Zanzibar ni Non secular state?

Ila hujajibu nilichokuuliza,hoja si muda wala baadhi ya nchi zinafanyaje bali nimetaka kujua kwa nchi ambayo haina mapumbuziko kwa sikukuu ya eid kwamba hiyo nchi ina uhuru au haina uhuru wa dini?
Uhuru wa Dini inayo, sababu watu wa imani husika wanapewa mapumziko
 
Ilibidi vitu vyote. Sheria ,katiba n.k za tanganyika zitumike hadi zanzibar.mtu ukitoka bara kwenda znz unaishi kwa shida utafikiri znz sio tanzania,au vinginevyo watuambie znz ni nchi kamili haipo tanzania.
Mkuu zanzibar ni nji kivulitu ili tuwatawale wale wehu tukiwaruhisu wajitawale hawa kawii kutulipuwa hawa, naapa kwajina la aliejuu wakiruhusiwa hawa tanzania bara tutakimbiana, MUNGANO UDUMU
 

Sasa mkuu tayari umeshasema nchi za kiislamu, nakama wewe si muislamu nini kinakuuma? si waachie wenyewe na taratibu zao? mbona mnakua mnacomplicate mambo sana lakini?
 
Kwaujinga huu zazbar itakuwa koloni la tanzania bara mpka mwisho wa dunia
 
Nitajie nji mbili zenyehayo mambo
 
Sasa mkuu tayari umeshasema nchi za kiislamu, nakama wewe si muislamu nini kinakuuma? si waachie wenyewe na taratibu zao? mbona mnakua mnacomplicate mambo sana lakini?
Ujue Dunia nzima ikiamua tufanye hivyo Waislam ndio biggest losers,

Waislam ndio wanaoongoza kukimbilia nchi za wengine huku wakitaka kuwekewa mazingira yanayoendana na tamaduni zao, na hawaishii hapo tu, wanajengewa misikiti, wanaruhusiwa kuvaa hijab sehemu ambazo hazikutakiwa

Juzi Udom walikuwa wakidai wajengewe msikiti chuoni wakati hakuna hata kanisa, japo Wakristo ndio wengi

Sasa Dunia nzima ikiamua kusema kama hutaki kufuata tamaduni za hapa muondoke itakua tabu sana kwenu
 
Maradhi huisha lakini ujinga hudumu
 
Mimi nafikiri kutojuwa historia,zanzibari kabla ya kutekewa na Tanganyika hayo ndio yalikuwa maisha yao, hata wazungu walishikishwa adabu walipo taka kuingia zanzibary kimatembezi. baada ya kutekwa na Nyerere kwa kivuli cha muungano ikawathiri.
Ustaarabu wao taratibu ukachanganyika na mila za Kipagani, ndio sabau unapofika muda wa kudhihirsha na kusheherekea mila na ustaarabu wao upagani nao unapiga kelele kwa kuwa na wenyewe ulichanganywa kule. Wakati wa miaka ya 60 mzanzibari akiokota hela barabarani huipeleka kituo cha polisi na kutangazwa ktk vyombo vya habari aliepoteza hela yake imeokotwa, wafanya biashara walikuwa wakiacha biashara zao wazi na kwenda kuabudu au kufanya shughuli nyingine na kuzikuta biashara zao salama, walipochanganya na mila za kipagani tu yote hayo yalitoweka, sasa kwa kipindi hichi waachieni washeherekee mila yao mwezi ukiisha watarudi kuchanganya na kipagani maisha yatasonga tena,
 

Si waislamu tu hata watu wadini yoyote watapendelea waeke mazingira ya utamaduni wao popote walipo, Ila kinachokosekana ni mamlaka yakufanya hivyo kwa vile ni ugenini, Kwahiyo wenye maamuzi wa kukuruhusuni ni wenyeji. Je umewahi ona hilo vuguvugu Uchina? au Russia? mana ni wazi wao hawataki mtu aende halafu ajifanyie mambo yake. Lakini nchi za magharibi wao wenyewe ndio walioeka taratibu za human Right na uhuru wa kuabaudu sasa watu wakiomba hakizao hapo pana kosa?

Ni vizuri uheshimu taratibu za ugenini ulipo ili uweze kuishi vizuri. ukihisi pana tatizo kwako basi ondoka.
 
Wanachofanya China au Russia sio sawa, ndio maana wanakosolewa, hata Waislam wamekuwa wakilalamikia sana wanachofanyiwa wenzao huko China na Russia, hiyo sio mifano ya kufuata

Nakubali kila nchi ina utamaduni wake ambao inataka usivurugwe lakini lazima kuwepo na kiwango cha uvumilivu, bila kuvumiliana basi hii Dunia ingekuwa imejaa chuki sana

Inavyoonyesha Zanzibar mkiachwa peke yenu basi mngechinja na kuchoma Wakristo na makanisa yote ili kulinda utamaduni wenu,
 
Uhuru wa Dini inayo, sababu watu wa imani husika wanapewa mapumziko
Mbona unajibu tofauti na navyouliza? au basi tuchukue jibu lako kwamba nchi zote(ukiondoa zenye wenye waislamu wengi) huwa zinatoa nafasi ya mapumziko kwa sikukuu
za kidini zote? hili ndio jibu lako,si ndivyo?
 

Mkuu hio sio sawa, nifikira zako tu ambazo zinatokana kuaminishwa hivyo. Hivi kwani Zanzibar hata kabla ya muungano hakukuwa na wakristo na wahindu? mbona walikua wanaishi vizuri tu. Hata hivi leo ukienda zanzibar wale wakristo waasili (namaanisha wazanzibar wakristo waliopo Zanzibar kwa miaka mingi) mbona wanaishi kwa amani tu? Hilo suala la makanisa ni propaganda ya CCM tu katika uendelezo wakutaka kutawala watu. Kama kweli Zanzibar waislamu walichoma makanisa mbona hakuna watu waliohukumiwa ? Hivi ni kweli Jeshi la polisi limeshindwa kuwakamata hao waliofanya hayo matokio?

Nakuhusu hilo suala la China na Russia wanachowafanyia raia wao ni kweli sio haki kabisa, mana kama raia wenu hata akiwa dini yake lazima nayeye anahaki zake. Ila kwa suala la wageni mimi sina tatizo nao kabisa.
 
kwa hiyo kama unaunga mkono wageni kushambuliwa kwa kuwa wana imani tofauti ila unapinga wananchi ambao wana imani za kigeni kutokushambuliwa?

China inawasulubu hao Wachina Waislam kwa sababu imani yao ni ni tofauti na ya Wachina wengi, na kama ni tofauti na wengi ina maana ililetwa, wanachofanya China sio tofauti na inachofanya Zanzibar

imani zetu karibia zote zimeletwa na wageni, kama ni kulinda utamaduni wetu mbona tuliacha huo utamaduni wetu original tukachukua huo wa Waarabu?
 

Mkuu hivo ni vitu viwili tafauti. Kumpa uhuru mgeni nyumbani kwako na kumpa uhuru mwananchi wako nchini kwake. hata akiwa na imani ya kigeni lakini anabaki kuwa mwananchi wako, na anahaki zake kama mwananchi. Mgeni sio lazima kukuwepo kwako. Nandio mana atatakiwa afate taratibu zako kama haziwezi anaweza ondoka tu.
 
ZANZIBAR NI NCHI KAMA NCHI NYINGINE NA INA MAMLAKA, KANUNI NA SHERIA ZAKE.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…