Zanzibar: Meli mpya yawasili!

Zanzibar: Meli mpya yawasili!

Heh, kumbe ilikuwa ferry? Hii ni hatari sana manake ferries are not meant to be used in deep and open sea navigation, si ni yale yale ya Skagit na Space Islander yatajirudia? Nchi hii makosa tunayoyafanya mara kwa mara hayatufundishi lolote kweli?

Ferry ni meli/ boat ya abiria...What matters is the built and capacity... Yes, not all ferries built for high seas but some are. Remember that ferry sailed from Greece to Zanzibar.
 
Wewe kweli kiboko... Sasa hizo ndege za Ulaya ,Asia na Marekani zinazokuja TZ kila siku zilihitaji Muungano na Tz kufanya safari zao? Kuna uhusiano gani baina ya Meli na Muungano ? Au ndio unataka kutengeneza uwongo, kwamba kabla ya Muungano kulikua hakuna safari za baharini baina ya Tanganyika na Zanzibar?


HIZO NDEGE za MATAIFA ya NJE ni VIGUMU kubeba MATAKATAKA toka Tanganyika kwenda Zanzibar

Sasa hizi MELI zinabeba hadi vitunguu, kandambili bure KWENDA ZANZIBAR... Sasa Umeona MELI TOKA MOMBASA

Kwenda ZANZIBAR inavyochunguzwa? na watu wanavyopakulikwa kama NONDO?

NO MORE FREELANCE free Movement of People and GOODS; So Damn Many RESTRICTIONS kama ni NCHI KWA NCHI

Tangu lini Unapata KUNGU toka MOMBASA ???
 
Narudia tena. Mtu akinunua gari jipya la kubebea mizigo na ku-convert kuwa basi la abiria ni sawa simply because gari lilikuwa jipya? Yaani ku-convert gari la mizigo kuwa basi la abiria ina uhusiano gani na mnunuzi kumcha Mungu? Kwa hiyo basi kama anamcha Mungu ruksa ku-convert ferry iliyokuwa inabeba abiria around 700 to zaidi ya 1,500?

Habari zinasema wazi kabisa kuwa the ferry was not
designed for East African lines which requires as much passengers space as the vessel can host. Walichofanya ili kupakia abiria 1,500 ambao ni zaidi ya abiria wanaokubaliwa kwenye hiyo ferry, ni ku-convert hiyo ferry from ferry shipping into cruise world. Hii itawezesha Azam kupakia abiria wengi on the same deck as cars. Kwa nini abiria wapakishwe kwenye deck iliyukuwa imetengezwa kwa ajili ya magari tuu? Kama huu si utapeli ni nini?

Tunafuata rules na sio nani anamcha au asiyemcha Mungu. Siku haya makosa yakisababisha hii ferry kumwaga ndugu zako baharini utakuja hapa na kusema kuwa ni sawa kabisa kwa vile mmiliki wa hiyo converted ferry ni mcha Mungu?

Maybe You know deep secrets... naturally...

"He will win who knows when to fight and when not to fight"
 
Ferry ni meli/ boat ya abiria...What matters is the built and capacity... Yes, not all ferries built for high seas but some are. Remember that ferry sailed from Greece to Zanzibar.

Do you know her built and capacity before it was converted?
And what exactly do you mean by "built"? Does this include her conversion as well or only the original built?
The fact that it sailed from Greece to Zanzibar does it make her safe? Spice Icelander ilikujaje?
 


HIZO NDEGE za MATAIFA ya NJE ni VIGUMU kubeba MATAKATAKA toka Tanganyika kwenda Zanzibar

Sasa hizi MELI zinabeba hadi vitunguu, kandambili bure KWENDA ZANZIBAR... Sasa Umeona MELI TOKA MOMBASA

Kwenda ZANZIBAR inavyochunguzwa? na watu wanavyopakulikwa kama NONDO?

NO MORE FREELANCE free Movement of People and GOODS; So Damn Many RESTRICTIONS kama ni NCHI KWA NCHI

Tangu lini Unapata KUNGU toka MOMBASA ???

As long as Tanganyika na Zanzibar ziko karibu ki-jeografia safari za meli zitakuwepo. Kuwepo au kutokuwepo kwa Muungano hakutazuwia hili. Wakati Mv , Mapinduzi (meli ya serikali ya Zanzibar) ilipokua bado nzima ,ilikua ikifanya safari za Zanzibar, Dar, Tanga, Mombasa na Comoro.
 
Just like you know the owner's faith secrets deeply.

"Make your character good for the people." --- Prophet Muhammad (s) as narrated Al-Muwatta, Volume 47, Hadith 1
 

"Make your character good for the people." --- Prophet Muhammad (s) as narrated Al-Muwatta, Volume 47, Hadith 1

And lawful characters tell the truth, keep their word, respect authority, honor tradition, and judge those who fall short of their duties.
 
