Yusuph Manji mgombea udiwani wa CCM Mbagala!

Yusuph Manji mgombea udiwani wa CCM Mbagala!

Hii inadhihirisha bila hela hapa bongo ni mambo hayaendi

gollocko;
Hapana sio hapa bongo. Usiogope; sema ukiwa na hela ccm unaweza kuwa popote na kupewa cheo chochote hata kama hukitaki.
Wakati watu wanatoana mimacho kugombea fomu yeye watu wanamchukulia, kumjazia, na kukata tu picha kwenye gazeti, bandika, wasilisha chaguliwa. Hii kali ya uchaguzi mkuu.
Ila, yoote kuonesha jeuri ya ccm. Wala hakuna pingamizi pamoja na lalamiko la M/kiti mkoa. Dah! Yaani inatia huruma ati, Watz tunavyo nywea mtu akitikisa tu mkoba wake
 
Zile Tzs 700m alizorudishiwa Dodoma zilimwakilisha kwenye kura ya maoni.
 
gollocko;
Hapana sio hapa bongo. Usiogope; sema ukiwa na hela ccm unaweza kuwa popote na kupewa cheo chochote hata kama hukitaki.
Wakati watu wanatoana mimacho kugombea fomu yeye watu wanamchukulia, kumjazia, na kukata tu picha kwenye gazeti, bandika, wasilisha chaguliwa. Hii kali ya uchaguzi mkuu.
Ila, yoote kuonesha jeuri ya ccm. Wala hakuna pingamizi pamoja na lalamiko la M/kiti mkoa. Dah! Yaani inatia huruma ati, Watz tunavyo nywea mtu akitikisa tu mkoba wake

Hahahaaaaa mkuu umeua.
Picha wanakata kwenye gazeti?
 
Hivi ana nyumba huko au ni askari wa kukodi?

Duh amehama lin masaki

Kama Nape tu kule mtama wenyewe wanamwita 'majeshi ya UN'...teh...teh...teh!

Ana nyumba na alikuwa na maeneo ya Mbagala kuu mengine yalichukuliwa na serikali wakapima ardhi (sijui mbagala gani ila ukiwa Mbagala kuu unaeelekea kusini mbele kidogo ambapo kushoto inakuwa Mtoni kijichi alafu kwa mbele sana pamepimwa viwanja na pameunga na Kigamboni. (nadhani eneo limepakana na Mbagala mgeni nani ni maarufu kwa Manji alikuwa na maeneo mengi sana )
 
Sasa kwa nini amerejeshwa wakati ameonyesha jeuri ya hali ya juu ambayo imeweka hata rekodi ya dunia?

Hata huko Marekani akina milionea Donald Trump wanaonekana wakikukuruka kutaka kugombea uraisi, yeye amelala nyumbani kwake Seaview anachaguliwa kugombea udiwani Mbagala, kama si kuwanunua vigogo ni nini?

Au tuelezwe basi criteria zilizotumika kumrejeshea ugombea udiwani wakati hakutokea hata mara moja katika mchakato mzima wa kuanzia kuchukuwa fomu, kujitetea mpaka kupiga kura

Alikuwa anapiga kampeni kwenye simu, Aende Mbagala Kuu kufanyaje tena kuwasiliana na simu tu inatosha.
 
Ana nyumba na alikuwa na maeneo ya Mbagala kuu mengine yalichukuliwa na serikali wakapima ardhi (sijui mbagala gani ila ukiwa Mbagala kuu unaeelekea kusini mbele kidogo ambapo kushoto inakuwa Mtoni kijichi alafu kwa mbele sana pamepimwa viwanja na pameunga na Kigamboni. (nadhani eneo limepakana na Mbagala mgeni nani ni maarufu kwa Manji alikuwa na maeneo mengi sana )

Ana nyumba lakini hajawahi kukaa huko hata siku moja.. Hivi manji akae mbagala kuu kweli?
 
Mfanyabiashara Yusuph Manji ameteuliwa kugombea Udiwani kata ya Mbagala kwa tiketi ya CCM.

