Zanzibar inaharibu sifa ya Tanzania

Zanzibar inaharibu sifa ya Tanzania

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,768
Reaction score
49,934
Ni wakati wa kutafakari faida za Muungano. Na kama zipo, ni muhimu kuwa na Muungano imara ambao tunakubaliana uwe ni Muungano wa namna gani.

Fikiria kuwa mikopo yote inatafutwa kwa jina la Tanzania, ambayo kimsingi ni Tanganyika. Na siku zote anayekopa ndiye anayedaiwa. Lakini pesa hiyo ya mkopo inapelekwa kuijenga Zanzibar, kuna wakati Zanzibar imepewa mpaka 20% ya mkopo.

Wakati Tanzania inahangaika kutafuta mikopo na misaada, inahangaika kuvutia wawekezaji, inahangaika na kufanya jitihada kubwa kuvutia watalii, Zanzibar inadidimiza sekta ya utalii kwa kufanya matendo ambayo kwa vyovyote, yatafifisha utalii.

Huko Zanzibar, watalii wamezuiwa kula hadharani. Ikumbukwe hawa watalii, hawakwenda Zanzibar wakashinde vyumbani, kutalii ni kuzunguka na kutembelea maeneo mbalimbali, na wanapotembea, wengine huwa na lunch boxes zao au snacks kama biscuits, n.k. Wamelipa gharama zote, hawakuambiwa kuwa wakifika Zanzibar wote watalazimishwa kufunga au kwenda kulia snacks zao vyooni/mafichoni. Wanaenda kukutana na karaha hii wakiwa wamefika Zanzibar.

Dini ni suala binafsi halitakiwi kulazimishwa kwa mtu mwingine. Anayekula hadharani, kwani amekuwekea wewe chakula mdomoni hata uumizwe na kula kwake? Wewe umeamua kuacha kula mchana kwa kipindi fulani, na kuamua kula wakati wa usiku, kwa nini uwalazimishe na wengine kufanya hivyo hivyo?

Nilitarajia kufunga kungeendana na matendo mema, lakini inaonekana ni kinyume chake kwa upande wa Zanzibar. Je, wanaoendekeza hayo, wamefunga au ni wanafiki wanaotaka kuharibu Taifa kwa mgongo wa dini?

Serikali ya Zanzibar ijitafakari. Haiwezekani Zanzibar wafanye matendo yanayofifisha uchumi wa nchi, halafu wakiwa katika uduni wa uchumi, mzigo unaangukia kwa nchi nzima kuwaokoa.

Tusiwe wanafiki, tukemee kwa nguvu zote unafiki unaoendelea Zanzibar. Kama Zanzibar, haitaki wageni, wanataka kila mmoja akifika Zanzibar awe muislam, waitangazie Dunia, na siyo kuwakerehesha watu wakati tayari wakiwa wamefika Zanzibar.

Sheria za nchi zifuatwe. Nchi yetu inatoa uhuru wa kila mtu kufuata imani yake na yale anayotaamini kwa kadiri ya mafundisho ya dini anayoiamini, bila ya kuingilia uhuru wa mtu mwingine, alimradi uhuru huo usikiuke sheria za nchi.
 
Muungano upo ili kuiweka TZ salama. Imagine baada ya kuvunja muungano utashangaa makundi ya kigaidi yanasogea Zanzibar kwa kuweka kambi kabisa. Wakishasogea hapo jua tu usalama wetu utakua mashakani sana. Nasema hivyo kwa maana Zanzibar inaweza rasimishwa kama Islamic state na ikawa inapokea mafao ivyo isiwe na uhuru mkubwa wa kimaamuzi kwenye mambo ya kiusalama na uchumi wake
 
Suala la nchi/Zanzibar nzima kufungishwa kwa lazima kipindi cha Ramadan lingekuwepo kisheria au kikatiba lingesaidia sana watalii na wengine wasiohusika kukaa mbali na Zanzibar kipindi hiko.

Haifai kuwategea watu wafike kwako kisha unawaletea mambo ya ajabu ajabu kwa kisingizio cha mila, desturi, na utamaduni wa Zanzibar!

If Zanzibar is for one religion only let it be known so formally! Hili suala liingizwe kwenye Katiba au litungiwe sheria ili liwe clear to everyone.
 
Ni wakati wa kutafakari faida za Muungano. Na kama zipo, ni muhimu kuwa na Muungano imara ambao tunakubaliana uwe ni Muungano wa namna gani.

