Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
Zaidi ya watu 200 nchini Tanzania wameshtakiwa kwa kosa la uhaini siku chache baada ya maandamano ya uchaguzi ambapo upinzani unasema mamia ya watu waliuawa. Haya ni kwa mujibu wa wakili mmoja Peter Kibatala na vyanzo vya mahakama vilivyoliarifu shirika la habari la AFP.
Hapo jana, Kibatala aliiambia AFP kwamba mamia ya watu walifikishwa mahakamani jijini Dar es Salaam.
Idadi ya watu 250 waliowajumuisha wake kwa waume, walishtakiwa kwa kesi tatu tofauti na wote kukabiliwa na mashtaka mawili tofauti.
Shtaka la kwanza ni njama ya kufanya uhaini na la pili ni uhaini wenyewe chanzo.DW Kiswahili
Hapo jana, Kibatala aliiambia AFP kwamba mamia ya watu walifikishwa mahakamani jijini Dar es Salaam.
Idadi ya watu 250 waliowajumuisha wake kwa waume, walishtakiwa kwa kesi tatu tofauti na wote kukabiliwa na mashtaka mawili tofauti.
Shtaka la kwanza ni njama ya kufanya uhaini na la pili ni uhaini wenyewe chanzo.DW Kiswahili