Manji ambaye awali alikatwa na mkoa amerejeshwa na kamati kuu. Hata hivyo m/kiti wa CCM Madabida amesema hakubaliani na uteuzi huo kwani Manji alivunja kanuni.

Chanzo: Tanzania Daima
CC wanajua madabida ni pandikizi la EL.... Madabida naye kuhama CCM ni shughuliu maana CCM hawakawii kumgeuzia kibao kwa ile kesi yake ya kuuza ARV feki.....kwa hapo naona mzee mzima inabidi afe na tai yake shingoni
 
Manji anaweza kuisimamisha KK ya ccm na kuiambia mguu pande mguu sawa, Julia geuka, mbele tembea na wakatii amri bila kuuliza maana huyo sio mfadhili wa chama tuu bali hata mjumbe mmoja mmoja
 
Ana nyumba na alikuwa na maeneo ya Mbagala kuu mengine yalichukuliwa na serikali wakapima ardhi (sijui mbagala gani ila ukiwa Mbagala kuu unaeelekea kusini mbele kidogo ambapo kushoto inakuwa Mtoni kijichi alafu kwa mbele sana pamepimwa viwanja na pameunga na Kigamboni. (nadhani eneo limepakana na Mbagala mgeni nani ni maarufu kwa Manji alikuwa na maeneo mengi sana )

Siyo Manji huyo mwenye maeneo hayo mzee ijapokuwa kunaitwa kwa Manji.
 
Ana nyumba lakini hajawahi kukaa huko hata siku moja.. Hivi manji akae mbagala kuu kweli?

Siyo Manji huyo mwenye maeneo hayo mzee ijapokuwa kunaitwa kwa Manji.

Ahsante kwa taarifa bitimkongwe, mie nilidhani ndo Manji huyo kumbe ni mwingine, LAKI si pesa nadhani jibu ni hana nyumba kama alivyosema jamaa hapo ila eneo lenyewe lipo well develop ndo maana nikadhani ni Manji yule, mie nilifika kule mara mbili kuna Makaburi mwanzoni ndo yanatenganisha Mbagala ya uswahili na kuingia hiyo Mbagala maarufu kwa Manji
 
Last edited by a moderator:
Hii nayo kubwa.Huenda Manji mwenyewe hata mbafala hapajui.Tanzania mbona Kama tupo kwenye sayari ya peke yetu?Aibu kubwa.
 
mimi iko punguza foleni,iko engeza mabasi ya kichina,iko jenga flyover na tayari kwisha agiza treni za mjini,iko panga eno kubwa ya machinga ktk jumba moja ya babu yangu tena bureeee! Iko harakisha ujenzi wa daraja la kigamboni.Iko badisha Dar zaidi ya Nairobi.Barabara che.Haste haste!!!!!!!!!
 
mimi iko punguza foleni,iko engeza mabasi ya kichina,iko jenga flyover na tayari kwisha agiza treni za mjini,iko panga eno kubwa ya machinga ktk jumba moja ya babu yangu tena bureeee! Iko harakisha ujenzi wa daraja la kigamboni.Iko badisha Dar zaidi ya Nairobi.Barabara che.Haste haste!!!!!!!!!

umetisha bro
 
Ana nyumba na alikuwa na maeneo ya Mbagala kuu mengine yalichukuliwa na serikali wakapima ardhi (sijui mbagala gani ila ukiwa Mbagala kuu unaeelekea kusini mbele kidogo ambapo kushoto inakuwa Mtoni kijichi alafu kwa mbele sana pamepimwa viwanja na pameunga na Kigamboni. (nadhani eneo limepakana na Mbagala mgeni nani ni maarufu kwa Manji alikuwa na maeneo mengi sana )

Manji yule alikuwa anafuga ngombe kule sio huyu wa Yanga na hata hiyo mfugaji alikuwa na mabanda ya mifugo na wachungaji tu.
 
Back
Top Bottom