Zanzibar: ZEC Yaamuru Maalim Seif akamatwe

Zanzibar: ZEC Yaamuru Maalim Seif akamatwe

Delegate

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2012
Posts
331
Reaction score
203
Wakati Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) ikisubiriwa kutangaza matokeo ya urais mapema asubuhi hii, sintofahamu imewagubika wananchi visiwani humo hasa baada ya mgombea urais kupitia CUF, Maalim Seif Sharif kujitangazia ushindi.

Kuchelewa kutolewa kwa matokeo hayo kumezua hali ya wasiwasi visiwani humo iliyopelekea kuimarishwa kwa ulinzi mkali kupitia jeshi la wananchi.

Wakati Maalim Seif akijihakikishia ushindi na kumtaka mshindani wake Dkt. Ali Shein kukubali matokeo, ZEC kutangaza matokeo mapema pamoja na Rais Jakaya Kikwete kusaidia katika hatua za kukabidhiana madaraka, imeripotiwa kuwa ZEC imelitaka jeshi la polisi kumkamata mgombea huyo kwa kile kilichodaiwa kuwa amekiuka sheria ya uchaguzi kwa kujitangaza mshindi.

Sheria ya Uchaguzi inaipa Tume ya Uchaguzi pekee mamlaka ya kumtangaza mshindi wa nafasi ya urais na mtu anayekiuka sheria hiyo anatenda kosa la jinai.

Chanzo: DAR24
ZEC: MAALIM SEIF ANAPASWA KUCHULIWA HATUA ZA KISHERIA KWA KUTANGAZA MATOKEO

Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imesema imesikitishwa na kitendo cha mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Wananchi (CUF) kujitangazia ushindi katika uchaguzi mkuu uliofanyika Jumapili tarehe 25 Oktoba, 2015 na imevitaka vyombo vinavyosimamia utii wa sheria kumchukulia hatua kiongozi huyo wa CUF.

"kitendo cha Maalim Seif kujitangaza mshindi amevunja kifungu cha 42 (5) cha sheria ya mwaka 1984 ambacho kinaipa mamlaka Tume ya Uchaguzi kuwa chombo pekee chenye mamlaka hayo" Mwenyekiti huyo alifafanua.

Akijibu maswali ya waandishi wa habari leo, Mweyekiti wa ZEC Jecha Salum Jecha alisema kuwa Maalim Seif ametenda kosa la jinai hivyo mamlaka zinazohusika zinapaswa kumchukulia hatua.

Kwa mujibu wa kifungu hicho, mtu akithibitika ametenda kosa hilo atahukumiwa kulipa faini ya Tzs laki tano au kwenda jela miaka mitano au adhabu zote.

"Tume haina mamlaka ya kumkamata wala kumhoji Maalim lakini viko vyombo vyenye mamlaka hayo hivyo itakuwa ni vyema vikatimiza wajibu wao kwa kumkamata na kumhoji mhusika hasa ukizingatiwa kuwa hii ni mara ya pili kwa Maalim Seif kutenda kosa kama hilo" Mwenyekiti wa Tume alieleza.

Alibainisha kuwa Tume yake imekijadili kitendo hicho kwa makini na uzito unaostahiki na kubainisha kuwa tangazo hilo linaweza kusababisha uvunjifu wa amani na utulivu uliopo nchini.

Bwana Jecha alibainisha kuwa Maalim Seif, kama walivyo wagombea wengine 13 wa nafasi ya urais wa Zanzibar wanaelewa fika sheria hiyo hivyo alitoa wito kwa wagombea wengine kuwa watulivu kama walivyo wananchi.

Kuhusu kasi ndogo ya Tumeyake kutangaza matokeo, Mwenyekiti huyo alisema hivi sasa kazi kubwa wanayoifanya ni kuhakiki kura kujua kama hakuna tofauti ya kura baina ya zile zilizoandikwa na hali halisi.

"Wanaoandika na kuhesabu kura wote ni binadamu hivyo wanaweza kuchanganya mahesabu na ndio maana kazi yetu hivi sasa ni kulinganisha kura"alisisitiza Mwenyekiti wa Tume.

