Your Ideas and knowledge please

OGOPASANA

JF-Expert Member
Apr 30, 2009
262
144
Habari,
Nina wazo la kufungua ofisi ya kukopesha fedha kwa riba ndogo na masharti nafuu, na kupokea fedha kutoka kwa watu na kurudisha kwa riba baada ya mda flani. Mfano: kwa kila TSH 10,000 nitakayopewa nitaweza kumrejeshea Tsh 13,000.00 kwa aliyenikopesha, na kwa kila Tsh 10,000.00 nitakayomkopesha mtu atanirudishia Tsh 12,000.00 baada ya mda fulani.. Je biashara kama hii ni halali kisheria?
 
Ni halali ila kwa vile unapata faida inatakiwa uregister kama financial institution. Tatizo kubwa ni wateja wako kulipa. Najua watatoa guarantee fulani, eg: kiwanja ila mwishowe unajikuta na viwanja 100, huna hela na huna mteja...
Mara nyingi biashara kama hiyo inaenda na business consulting ambayo ni compulsory kila mtu anae taka kukopa kwako apitie pale akapate ushahuri wa namna ya kufanya biashara ao ku-save ili wakulipe...
Good luck
 
Habari,
Nina wazo la kufungua ofisi ya kukopesha fedha kwa riba ndogo na masharti nafuu, na kupokea fedha kutoka kwa watu na kurudisha kwa riba baada ya mda flani. Mfano: kwa kila TSH 10,000 nitakayopewa nitaweza kumrejeshea Tsh 13,000.00 kwa aliyenikopesha, na kwa kila Tsh 10,000.00 nitakayomkopesha mtu atanirudishia Tsh 12,000.00 baada ya mda fulani.. Je biashara kama hii ni halali kisheria?

Ni halali kabisa ki nchi, kidini haswa kiislaam si halali. Si ndio wanavyofanya mabenki yote, nenda BOT wakakupe muongozo zaidi wa leseni yake.
 
kuna kampuni nyingi tu zinafanya hii biashara. hata huku kitaani kuna mapedeshee wengi tu hufanya biashara hii bila vibali. tatizo kubwa ni uaminifu wa hao watu hasa watu wa hali ya chini
 
Nashukuruni sana wakuu kwa mawazo na ujuzi wenu juu ya hili, i will let u know ntakapoanza, ofisi, vibali ntakavyopata, maendeleo na kuwakaribisha pia kukopa ama kuweka.

Mungu awabariki.
 
Back
Top Bottom