Fikiria kuwa mikopo yote inatafutwa kwa jina la Tanzania, ambayo kimsingi ni Tanganyika. Na siku zote anayekopa ndiye anayedaiwa. Lakini pesa hiyo ya mkopo inapelekwa kuijenga Zanzibar, kuna wakati Zanzibar imepewa mpaka 20% ya mkopo.

Wakati Tanzania inahangaika kutafuta mikopo na misaada, inahangaika kuvutia wawekezaji, inahangaika na kufanya jitihada kubwa kuvutia watalii, Zanzibar inadidimiza sekta ya utalii kwa kufanya matendo ambayo kwa vyovyote, yatafifisha utalii.

Huko Zanzibar, watalii wamezuiwa kula hadharani. Ikumbukwe hawa watalii, hawakwenda Zanzibar wakashinde vyumbani, kutalii ni kuzunguka na kutembelea maeneo mbalimbali, na wanapotembea, wengine huwa na lunch boxes zao au snacks kama biscuits, n.k. Wamelipa gharama zote, hawakuambiwa kuwa wakifika Zanzibar wote watalazimishwa kufunga au kwenda kulia snacks zao vyooni/mafichoni. Wanaenda kukutana na karaha hii wakiwa wamefika Zanzibar.

Dini ni suala binafsi halitakiwi kulazimishwa kwa mtu mwingine. Anayekula hadharani, kwani amekuwekea wewe chakula mdomoni hata uumizwe na kula kwake? Wewe umeamua kuacha kula mchana kwa kipindi fulani, na kuamua kula wakati wa usiku, kwa nini uwalazimishe na wengine kufanya hivyo hivyo?

Nilitarajia kufunga kungeendana na matendo mema, lakini inaonekana ni kinyume chake kwa upande wa Zanzibar. Je, wanaoendekeza hayo, wamefunga au ni wanafiki wanaotaka kuharibu Taifa kwa mgongo wa dini?

Serikali ya Zanzibar ijitafakari. Haiwezekani Zanzibar wafanye matendo yanayofifisha uchumi wa nchi, halafu wakiwa katika uduni wa uchumi, mzigo unaangukia kwa nchi nzima kuwaokoa.

Tusiwe wanafiki, tukemee kwa nguvu zote unafiki unaoendelea Zanzibar. Kama Zanzibar, haitaki wageni, wanataka kila mmoja akifika Zanzibar awe muislam, waitangazie Dunia, na siyo kuwakerehesha watu wakati tayari wakiwa wamefika Zanzibar.

Sheria za nchi zifuatwe. Nchi yetu inatoa uhuru wa kila mtu kufuata imani yake na yale anayotaamini kwa kadiri ya mafundisho ya dini anayoiamini, bila ya kuingilia uhuru wa mtu mwingine, alimradi uhuru huo usikiuke sheria za nchi.
Ndo
Ni wakati wa kutafakari faida za Muungano. Na kama zipo, ni muhimu kuwa na Muungano imara ambao tunakubaliana uwe ni Muungano wa namna gani.

Fikiria kuwa mikopo yote inatafutwa kwa jina la Tanzania, ambayo kimsingi ni Tanganyika. Na siku zote anayekopa ndiye anayedaiwa. Lakini pesa hiyo ya mkopo inapelekwa kuijenga Zanzibar, kuna wakati Zanzibar imepewa mpaka 20% ya mkopo.

Wakati Tanzania inahangaika kutafuta mikopo na misaada, inahangaika kuvutia wawekezaji, inahangaika na kufanya jitihada kubwa kuvutia watalii, Zanzibar inadidimiza sekta ya utalii kwa kufanya matendo ambayo kwa vyovyote, yatafifisha utalii.

Huko Zanzibar, watalii wamezuiwa kula hadharani. Ikumbukwe hawa watalii, hawakwenda Zanzibar wakashinde vyumbani, kutalii ni kuzunguka na kutembelea maeneo mbalimbali, na wanapotembea, wengine huwa na lunch boxes zao au snacks kama biscuits, n.k. Wamelipa gharama zote, hawakuambiwa kuwa wakifika Zanzibar wote watalazimishwa kufunga au kwenda kulia snacks zao vyooni/mafichoni. Wanaenda kukutana na karaha hii wakiwa wamefika Zanzibar.

Dini ni suala binafsi halitakiwi kulazimishwa kwa mtu mwingine. Anayekula hadharani, kwani amekuwekea wewe chakula mdomoni hata uumizwe na kula kwake? Wewe umeamua kuacha kula mchana kwa kipindi fulani, na kuamua kula wakati wa usiku, kwa nini uwalazimishe na wengine kufanya hivyo hivyo?

