J.K.Rayhope
JF-Expert Member
- Oct 26, 2011
- 316
- 31
Wakuu wa jamvi,habari!Natumai wote hamjambo.Nimekuwa na maswali mengi kichwani kuhusu Zanzibar na muungano kwa ujumla.Kwa wale wenye kumbukumbu chokochoko za muungano zinazidi kuongezeka kila mwaka na kila awamu ya urais inapoingia,ni wazi kwamba yapo mambo ya msingi ambayo Wazanzibari wanahitaji.Inawezekana serikali zote 2 zinayapuuza na kuyaona ni ya "kitoto" lakini kwa ulimwengu tulionao kiongozi hapaswi kuziba masikio.Kwa maoni yangu,siyo kuanza kuuunda tume za kiintelijensia,kiongozi mwenyewe,toka ofisini,kaulize kunani huko.Chonde MwanaJF kama unafahamu hata kiduchu kwamba wazanzibar wanataka nini hasa,tujuze tupate kujua.Mungu tusamehe Tanzania,tumeanza kuchoma hata madhabahu yako.Tusamehe na utupe roho wa kutuongoza tuishi kwa amani.Aaamen.