Huyu ndiyo Mtanzania wa kweli. Ingawa ice cream soda na maji yake hayalipiwi kodi lakini wananchi wananufaika. Keep it up bro.
 
Inachuka abiria 1,500, sasa subiri iko siku watakuwa 10,000

Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi Zanzibar

attachment.php


Kampuni ya Azam Marine inayomiliki boti ziendazo kasi hapa nchini, leo imeingiza meli mpya na ya kisasa itakayochukua zaiidi ya abiria 1500 na magari 200. Meneja Mkuu wa Kamuni ya Azam Marine, Bw. Hussein Mohammed Saidi, amesema leo mjini Zanzibar kuwa meli hiyo ambayo itafanya safari zake kati ya Dar es Salaam, zanzibar na Pemba itatoza nauli nafuu kwa abiria wake.

Amesema meli hiyo ambayo inatarajiwa kuanza safari zake mara baada ya kukamilisha taratizo za mamlaka mbalimbali. Meli hiyo inayoitwa AZAM SEALINKI ni ya kisasa katika ukanda huu wa Mwambao wa nchi za Kusini na Pembe ya Afrika.

Bw. Hussein amesema Meli hiyo ambayo imetengenezwa nchini Ugiriki na inatayarishiwa eneo maalumu litakalotumika kwa kupakia na kushusha abiria na mizigo yakiwemo magari. Amesema meli hiyo itasafiri kwa muda wa saa tatu kutoka Dar es salaam na Zanzibar na saa 4 kutoka Zanzibar na Pemba ama saa 7 kutoka dar es salaam na Pemba.

Amesema pamoja na kuwasili kwa Meli hiyo, Kampuni ya Azam pia inatarajia kuleta meli nyingine ya abiiria inayojulikana kama Kilimanjaro namba 4.

Kwa upande wao, baadhi ya wananchi wa Visiwa vya zanzibar wamepongeza ujio wa meli hiyo lakini wakaitaka serikali kuendelea kudhibiti uingizwaji wa meli chakavu na kukuu ili kuepuka uwezekano wa kutokea ajali za mara kwa mara.

Bwana Rajabu Khamisi mkazi wa Pemba na Bi. Rehema Omari wa mjini Zanzibar, wamesema kuna haja ya Serikali kusimamia ukomo wa nauli ili kila mwananchi aweze kusafiri kutoka sehemu moja na nyingine kwani wamesema vipato havilingani.
 
Meneja wa Kampuni ya Meli za Azam Marine,m Husssein M Said, akizungumza na Waandishi wa habari katika bandari ya Malindi Zanzibar wakati wa kuwasili meli yao mpya ya Sea Link katika bandari ya Malindileo mchana.​

Meli hiyo ikitokea nchi Ugiriki ilikotengenezwa meli hiyo itaanza kazi baada ya kumaliza taratibu zote za Kisheria za Baharini na Taasisi husika kukaguliwa kwa kupata leseni ya kuchukulia abiria na mizigo.

Amesema meli hiyo ina uwezo wa kuchukuwa abiria 1500 na mizigo pamoja ya magari 270 kwa wakati mmoja,na itaanza safari zake baada ya kupata kibali na kufanyiwa ukaguzi.


Amesema itafanya safari zake kati ya Unguja Pemba na Dar-es-Salaam hivi karibuni ili kuondoa tatizo la usafiri wa maji kati ya visiwa vya Pemba na Unguja ambako kuna tatizo la usafiri, tangu kutokea kwa ajili ya meli kuzama na baadhi ya meli kufutiwa leseni zao kuchukuwa abiria kutokana na vyombo hivyo haviko katika hali ya kutowa huduma kwa wananchi.


Wananchi wamefarijika kuona meli hiyo katika bandari ya Zanzibar na kuona tatizo la Usafiri kati ya Unguja na Pemba limepata ufumbuzi baada ya kuwasili meli hiyo na kuwa na imani na huduma yake itakuwa nzuri na ya kuridhisha.

Wananchi pia wamewataka wafanyabiashara kupunguza nauli za vyombo ili kila mwananchi aweze kumudu huduma hiyo na wasiwe katika biashara zaidi kuliko kutowa huduma kwa wananchi wa hali ya chini ambao hutegemea usafiri huo.


Nae Meneja Hussein Said amesema meli yao itakuwa katika kutowa huduma zaidi kuliko biashara ili kuona kila Mwananchi anafaidika na huduma zao na wataweka nauli za bei nafuu kwa wananchi hao ili kuweza kutowa huduma za uhakika na safi wakati wate wa safari zao.


Na kuwataka Wananchi kuwa na subira kama walivyokuwa kwa muda mrefu kupata ufumbuzi wa tatizo lao la usafiri karti ya pande hizi mbili za Visiwa, na kuwataka kupokea huduma zao kwa furaha wakati wote wa safari zao.





Imewekwa na MAPARA at 5:48 PM
 
Back
Top Bottom