Nilitarajia kufunga kungeendana na matendo mema, lakini inaonekana ni kinyume chake kwa upande wa Zanzibar. Je, wanaoendekeza hayo, wamefunga au ni wanafiki wanaotaka kuharibu Taifa kwa mgongo wa dini?

Serikali ya Zanzibar ijitafakari. Haiwezekani Zanzibar wafanye matendo yanayofifisha uchumi wa nchi, halafu wakiwa katika uduni wa uchumi, mzigo unaangukia kwa nchi nzima kuwaokoa.

Tusiwe wanafiki, tukemee kwa nguvu zote unafiki unaoendelea Zanzibar. Kama Zanzibar, haitaki wageni, wanataka kila mmoja akifika Zanzibar awe muislam, waitangazie Dunia, na siyo kuwakerehesha watu wakati tayari wakiwa wamefika Zanzibar.

Sheria za nchi zifuatwe. Nchi yetu inatoa uhuru wa kila mtu kufuata imani yake na yale anayotaamini kwa kadiri ya mafundisho ya dini anayoiamini, bila ya kuingilia uhuru wa mtu mwingine, alimradi uhuru huo usikiuke sheria za nchi.
Kwani ndo umeanza kujua hilo leo!
Ni utamaduni wa wazanzibari miaka mingi na hauna madhara
 
Muungano upo ili kuiweka TZ salama. Imagine baada ya kuvunja muungano utashangaa makundi ya kigaidi yanasogea Zanzibar kwa kuweka kambi kabisa. Wakishasogea hapo jua tu usalama wetu utakua mashakani sana. Nasema hivyo kwa maana Zanzibar inaweza rasimishwa kama Islamic state na ikawa inapokea mafao ivyo isiwe na uhuru mkubwa wa kimaamuzi kwenye mambo ya kiusalama na uchumi wake
We ni William Lukuvi nn.
Mana nliona clip yake ina maneno kama haya
 
These barbaric acts officially inform the international community that in Zanzibar there is religious terrorism led by muslims.
 
Ndo

Kwani ndo umeanza kujua hilo leo!
Ni utamaduni wa wazanzibari miaka mingi na hauna madhara

Huwezi kusema hauna madhara. Hujui kwa taratibu za ajabu zisizofuata sheria za nchi zimewafanya watu wangapi wasije Tanzania. Mtalii anaweza kuja Tanzania, akafanyiwa hivyo vitimbwi, na baada ya hapo akasema tu kuwa nchi hii ni ya washenzi, siendi tena, na akawajulisha wale anaowafikia. Huku mnaendelea kuhangaika na kutengeneza filamu, halafu msipate matokeo yoyote ya maana. Wataongezeka watu 10,000, kumbe msingekuwa na mambo ya kipuuzi, wangeongezeka watu 100,000.

Tanzania pamoja na vyote vinavyoitwa vivutio inatembelewa na watalii wachache sana ukilinganisha na mataifa baadhi ya Afrika, kama Kenya, South Africa, Egypt, Morroco na Tunisia.
 
Ni wakati wa kutafakari faida za Muungano. Na kama zipo, ni muhimu kuwa na Muungano imara ambao tunakubaliana uwe ni Muungano wa namna gani.

Fikiria kuwa mikopo yote inatafutwa kwa jina la Tanzania, ambayo kimsingi ni Tanganyika. Na siku zote anayekopa ndiye anayedaiwa. Lakini pesa hiyo ya mkopo inapelekwa kuijenga Zanzibar, kuna wakati Zanzibar imepewa mpaka 20% ya mkopo.

Wakati Tanzania inahangaika kutafuta mikopo na misaada, inahangaika kuvutia wawekezaji, inahangaika na kufanya jitihada kubwa kuvutia watalii, Zanzibar inadidimiza sekta ya utalii kwa kufanya matendo ambayo kwa vyovyote, yatafifisha utalii.

Huko Zanzibar, watalii wamezuiwa kula hadharani. Ikumbukwe hawa watalii, hawakwenda Zanzibar wakashinde vyumbani, kutalii ni kuzunguka na kutembelea maeneo mbalimbali, na wanapotembea, wengine huwa na lunch boxes zao au snacks kama biscuits, n.k. Wamelipa gharama zote, hawakuambiwa kuwa wakifika Zanzibar wote watalazimishwa kufunga au kwenda kulia snacks zao vyooni/mafichoni. Wanaenda kukutana na karaha hii wakiwa wamefika Zanzibar.

