tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Jeshi la Polisi Tanzania limeimarisha maandalizi ya kuhakikisha amani na usalama kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, likionya dhidi ya uchochezi, uzushi na usambazaji wa taarifa zisizo sahihi kwenye mitandao ya kijamii.
Msemaji wa Jeshi hilo, DCP David Misime, amesema zaidi ya askari 4,000 wamesambazwa Tanzania Bara na Zanzibar kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya mitandao na kulinda amani ya wananchi.
Amesisitiza kuwa wazazi na walezi wanapaswa kuwaelimisha vijana kuheshimu sheria na kuepuka kushiriki vitendo vya uchochezi mtandaoni.
Soma pia: Askari wa jeshi la akiba (Mgambo)watakiwa kulinda amani kuelekea uchaguzi mkuu
Msemaji wa Jeshi hilo, DCP David Misime, amesema zaidi ya askari 4,000 wamesambazwa Tanzania Bara na Zanzibar kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya mitandao na kulinda amani ya wananchi.
Amesisitiza kuwa wazazi na walezi wanapaswa kuwaelimisha vijana kuheshimu sheria na kuepuka kushiriki vitendo vya uchochezi mtandaoni.
Soma pia: Askari wa jeshi la akiba (Mgambo)watakiwa kulinda amani kuelekea uchaguzi mkuu