Japhari Shabani (RIP)
R I P
- Jan 16, 2007
- 721
- 176
Mambo mengi yametokea na yanaendelea kutokea yenye uzito wa kitaifa na kuitikisa nchi,hatusikii kauli yoyote kutoka kwa Mh.Rais.Mfano mzuri yaliyotokea katika kampeni za uchaguzi vurugu,wizi wa kura na vurugu katika kuwapata mameya na viongozi wa halimashauri za wilay,migomo ya wanafunzi na walimu wa vyuo vikuuu-ambapo risasi za moto,mabomu ya kutoa machozi,maji ya kuwasha na virungu na ubabe wa vyombo vya dola- Imekua jambo la kawaida.Kubwa zaidi ni mauaji yaliyotokea Arusha na swala la malipo ya umeme kwa kampuni ya Dowans,maswala ambayo nafikiri kwa Mtanzania yeyote na asie Mtanzania ni mambo muhimu yaliyo na yanayoendelea kuitikisa nchi.Pamoja na yote hayo Rais Mh.JK kimya kana kwamba ni mambo ya kawaida.Na badala yake tunashuhudia kauli za viongozi wa ccm na serikali zikipingana.Hali hii inatupeleka pabaya kwani waswahili walisema "usipoziba ufa utajenga ukuta"MUNGU IBARIKI TANZANIA