Dini ni suala binafsi halitakiwi kulazimishwa kwa mtu mwingine. Anayekula hadharani, kwani amekuwekea wewe chakula mdomoni hata uumizwe na kula kwake? Wewe umeamua kuacha kula mchana kwa kipindi fulani, na kuamua kula wakati wa usiku, kwa nini uwalazimishe na wengine kufanya hivyo hivyo?

Nilitarajia kufunga kungeendana na matendo mema, lakini inaonekana ni kinyume chake kwa upande wa Zanzibar. Je, wanaoendekeza hayo, wamefunga au ni wanafiki wanaotaka kuharibu Taifa kwa mgongo wa dini?

Serikali ya Zanzibar ijitafakari. Haiwezekani Zanzibar wafanye matendo yanayofifisha uchumi wa nchi, halafu wakiwa katika uduni wa uchumi, mzigo unaangukia kwa nchi nzima kuwaokoa.

Tusiwe wanafiki, tukemee kwa nguvu zote unafiki unaoendelea Zanzibar. Kama Zanzibar, haitaki wageni, wanataka kila mmoja akifika Zanzibar awe muislam, waitangazie Dunia, na siyo kuwakerehesha watu wakati tayari wakiwa wamefika Zanzibar.

Sheria za nchi zifuatwe. Nchi yetu inatoa uhuru wa kila mtu kufuata imani yake na yale anayotaamini kwa kadiri ya mafundisho ya dini anayoiamini, bila ya kuingilia uhuru wa mtu mwingine, alimradi uhuru huo usikiuke sheria za nchi.
Pole sana
 
Muungano upo ili kuiweka TZ salama. Imagine baada ya kuvunja muungano utashangaa makundi ya kigaidi yanasogea Zanzibar kwa kuweka kambi kabisa. Wakishasogea hapo jua tu usalama wetu utakua mashakani sana. Nasema hivyo kwa maana Zanzibar inaweza rasimishwa kama Islamic state na ikawa inapokea mafao ivyo isiwe na uhuru mkubwa wa kimaamuzi kwenye mambo ya kiusalama na uchumi wake
Ona huyu nae magaidi wanaingia Marekani na Urusi sembuse huku mwisho wa dunia.
 
Wakili Hassan Kijogoo afafanua hakuna sheria inayozuia watu kula hadharani Zanzibar, hivyo ashauri wanaotamani sheria hiyo iwepo basi wapeleke hoja ili itungwe lakini hadi sasa hakuna sheria kama hiyo inatokataza watu kula hadharani mchana.

WAKILI MSOMI HASSAN KIJOGOO : WALIOKAMATWA KWA KULA MCHANA ZANZIBAR, 'WANAWAONEA'


View: https://m.youtube.com/watch?v=Eu0V9V2_Z2Y
 
TOKA MAKTABA :

Kamanda Ataja majina na kabila za waliokamatwa wakila hadharani


View: https://m.youtube.com/watch?v=l4mmqjdRX3o
Maafisa wa polisi visiwani Zanzibar wametangaza kuwakamata watu 12 kwa tuhuma za kukiuka utaratibu wa dini ya Kiislamu kwa kula mchana hadharani kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Abubakar Khamis Ally amesema kufuatia video iliyosambaa mitandaoni ikiwaonyesha baadhi ya watu katika eneo la viwanja vya mnazi mmoja Zanzibar kula hadharani wakati wa mchana wa Ramadhani, Jeshi hilo lilifanya msako na kuwakamata watu wapatao kumi na wawili wakiwa na vielelezo ambapo amesema wanaendelea na taratibu nyengine ili kuwafikisha Mahakamani.

Waliokamatwa ni pamoja na Issa Hamad Juma (40) wa Kikwajuni, Hamad Indole (25) wa Mtwara, , Hashimu Bakari Nassoro (35) wa Kwarara, Selemani Ismail Nalinga (34) wa Magogoni na wengine 8 wote wametupwa mahabusu kituo cha Polisi Madema huku uchunguzi ukiendelea kwa ajili mashitaka wawe kuwafikishwa mahakamani...
 
Hili ni bandiko kwa ajili ya watu wenye akili kubwa. Kama mada imekuzidi uzito kaa pembeni au uliza ujifunze
Akili gani sasa hapo umetumia zaidi ya kuandika uozo. Wakati magaidi wakifanya yao hapa Dar huo muungano ulienda likizo, acha hoja za kitoto. Huo muungano una wenye nao.
 

