Yuko wapi Hassan Juma mwanariadha wa Tanzania aliyeshiriki commonwealth games 1974?

Yuko wapi Hassan Juma mwanariadha wa Tanzania aliyeshiriki commonwealth games 1974?

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
19,295
Reaction score
39,977
Ninakereka sana na huu utamaduni wa nchi yetu kuandika historia huku taarifa nyingi sana zikifichwa. Kwa mfano historia ya muungano wetu huwa inaanza na kumaliza na majina mawili tu, Nyerere na Karume. Hata kwenye uhuru asilimia kubwa anatajwa Nyerere peke yake. Inasikitisha sana.

Leo nilikuwa natazama video za mchezo wa riadha huko You Tube mara ghafla nikaona Marathon ya mwaka 1974 jumuiya ya madola kuna jina Hassan Juma, mtanzania. Ingawa hakupata medali ila alimaliza mbio kwa muda wa masaa 2:38

Kama lisivyotajwa sana jina la Suleiman Nyambui ambaye alishiriki mbio za 1500m mwaka 1974 pamoja na Filbert Bayi ndo ilivyo kwa Hassan Juma. Nitoe wito kwa mamlaka zinazohusika kuandaa hata documentary ya kuonyesha tulipotoka na tunapoenda kwenye riadha. Yaani huu mchezo anayetajwa miaka yote ni Bayi tu kiasi kwamba kuna wanaodhani Bayi bado anakimbia. Angalau sasa hivi Simbu anatajwa.

Je, Mzee Hassan Juma yuko wapi? Kuna mwenye taarifa kumhusu?


View: https://youtu.be/4fwdXKXp2co?si=JLTL_j3GEVdmkmUY
 
Ninakereka sana na huu utamaduni wa nchi yetu kuandika historia huku taarifa nyingi sana zikifichwa. Kwa mfano historia ya muungano wetu huwa inaanza na kumaliza na majina mawili tu, Nyerere na Karume. Hata kwenye uhuru asilimia kubwa anatajwa Nyerere peke yake. Inasikitisha sana.

Leo nilikuwa natazama video za mchezo wa riadha huko You Tube mara ghafla nikaona Marathon ya mwaka 1974 jumuiya ya madola kuna jina Hassan Juma, mtanzania. Ingawa hakupata medali ila alimaliza mbio kwa muda wa masaa 2:38

Kama lisivyotajwa sana jina la Suleiman Nyambui ambaye alishiriki mbio za 1500m mwaka 1974 pamoja na Filbert Bayi ndo ilivyo kwa Hassan Juma. Nitoe wito kwa mamlaka zinazohusika kuandaa hata documentary ya kuonyesha tulipotoka na tunapoenda kwenye riadha. Yaani huu mchezo anayetajwa miaka yote ni Bayi tu kiasi kwamba kuna wanaodhani Bayi bado anakimbia. Angalau sasa hivi Simbu anatajwa.

Je, Mzee Hassan Juma yuko wapi? Kuna mwenye taarifa kumhusu?


View: https://youtu.be/4fwdXKXp2co?si=JLTL_j3GEVdmkmUY

Achana na huyo
Kuna huyu anaejulikana duniani kote japo alikuwa wa mwisho kwenye Marathon, anaitwa John Stephen Akhwari
Hii ilikuwa mwaka 1968, kwenye mashindano ya Oympic nchini Mexico
Alikuwa mwanariadha wa mashindano ya Marathon,
Siku ya mashindano hayo, wanariadha wanaanzia uwanjani na kupotelea mitaani, na wa kwanza kurudi ndio mshindi, sasa baada ya muda wale walioweza kuingia na kurudi uwanjani walishangiliwa na kupewa medali zao,
Kumbe mwenzetu alianguka na kuumia mguu, lakini alikuwa bado anaendelea kukimbia
Huku uwanjani washabiki wakishajua wote wanariadha wa marathon wamesharudi na ndio imetoka hio, huku wakiendelea kuburudika na michezo mingine.
Mara wanaona mtu anaingia uwanjani akikimbia kwa kuchechemea na haileweki ni mchezo anashiriki, haikupita dakika washabiki wakajua ni kati ya wale waliokuwa kwenye Marathon, basi uwanja mzima ulilipuka kwa shangwe na vigelele huku wote wakisimama na kupiga makofi huku mwamba akiingi akwa kuchechemea
Wazungu walichoka na majibu yake alipoulizwa kwanini hakuamua kuachia ngazi alipojua hataweza kushinda, akawajibu
"My country did not send me 5000 miles away just to start the race"


