Noti mpya tz
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 974
- 244
Mara ya mwisho Nilimsikia Prof. Mark Mwandosya aliporudi toka kutibiwa nje ya nchi baada ya hapo sijui yuko wapi, mwenye kujua please saidia mimi.
Nchi ya ajabu sana hii. Huyu ni waziri, analipwa mshahara na kutibiwa kwa kodi zetu lakini hali yake tunaambiwa ni siri yake na daktari wake. Inapaswa kuwa tofauti kwa viongozi. Tunayo kila sababu kujua maendeleo ya afya zao.
INASIKITISHA KWELI, WaZiRi lakin wengine hata tukawa hatujui hata habari zake mbali ya ugonjwa wake... Na mbona yeye hasikiki kama mwenzake Mwakyembe?
Utumishi wa Mwandosya (Waziri) hauhusiani na hiyo sheria. Hiyo sheria inahusu Civil servants na sisi walalahoi wengine kwenye Private sector. Mwandosya anaweza kuendelea na uwaziri hadi 2015 hata kama hatakanyaga ofisini hata siku moja ili mradi mamlaka iliyomteua itaona inafaa. Ipo haja ya kupunguziwa majukumu mengine hii mamlaka.Sheria za kazi zinatoa miezi mitatu ya kuugua kwa full mshahara then inafuata miezi mitatu ya mshahara nusu baada ya hapo anatakiwa kupumzishwa bila malipo hadi apone au aachishwe kazi under medical ground. Mwandosya hastahili kubakia waziri kwa vile afya yake ni mbovu na anatumia kodi zetu vibaya, ingawa tunamuonea huruma na kumuombea apone haraka.