Zambia inaangamia kwa Kimeta. Waziri Ulega hakikisheni mnachukua tahadhari zote huko Rukwa, Songwe na Mbeya

Investigation Unit

Senior Member
Nov 26, 2023
164
223
IMG-20240107-WA0133.jpg

Moja kwa Moja kwenye mada,

Hapana Nakonde Zambia hali ni mbaya, Ugonjwa wa Kimeta unapukutisha watu na mifugo,

Watu wanaopenda kulà nyama na wanaoishi mikoa ya Rukwa,Mbeya na Songwe kuweni makini sana na ugonjwa huu unaua tena kwa kasi zaidi ya Korona.

Ukila nyama ya mnyama mwenye ugonjwa huu na wewe utakuwa katika hatari ya kupata ugonjwa huu.

Dalili za huu ugonjwa mtu anakuwa kama kamwagiwa maji ya moto na anaanza kuvuka ngozi hakika huu ugonjwa ni wahatari sana.

Kulingana na WHO, kesi 26 kati ya 60 zinazoshukiwa nchini Zambia zinatokana na "ulaji wa nyama iliyochukuliwa kutoka kwa mizoga ya viboko, ngo'mbe na Mbuzi.

Shirika hilo limeonya juu ya hatari "kubwa" ya ugonjwa wa Kimeta kuenea katika nchi jirani hasa Tanzania, kutokana na "mienendo ya mara kwa mara (ya kuvuka mpaka) ya watu na wanyama."

Kando na Zambia, Kenya, Malawi, Uganda na Zimbabwe pia zimerekodi visa vya Kimeta mwaka huu, na jumla ya vifo 20 na visa vingine 1,100 vinavyoshukiwa.

Naziomba mamlaka za Tanzania hasa Waziri wa mifugo na yule wa Afya kuhakikisha anachukua tahadhari zote kupambana na ugonjwa hasa katika mikoa ya pembezoni na iliyo mipakani mwa Tanzania na Zambia,

Ugonjwa huu hauna tiba thabiti mpaka sasa ila unatokomezwa kwa kuwapa chanjo mifugo kama kitimoto, ngo'mbe, Mbuzi, Punda etc

#Kila mmoja chukua tahadhari maisha ni mali yako sio ya Serikali.

Mungu ibariki Tanzania na walaji wote wa nyama.

Cc: Waziri Ummy Mwalimu,
Waziri Ulega
Waziri Mkuu,
 
Shirika hilo limeonya juu ya hatari "kubwa" ya ugonjwa wa Kimeta kuenea katika nchi jirani hasa Tanzania, kutokana na "mienendo ya mara kwa mara (ya kuvuka mpaka) ya watu na wanyama."

Kando na Zambia, Kenya, Malawi, Uganda na Zimbabwe pia zimerekodi visa vya Kimeta mwaka huu, na jumla ya vifo 20 na visa vingine 1,100 vinavyoshukiwa.
Ummy yuko wapi?
 
Karantini ya mifugo kwa maeneo hayo iwekwe mara moja kuepusha kuenea kwa ugonjwa huo hatari.
 
Tanzania nchi yangu ,tuwe tunajifunza kwa wenzetu, tuelewe kuwa Kinga ni bora kuliko kutibia,idadi ya mifugo tuliyokua nayo haipishani sana na ya Botswana, sasa angalia wenzetu walivyo makini na maradhi ya mifugo kuliko sisi, wenzetu njia zote zinazoingia Botswana wamechimba ki pool ambacho gari lazima ipitie pale na binadamu lazima watoke na kukanyaga dawa ,na viatu vyote vya ziada, pale tunduma ilitakiwa nasi tujenge ki pool hiki, uki cross tu kutoka zambia lazima upitie hapa ili kuzuia maambukizi haya,sasa tutafanya kazi kama zimamoto brigade!!!
 
Kwahiyo Kimeta hakipiti pia?
Nzige walikuja Hadi hapo mpakani Kilimanjaro na kurudi,

Korona ilifukuzwa duniani Kutokea Tanzania.

Kuna ugonjwa mwingine uliyokuwa na makali zaidi ya Ebola, ulifika mpakani, ukaisha nguvu na kupotea.

Tanzania ni mteuliwa na Mbarikiwa.

Malango ya nchi hayako wazi kama unavyodhani.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Amen
 
Tanzania nchi yangu ,tuwe tunajifunza kwa wenzetu, tuelewe kuwa Kinga ni bora kuliko kutibia,idadi ya mifugo tuliyokua nayo haipishani sana na ya Botswana, sasa angalia wenzetu walivyo makini na maradhi ya mifugo kuliko sisi, wenzetu njia zote zinazoingia Botswana wamechimba ki pool ambacho gari lazima ipitie pale na binadamu lazima watoke na kukanyaga dawa ,na viatu vyote vya ziada, pale tunduma ilitakiwa nasi tujenge ki pool hiki, uki cross tu kutoka zambia lazima upitie hapa ili kuzuia maambukizi haya,sasa tutafanya kazi kama zimamoto brigade!!!
Vipi maisha ya Botswana Ni rafiki Kwa wabongo?
 
Ndio maana ustaarabu Unatakiwa Kwa uhai wa viumbe,Kula mizoga matokeo yake ndio hayo sasa,Allah atuepushe.
 
Vipi maisha ya Botswana Ni rafiki Kwa wabongo?
Yes ila ingilia mlangoni, usiingilie dirishani,kuwa na permit (sio nchi Choo kama ya kwetu),na elewa wapo under 3M tu,kupo super demokrasia imetamalaki, kuko peace sana,ukizidiwa wakati wa driving unaweza lala kwenye military check points au mbele ya kambi ya jeshi!!(nilishawahi kulala pale Pandamatenga barracks, Nika drop name ya Nyerere na kahawa nikapewa)
 
Nzige walikuja Hadi hapo mpakani Kilimanjaro na kurudi,

Korona ilifukuzwa duniani Kutokea Tanzania.

Kuna ugonjwa mwingine uliyokuwa na makali zaidi ya Ebola, ulifika mpakani, ukaisha nguvu na kupotea.

Tanzania ni mteuliwa na Mbarikiwa.

Malango ya nchi hayako wazi kama unavyodhani.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Amen
umesahau na hii.. Kimbunga kilipiga Mozambique ila 🇹🇿 hakikufika.
 
Back
Top Bottom