Zaidi ya watu 90 waliokuwa wakichota mafuta kutoka kwenye lori la mafuta lilopinduka katika mji wa Molo nchini Kenya wamefariki kwa kuungua vibaya baada ya lori hilo la mafuta kulipuka.
Watu 50 kati yao waliungua vibaya mpaka kugeuka mkaa hali iliyofanya maiti zao kushindwa kutambulika.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana zilisema kuwa moto huo ulizuka baada ya mamia ya watu kukusanyika kukusanya mafuta ya petrol yaliyomwagika baada ya lori kupinduka katika mji wa Molo na lori hilo kulipuka.
Watu wengine kadhaa wamejeruhiwa vibaya na moto huo. Idadi ya vifo kutokana na moto inategemewa kuongezeka.
Sababu ya moto huo haijajulikana ingawa baadhi ya taarifa zinasema kuwa moto huo ulisababishwa na sigara huku taarifa zingine zikisema kuwa moto huo ulianzishwa makusudi na mtu aliyezuiliwa na polisi kwenda kuchota mafuta hayo.
"Watu walimiminika kwenda kukusanya petrol, baada ya hapo moto mkubwa ulizuka , inawezekana kuna mtu aliwasha sigara" alisema Titus Mung'ou msemaji wa Red Cross nchini Kenya.
Source: http://www.nifahamishe.com
Watu 50 kati yao waliungua vibaya mpaka kugeuka mkaa hali iliyofanya maiti zao kushindwa kutambulika.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana zilisema kuwa moto huo ulizuka baada ya mamia ya watu kukusanyika kukusanya mafuta ya petrol yaliyomwagika baada ya lori kupinduka katika mji wa Molo na lori hilo kulipuka.
Watu wengine kadhaa wamejeruhiwa vibaya na moto huo. Idadi ya vifo kutokana na moto inategemewa kuongezeka.
Sababu ya moto huo haijajulikana ingawa baadhi ya taarifa zinasema kuwa moto huo ulisababishwa na sigara huku taarifa zingine zikisema kuwa moto huo ulianzishwa makusudi na mtu aliyezuiliwa na polisi kwenda kuchota mafuta hayo.
"Watu walimiminika kwenda kukusanya petrol, baada ya hapo moto mkubwa ulizuka , inawezekana kuna mtu aliwasha sigara" alisema Titus Mung'ou msemaji wa Red Cross nchini Kenya.
Source: http://www.nifahamishe.com