Zambia: Mchungaji aliyeomba kuzikwa ili afufuke siku ya 3 kama Yesu akutwa amefariki dunia

Kama unamjua uyu jamaa,

Hawa wachungaji wa kisasa matapeli watapata KAZI Sana kukushika Akili.

Uyu jamaa aliwahi kuzikwa hai, ata sikU tatu hazikufika tayar akafufuka

Uyu jamaa aliwahi kutembea juu ya maji

Uyu jamaa aliwahi kuficha tembo kwenye mfuko wa shati

Uyu jamaa aliwahi kusagwa na mashine ya mbao vipande vipande na akarudi kua hai bila hata kovu moja

Uyu jamaa aliwahi kubadili majani kua Pesa na akanunua bidhaa

UYU MWAMBA AKILI MINGI MNO
images-352.jpg
 
Hahahahahaaa Aisee Hivi waafrika ni nani katuloga,Kuna mambo yanashangaza Sana hapo misukule kabla hajafanya huo upupu wanasema kavuviwa na roho mtakatifu
Amina!

Shwaini!
 
Kama alitumia jeneza bila shaka huyu jamaa alikufa ndani ya dk 15 tu baada ya udongo kuziba mbao za jeneza.

Soma hii huku ukiimagine kwa nguvu zako zote.

Baada ya kuingia kwenye jeneza na kufungiwa alijiamini sababu bado aliweza kupumua kupitia penyo za mbao.

Then wakamshusha kwenye shimo la futi 6 na kuanza kufukiwa na udongo mzito wa ufinyanzi.
Baada ya dk 5 za kwanza udongo ukaanza kuenea juu ya mlango wa jeneza huku wafukiaji wakiongeza speed ya ufukiaji then dk ya 7 mlango wa jeneza ulikuwa tayari umeshazibwa entirely.

Dk 8 jamaa akaanza kuhisi hewa inaanza kuwa nzito taratibu huku akianza kupumua kwa tabu sababu oxygen iliyokuwepo ndani ya jeneza ilianza kupungu na carbon dioxide kuanza kuenea ndani ya jeneza.

Dk 9 jamaa akaanza kupiga kelele za kufunguliwa na kupiga mlango wa jeneza kwa nguvu zote ili wamfukue.

Kibaya wafukuaji waliendelea na shughuli ya kufukia kwa kasi na kushindwa kumsikia jamaa sababu sauti ilishindwa kupita kutoka ndani ya jeneza kuja juu ni zaidi ya soundproof.

Kibaya zaidi ni kwamba alishindwa kupiga kelele sababu hakuweza tena kupumua na aliishia kufurukuta mdomo wake ukiwa wazi akiugulia maumivu makali huku nguvu za kupiga mlango wa jeneza zikimuishia sababu ubongo ulianza kukosa nguvu kwa lack of oxygen na jamaa kuanza kusikia kizunguzungu na jasho jingi likiwa limejaa ndani ya jeneza kutokana na joto la ardhi na kitendo cha yeye kufukiwa na kukosa hewa kutoka nje.

Dk ya 13 jamaa alikuwa akiendelea kufurukuta na kutetemeka kama mtu mwenye kifafa then alitulia mdomo ukiwa wazi kama mamba anayeota jua huku macho yamemtoka na taratibu akianza kukosa fahamu kwa maumivu makali sababu ubongo ulikuwa ukivuta kutokana na kukosa hewa na energy huku maumivu ya kichwa kuwa makali kupitiliza.

Dk ya 14 jamaa akapoteza fahamu kabisa na dk ya 15 kufa kifo kibaya sana.

Hollow movie hiyo hapo!
Nimeimagine kilichotokea.

Pia kuna movie moja ya Ryan Reynolds inahusu hivihivi walimzika hai.

Bongo movie kuweni wabunifu script na story hivyo hapo siyo kila siku mdada tajiri kampenda kapuku wa mbagala, simple location, simple cameras na simple lighting na budget ndogo tu.

Actually ina maana huyu jamaa ameshindwa kujua kwamba binadamu akikosa oxygen basi atakufa kwa suffocation?

Alafu cha ajabu atakuwa na degree hapo.
 
Back
Top Bottom