Zanzibar​

March 29, 2024​

Kamisheni ya utalii Zanzibar yaipiga faini kampuni ya utalii kwa kuruhusu wageni kula hadharani Zanzibar​

Kamisheni ya Utalii Zanzibar imethibitisha kuipiga faini ya dola 500 kampuni ya utalii ya Organisateur Francophone Tours and Travel kwa kuruhusu watalii kula hadharani katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan.

Katika taarifa kwa umma Afisa Uhusiano wa Tume ya Utalii Zanzibar Mohamed Nassor Bajuni alisema kampuni hiyo ilikiuka miongozo na maagizo yaliyotolewa kwa wafanyabiashara wa utalii wakati huu wa mfungo wa Ramadhani.

"Toka kuanzishwa kwa kamisheni huo tunatoa notisi maalumu kwa kipindi cha mwezi wa Ramadhani kuhusiana na suala hili" alisema Bw.Mohamed.

Muongoza watalii wa kampuni hiyo, Khamis M. Kahogo pia amezuiliwa kufanya shughuli zozote za utalii kwa muda wa miezi mitatu," aliongeza kusema.

Kamisheni hiyo imesisitiza umuhimu wa kufuata desturi na mila za visiwa vya Zanzibar hasa wakati huu wa mfungo wa Ramadhan
 
Ni wakati wa kutafakari faida za Muungano. Na kama zipo, ni muhimu kuwa na Muungano imara ambao tunakubaliana uwe ni Muungano wa namna gani.

Fikiria kuwa mikopo yote inatafutwa kwa jina la Tanzania, ambayo kimsingi ni Tanganyika. Na siku zote anayekopa ndiye anayedaiwa. Lakini pesa hiyo ya mkopo inapelekwa kuijenga Zanzibar, kuna wakati Zanzibar imepewa mpaka 20% ya mkopo.

Wakati Tanzania inahangaika kutafuta mikopo na misaada, inahangaika kuvutia wawekezaji, inahangaika na kufanya jitihada kubwa kuvutia watalii, Zanzibar inadidimiza sekta ya utalii kwa kufanya matendo ambayo kwa vyovyote, yatafifisha utalii.

Huko Zanzibar, watalii wamezuiwa kula hadharani. Ikumbukwe hawa watalii, hawakwenda Zanzibar wakashinde vyumbani, kutalii ni kuzunguka na kutembelea maeneo mbalimbali, na wanapotembea, wengine huwa na lunch boxes zao au snacks kama biscuits, n.k. Wamelipa gharama zote, hawakuambiwa kuwa wakifika Zanzibar wote watalazimishwa kufunga au kwenda kulia snacks zao vyooni/mafichoni. Wanaenda kukutana na karaha hii wakiwa wamefika Zanzibar.

Dini ni suala binafsi halitakiwi kulazimishwa kwa mtu mwingine. Anayekula hadharani, kwani amekuwekea wewe chakula mdomoni hata uumizwe na kula kwake? Wewe umeamua kuacha kula mchana kwa kipindi fulani, na kuamua kula wakati wa usiku, kwa nini uwalazimishe na wengine kufanya hivyo hivyo?

Nilitarajia kufunga kungeendana na matendo mema, lakini inaonekana ni kinyume chake kwa upande wa Zanzibar. Je, wanaoendekeza hayo, wamefunga au ni wanafiki wanaotaka kuharibu Taifa kwa mgongo wa dini?

Serikali ya Zanzibar ijitafakari. Haiwezekani Zanzibar wafanye matendo yanayofifisha uchumi wa nchi, halafu wakiwa katika uduni wa uchumi, mzigo unaangukia kwa nchi nzima kuwaokoa.

Tusiwe wanafiki, tukemee kwa nguvu zote unafiki unaoendelea Zanzibar. Kama Zanzibar, haitaki wageni, wanataka kila mmoja akifika Zanzibar awe muislam, waitangazie Dunia, na siyo kuwakerehesha watu wakati tayari wakiwa wamefika Zanzibar.

Sheria za nchi zifuatwe. Nchi yetu inatoa uhuru wa kila mtu kufuata imani yake na yale anayotaamini kwa kadiri ya mafundisho ya dini anayoiamini, bila ya kuingilia uhuru wa mtu mwingine, alimradi uhuru huo usikiuke sheria za nchi. 8
Alafu tunadai kero za muungano zimekwisha tatuliwa kweli
 
Back
Top Bottom