View: https://www.youtube.com/watch?v=tNC2r4MOb1w&t=2s

1766101064559.png
 
Achana na huyo
Kuna huyu anaejulikana duniani kote japo alikuwa wa mwisho kwenye Marathon, anaitwa John Stephen Akhwari
Hii ilikuwa mwaka 1968, kwenye mashindano ya Oympic nchini Mexico
Alikuwa mwanariadha wa mashindano ya Marathon,
Siku ya mashindano hayo, wanariadha wanaanzia uwanjani na kupotelea mitaani, na wa kwanza kurudi ndio mshindi, sasa baada ya muda wale walioweza kuingia na kurudi uwanjani walishangiliwa na kupewa medali zao,
Kumbe mwenzetu alianguka na kuumia mguu, lakini alikuwa bado anaendelea kukimbia
Huku uwanjani washabiki wakishajua wote wanariadha wa marathon wamesharudi na ndio imetoka hio, huku wakiendelea kuburudika na michezo mingine.
Mara wanaona mtu anaingia uwanjani akikimbia kwa kuchechemea na haileweki ni mchezo anashiriki, haikupita dakika washabiki wakajua ni kati ya wale waliokuwa kwenye Marathon, basi uwanja mzima ulilipuka kwa shangwe na vigelele huku wote wakisimama na kupiga makofi huku mwamba akiingi akwa kuchechemea
Wazungu walichoka na majibu yake alipoulizwa kwanini hakuamua kuachia ngazi alipojua hataweza kushinda, akawajibu
"My country did not send me 5000 miles away just to start the race"


View: https://www.youtube.com/watch?v=tNC2r4MOb1w&t=2s

View attachment 3517409

Huyu anaheshimika sana kwa wazungu
 
Udini umeanza
Ndio tatizo lenu wagalatia, mkiona majina waislamu yanatajwa kwenye nyanja fulani mnawashwawashwa kwa sababu milshaaminishwa tokea enzi ya yule mpuuzi nyerere kuwa waislamu hawana elimu na pia mlizoea kuona wenzenu kwenye kila wadhifa, ila sasa kila mkiona kuna majina ya waislamu hamtaki kuamini, mnaona haiwezekani
Haya sasa wakati ukuta, mtatoa kila aina ya milio, lakini vita mbele
Na vipi ukimbiwa safu yote ya majenerali wanaosubiri kuchukua nafasi ya CDF ni waislamu?

1. Rear Admiral Ameir Hassan - Mkuu wa Jeshi la Wanamaji (Naval Command)
2 Meja Jenerali Fadhili Omary Nondo - Mkuu wa Jeshi la Nchi Kavu (Land Forces)
3. Meja Jenerali Shabani Mani - Mkuu wa Majeshi ya Anga (Air Force)
4. Meja Jenerali Iddi Nkambi - Mkuu wa Majeshi ya Vikosi vya Chini ( Battalions)
5. Meja Jenerali Rajabu Mabele - Mkuu wa Majeshi ya Taifa (National Service)
 
Udini umeanza
Sidhani kama ni udini. Mleta mada ana hoja nzito. Mambo mengi ya nchi hii ni tofauti na inavyosimuliwa. Riadha ya Tanzania inaanza na Bayi na kuishia na Bayi kumbe kuna hadi kina Hassan Juma waliokuwa na kina Bayi hawatajwi popote.
 
Back
Top Bottom