Gaga
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 4,558
- 1,968
Habari za ijumaa wakuu, najua leo kila mtu anafurahia kuanza week end kwa namna yake.....Mie napenda kuja na hii,...... Zawadi, mnajua kwamba zawadi ni kitu kidogo sana lakini impact yake huwa ni kubwa sana hasa kwenye swala zima kwa wapendanao, kuna wanaopenda kupokea zawadi toka kwa wapenzi wao, lakini wao hata siku moja hawajigusi kuwapa wenzao zawadi ya aina yoyote ile, yaani unakuta mwenzake kila tukio au hata kusipokuwa na tukio lolote lile anachukuwa muda wake anamtafutia zawadi nzuri, embu jiulize kwa nini huwa humpi na yeye zawadi?
Nimeleta hili kwenu leo baada ya jana kukuta home nimeletewa sasa kama mnavyojua tena sie wadada huwa hatukawii kusumulia mashost ofisini na kama vile, mmoja wa marafiki zangu akawa analalamika kwamba kila mara huwa anampelekea zawadi mpenzi wake, iwe perfumes , shati, hata chocolate na cake za birthdays ila huyo wake hata siku moja hajawahi mpa zawadi hata ya pipi na sasa wana miaka mitano ya uhusiano.
Mwisho kabisa namalizia kwa kusema, zawadi sio kipimo cha mapenzi, ila ina maana sana kwa mpenzi wako, anaona kuwa unamjali na kumthamini sana, Pia umeacha shughuli zako ukakumbuka kuna mtu wako wa muhimu ukamnunulia zawadi, na zawadi inaweza kuwa yeyote kulingana na uwezo wa mtu, na nawakumbusha wadada kuwa wasijibweteke kwa kuona wao ndio wana haki ya kupewa zawadi na waume na wapenzi wao hata sie pia tuwe tunajitoa na kufanya hilo.. sasa nakuuliza wewe lini umemnunulia mpezi/mke/mume wako zawadi? embu jaribu leo hata pipi tu uone atakavyofurahi
Nawakilisha, ahsanteni wakuu.
Nimeleta hili kwenu leo baada ya jana kukuta home nimeletewa sasa kama mnavyojua tena sie wadada huwa hatukawii kusumulia mashost ofisini na kama vile, mmoja wa marafiki zangu akawa analalamika kwamba kila mara huwa anampelekea zawadi mpenzi wake, iwe perfumes , shati, hata chocolate na cake za birthdays ila huyo wake hata siku moja hajawahi mpa zawadi hata ya pipi na sasa wana miaka mitano ya uhusiano.
Mwisho kabisa namalizia kwa kusema, zawadi sio kipimo cha mapenzi, ila ina maana sana kwa mpenzi wako, anaona kuwa unamjali na kumthamini sana, Pia umeacha shughuli zako ukakumbuka kuna mtu wako wa muhimu ukamnunulia zawadi, na zawadi inaweza kuwa yeyote kulingana na uwezo wa mtu, na nawakumbusha wadada kuwa wasijibweteke kwa kuona wao ndio wana haki ya kupewa zawadi na waume na wapenzi wao hata sie pia tuwe tunajitoa na kufanya hilo.. sasa nakuuliza wewe lini umemnunulia mpezi/mke/mume wako zawadi? embu jaribu leo hata pipi tu uone atakavyofurahi
Nawakilisha, ahsanteni wakuu.