Yu wapi IGP Mangu?

Camilo Cienfuegos

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2015
Posts
19,228
Reaction score
68,246
Ni muda mrefu umepita IGP Ernest Mangu hajaonekana hadharani wala kwenye media hasa ukizingatia katika vita ya madawa ya kulevya tungependa kusikia msimamo wake upoje.

Jana kwenye mkutano wa wakuu wa Majeshi ya Polisi kwa Nchi za Kusini mwa Afrika uliofanyika mjini Bagamoyo hakuwepo na badala yake aliwakilishwa na IGP Msaidizi Kaniki.

Ukimya wake unatutisha sisi wananchi hasa ukizingatia kwasasa tetesi ni nyingi kuhusu uhusiano wake na Kiranja.

Mwenye kujua atujuze alipo IGP Mangu.
 

Sio yeye tu, uliza wapi alipo Mama Samia, wapi Majaliwa?

Nchi iko na watu watatu tu kwa sasa JPM, Makonda na Sirro
 
Kila mtu na kazi yake, IGP sio msanii wa kuonekana kila siku. Madawa ya kulevya yana kitengo chake.
 


AKIONEKANA HADHARANI ILI IWEJE WAKATI AMEKWISHA TUMBULIWA? MUACHENI APANGIWE MAJUKUMU MENGINE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…