Suzy Elias
JF-Expert Member
- Nov 9, 2021
- 1,067
- 6,193
Wakati mwingine ujuaji usio na kiasi huweza kumsababishia mhusika matatizo yasiyo ya lazima mbele ya safari ambayo pengine angefika salama.
Haji Manara kwa mfano. Bwana yule hujifanya anayo mengi ayatambuayo. Na kutokuwa kwake makini na ayasemayo, hatimaye yanaelekea kumfitinisha hata na waliopo kwenye mfumo ( serikalini).
Kwa msiofahamu, mapema jana, bwana Haji kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, alidai haoni mantiki ya timu za Taifa kuchangiwa na Wananchi ilhali gharama zote zihusuzo ushiriki wake kwenye mashindano mbalimbali yaliyo chini ya chama cha soka barani Afrika, hugharamikiwa na wao (CAF).
Huenda bwana Haji alikuwa sawa kutoa malalamishi yale, pengine.
Lakini unajiuliza, je, bwana yule hakugundua halibio lile lingewaathiri hata maswahibaye walio ndani ya mpango ule wa upigaji!? Kwamba, Haji hatambui tawi pekee (Serikali) linalomfanya aweze japo kubaki akining'inia asidondoke ndilo hilo ameanza kulitusi eti linamuumiza?
Hakika, naanza kuuona mwisho wa zama za Haji! Na akiendelea kufanya mchezo, hata hizo zama zilizopo ukingoni-zitawahishwa na ujuaji wake usio na kiasi.
Acha muda/mda uwe Mwalimu.
Haji Manara kwa mfano. Bwana yule hujifanya anayo mengi ayatambuayo. Na kutokuwa kwake makini na ayasemayo, hatimaye yanaelekea kumfitinisha hata na waliopo kwenye mfumo ( serikalini).
Kwa msiofahamu, mapema jana, bwana Haji kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, alidai haoni mantiki ya timu za Taifa kuchangiwa na Wananchi ilhali gharama zote zihusuzo ushiriki wake kwenye mashindano mbalimbali yaliyo chini ya chama cha soka barani Afrika, hugharamikiwa na wao (CAF).
Huenda bwana Haji alikuwa sawa kutoa malalamishi yale, pengine.
Lakini unajiuliza, je, bwana yule hakugundua halibio lile lingewaathiri hata maswahibaye walio ndani ya mpango ule wa upigaji!? Kwamba, Haji hatambui tawi pekee (Serikali) linalomfanya aweze japo kubaki akining'inia asidondoke ndilo hilo ameanza kulitusi eti linamuumiza?
Hakika, naanza kuuona mwisho wa zama za Haji! Na akiendelea kufanya mchezo, hata hizo zama zilizopo ukingoni-zitawahishwa na ujuaji wake usio na kiasi.
Acha muda/mda uwe Mwalimu.