Jicho la Tai
JF-Expert Member
- Oct 10, 2012
- 1,449
- 574
WANANCHI mkoani Unguja Kaskazini wametofautiana juu ya suala la elimu katika Muungano kutokana na baadhi kutaka ushirikiano uanzie shule za awali hadi vyuo vikuu, huku wengine wakitaka liondolewe hata kwenye elimu ya juu. Aidha hatua ya wanafunzi wa Zanzibar kufutiwa matokeo na Baraza la Taifa la Mitihani (Necta) imekuwa hoja kuu kwenye mikutano ya kuchangia maoni ya Katiba baada ya asilimia kubwa ya wachangiaji, kutaka mitihani ya kidato cha nne itungwe na kusahihishwa visiwani hapa.
Katika mikutano ya kukusanya maoni ya katiba inayoendelea katika shehia mbalimbali mkoani Unguja Kaskazini, wapo baadhi ya wachangiaji hususan wanafunzi na walimu waliotaka Zanzibar ijiondoe katika ushirikiano kwenye mitihani ya kidato cha nne na elimu ya juu. Mbele ya wajumbe wa tume, walitaka Katiba mpya itamke kwamba Zanzibar iwe na Baraza lake la mitihani na Necta ibaki kuwa ya bara, wakisema imekuwa ikiwahujumu wanafunzi wa visiwani hapa kwa kusahihisha vibaya mitihani yao na kuwafutia matokeo.
Tofauti na msimamo wa kutaka kila upande ujitegemee kielimu, mkazi wa Shehia ya Gamba, Rahma Abdalla Maisara alitaka Katiba itamke pande mbili za Muungano zishirikiane kuanzia elimu ya awali hadi chuo kikuu. Hata hivyo, Maisara ambaye ni Mtumishi wa Idara ya Afya Zanzibar, aliungana na wanaotaka utungaji na usahihishaji wa mitihani ushirikishe pande zote za muungano, akisema hatua hiyo itaondoa utata uliopo.
Akikosoa wanaotaka elimu ya juu iondolewe kwenye ushirikiano, mkazi wa Shehia ya Moga, Tano Hamisi Issa alisema ni vyema Zanzibar ikabaki kwenye muungano utakaowawezesha kupata elimu yenye viwango. Elimu ibaki kwenye Muungano. Tunapiga kelele angalia mwalimu ana digrii lakini anachozungumza hakieleweki, alisema Issa ambaye alikuwa akirejea kwenye kauli ya mchangiaji katika moja ya mikutano ambaye licha ya kujitambulisha kuwa ni mwalimu wa sekondari, hakumudu kutoa ufafanuzi wa hoja zake
Katika mikutano ya kukusanya maoni ya katiba inayoendelea katika shehia mbalimbali mkoani Unguja Kaskazini, wapo baadhi ya wachangiaji hususan wanafunzi na walimu waliotaka Zanzibar ijiondoe katika ushirikiano kwenye mitihani ya kidato cha nne na elimu ya juu. Mbele ya wajumbe wa tume, walitaka Katiba mpya itamke kwamba Zanzibar iwe na Baraza lake la mitihani na Necta ibaki kuwa ya bara, wakisema imekuwa ikiwahujumu wanafunzi wa visiwani hapa kwa kusahihisha vibaya mitihani yao na kuwafutia matokeo.
Tofauti na msimamo wa kutaka kila upande ujitegemee kielimu, mkazi wa Shehia ya Gamba, Rahma Abdalla Maisara alitaka Katiba itamke pande mbili za Muungano zishirikiane kuanzia elimu ya awali hadi chuo kikuu. Hata hivyo, Maisara ambaye ni Mtumishi wa Idara ya Afya Zanzibar, aliungana na wanaotaka utungaji na usahihishaji wa mitihani ushirikishe pande zote za muungano, akisema hatua hiyo itaondoa utata uliopo.
Akikosoa wanaotaka elimu ya juu iondolewe kwenye ushirikiano, mkazi wa Shehia ya Moga, Tano Hamisi Issa alisema ni vyema Zanzibar ikabaki kwenye muungano utakaowawezesha kupata elimu yenye viwango. Elimu ibaki kwenye Muungano. Tunapiga kelele angalia mwalimu ana digrii lakini anachozungumza hakieleweki, alisema Issa ambaye alikuwa akirejea kwenye kauli ya mchangiaji katika moja ya mikutano ambaye licha ya kujitambulisha kuwa ni mwalimu wa sekondari, hakumudu kutoa ufafanuzi wa hoja zake