Shigongo aliisha wahi kutoa makala ya kuwataaharisha kuwa wasijione wamefika safari bado na akakumbushia walipoanza wanaenda pale Global wanachekesha chekesha wanapewa buku
 
Kitendo cha kuvaa kama mashoga sikipendi epuuuuuuuuuuuuuuuuuuu! Ile dharau kwa mzee mengi siipendi kabisa. kujiona wamefika sipendi, kuliko kuangalia ze komedy ya masanja ni afadhali kulalal fofofo.
 
Siku hizi sijui wamekuwaje hawa watu!! Sawa vipaji vya kuigiza wanavyo lakini hiyo sio komedy kabisa wapo kawaida sana wala hawachekeshi tofauti na zamani ilipokuwa comedy ya ukweli. Wajipange upya kwakweli wameluz control.
 
-Vijana wabunifu sana, wasanii wa kweli! Walianzia EATV-walifanya vizuri, wakawa maarufu wakaitwa Bungeni mpaka Ikulu wakajisahau wakadhani ni maarufu kuliko EATV yenyewe, wakatemwa!
-Wakaja TBC wakaanza vizuri, wakapata tenda nono, wakajiona wako juu ya DUNIA, matanuzi kwa sana, wakaanza kutukana watu (kwamba wamefulia)!
-Sasa, hawana mvuto, hawaeleweki wanafanya nini, wanaburudisha au wanaganga njaa tu! mashabiki hakuna tena, Wapo TBC tu kwa sababu ya Contract ya Vodacom, Ikiisha-KAZI BASI! Warudi kijiweni...

Tuwaite nao wamefulia kama walivyowaita wenzao??
Message;
Ukiwa Juu usijishau na usione wengine ni wapumbavu badala yake ongeza juhudi zaidi na heshimu watu wote!

ninachofaham ni kwamba kamwe hawawezi kufurahisha kila mtu-ndo maana kuna comedy kwenye channel nyingine-kama wanaboa-usiwaangalie-sisi na wengine tutaendela kuwaangalia
 
kuku hata hasipo oga anataga yai jeupe!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Hii nayo pia ni indicator ya kwamba "watanganyika si mabwege tena". The biggest problem ni kwamba walivyohamia huko TBC wakaanza kuplay against the people. Tunaowaita mafisadi wao wakawa wanawasifia, wakakejeli watu wanaoaminiwa na watanzania mfano Dr. Slaa, wakawa hawapo tena update with the issues. Hebu imagine the following opportunities kwa comedian:

1. JK alivyoanguka jukwaani



2. Kuvua magamba

3. Mafisadi kuendelea kupeta ilhali wabunge wa upinzani wakikamatwa kwa masuala ya kisiasa.

4. Kujiuzulu kwa Makamba

5. Nape etc.

Sasa wako upande ule hawawezi tena kuikejeli CCM wala serikali yake maana ndiyo upande wao. Hii inanikumbusha marehemu Kolimba, kwa wanaomfahamu the guy wa one of the samartest and a no non-sense person. Wakampa licheo CCM akaanza kutetea yale asiyoamini baadae akawa anaonekana kituko na asiye na mvuto.

Vipaji bado wanavyo, wakihama tu upande you will see!!!!! Umaarufu utarudi pale pale au hata zaidi.
 
Sijawaangalia muda mrefu sana. Sijui wamefikia wapi. Lakini tukumbuke hawa ni watoto wa Tanzania/Afrika. Na mtoto akinyea kiganja hukikati. Nadhani watu wawape ushauri na namna ya kufanya kazi yao iwe na maana ili kuwasaidia kuelewa hawako pale kwa ajili ya kundi fulani bali kwa maslahi ya Utaifa. Vinginevyo comment nyingi humu ni kama za watu wanaosubiri kuona watakavyoanguka na kufa kifo cha mende. Hili limenisikitisha, hatusaidiani never, bali kuombeana mabaya tu. Hebu jamani tuangalie namna gani ya kuwapatia mwongozo hao watoto wa Afrika na sio kusubiri kuwazika kwa nderemo. Yangu hayo tu! :A S 114:
 
Back
Top Bottom