Kuhusu kukamatwa kwa karatasi za kupigia kura huko katika jimbo la uchaguzi la Chonga, Wilaya ya Chake Chake, mkoa wa Kusini Pemba, Bwana Jecha alikiri kutokea kwa hilo na kwamba suala hilo sasa liko chini ya mikono ya Jeshi la Polisi.

Alitahadharisha juu vitendo vya baadhi ya wagombea kuchukua vyeti bandia vinavyoonesha kuwa tayari wao wameshinda nafasi za ubunge au ujumbe wa Baraza la Wawakilishi.

Bwana Jecha alitoa wito kwa wananchi kufanya subira wakati huu Tume yake ikifanya kazi ya kukusanya na kuhakiki kura na baadae kuwatangaza washindi.

 
alichofanya seif ni sawa na alichofanya makamba
 
maskini maalim seif wanaweza kumkamata kweli hawa jamaa:spy:
 
Wanajidanganya mbona Makamba hawajamkamata au kwa vile yeye hakuita waandishi wa habari
 
akamatwe tu, vipi ajitangaze mshindi wakati kura hazijahesabiwa zote? Huyu mzee bora akaozee jela tu. Na huku kwetu marienge na yeye yuko njiani.
 
Sasa vyama vingi vya nini??? CCM WATAWALE NCHI HII PEKE YAO....KAMA CHINA Chama kimoja tu...Wametupotezea muda wetu bure....!!!!
 
Makamu wa Rais anawezaje kukamatwa na Polisi kwani analindwa na Polisi au watu gani !! Hicho kitendo kinaweza kusababisha machafuko ya hali ya juu.
 
akamatwe tu, vipi ajitangaze mshindi wakati kura hazijahesabiwa zote? Huyu mzee bora akaozee jela tu. Na huku kwetu marienge na yeye yuko njiani.

Funga bakuli lako we mtu usiye na haya haya.wa.ni mkubwa. Nzanzibar siku ile ile ya uchaguzi matokeo yote yalikuwa tayari
 
alichofanya seif ni sawa na alichofanya makamba

Alichofanya Seif na alichofanya Makamba ni vitu viwili tofauti kabisa....! Utofauti huo upo katika maeneo yafuatayo;
  1. Seif alizungumzia matokeo ya urais, wakati Makamba alizungumzia ushindi wa majimbo....!
  2. Kumbuka Seif alienda mbali na kuiamuru Tume itangaze kama anavyotaka yeye, wakati Makamba hakufanya hivyo...!
Pengine mi nashauri kuwa ni vema ikaangaliwa kuwa Katiba ya Zanzibar, na Sheria ya uchaguzi inasemaje katika hali kama hii...! Halafu hatua ichukuliwe ipasavyo...!
 
Zanzibar itawaka moto...!! I see it coming...!!!
 
Kwanza Maalim hakujitangaza mshindi yeye katangaza kura zake na za mwenzake kama zilivyobandikwa vituoni Public. Kwani ni kosa kujumlisha matokeo yaliyo bandikwa kituo A + B+ C?
Mwaka huu Zanzibar kitanuka kweli, mlizoea kumpoza huyo mzee na kumwomba awatulize wafuasi wake kisha mambo yakipoa mnamtukana na kumkashifu sana. Kachoka kufanya hivyo na kajitambua kuwa alichokuwa anafanya sii kuwatendea haki wapiga kura wake.
 
Akikamatwa kutachafuka sana Zanzibar. Wamwache tu
 
Ukiona nchi inanunua silaha against its own poor people ujue hapo viongozi wake wanatumia yule mgombea aliyeshindwa ubunge pale karibu na kituo kikuu kwa kufikiri. Pole km hukunielewa lkn hbr ndio hiyo. Ni aibu akina mama wajawazito wanalala mzungu wa4 hosp hakuna dawa maji hskuna elimu ndio kabisaaaa uozo. Wao wako busy kumkamua mchovu huyu ili wanunue midege ya vita. Vifaru. Magati ya washa2. Akili matope?
 
Back
Top Bottom