crabat
JF-Expert Member
- Dec 28, 2012
- 4,323
- 2,210
Siyapendi mazungumzo ya huyu Maalim Seif, anaitwa na anakwenda kuongea mambo ya msingi yanayohusu wananchi kama vile anaongea na babaake mdogo.
Amekosa Protocol ya kichama wakimaliza kuongea wanamgeuka, anafanya siasa za kizamani washauri wake dhaifu au ni mbishi?
Anafanya vikao na viongozi zaidi ya 4 wa ulibzani wake yeye yuko pekeyake anamaslahi gani kwa kura za waliomchagua?
Nina wacwac na uongozi wa huyu Maalim?
Ukiona Hivyo ujue nani Maalim...The Hulk...the Superman..haahahah you call him the Shakespear , you name him he fit the suit.
Mmoja kwa watano anawakabili peke yake hataki mambo yavuje , yatatoka yakiwa tayari.
wewe humjui SEIF , Huyu 1986 alikua Chief Minister , wakataka kumdhuru akaenda kutibiwa njee
alipo rudi akapokewa na umati wa Wazanzibari na Maneno yake aliwambia nitawatumikia na kudai haki zenu nikiwa ndani ya ccm au nje ya ccm.
baada ya maneno hayo akaachishwa Uchifu minister na baadae akavuliwa Uwanachama wa ccm.
Mwalimu Nyerere alitangaza mwenyewe kumfukuza na alimkubali kwa kusema na kijichekesha kuwa aaah huyu amepokelewa na wapenzi wake wengi sana sana...!!!!
baadae Seif akakamatwa na kutiwa ndani kwa kesi za kutunga na kukaa ndani jela ya mateso kwa zaidi ya miaka 3.
Serikali ya ujerumani haikupendezwa na hili haswa aliyekua balozi wao hapa aliitaka serikali imwachie haraka na akaaachiwa.
alitoka afya yake imezorota sana lakini akajiunga tena katika harakati za ukombozi wa znz na bado haja choka yupo anadai na ni kiongozi shupavu hakuna mfano wake.
ndio maana yeye mmoja tu atosha hata ccm 100...wakae wamzunguke hoja zake na busara zake ni uhakika na ukweli . ni mstaahamilivu mnooooo
tusubiri ila wakifanya hiana ccm , la uhakika Maalim mara hii watamuona mbaya hakubali democracia ikachezewa kwa manufaa ya kikundi kidogo ..Time will tell