Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Aliyekuwa Kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Yericko Nyerere, amemshutumu vikali Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, akimtaja kuwa chanzo kikuu cha kuvurugika kwa mchakato wa maridhiano ya kisiasa nchini.
Akizungumza leo Agosti 06, 2025 jijini Dar es Salaam, mara baada ya kutangaza rasmi kujiunga na Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Yericko amesema kuwa hali ya maridhiano ilianza kubadilika mara tu Lissu alipopewa nafasi ya kushiriki vikao vya mazungumzo licha ya kutokuwa mjumbe rasmi.
"Aliyeua maridhiano ni Tundu Lissu, tutawaambia aliwauaje. Baada ya ombi la waliokuwa uhamishoni kurejea na mikutano ya siasa kufunguliwa, aliporudi tu, Mwenyekiti Freeman Mbowe alimwalika Lissu kwenye vikao vya maridhiano wakati hakuwa mjumbe. Alikiomba kikao kwa kusema: 'Ninamuomba kwa heshima aliyekuwa mgombea urais ashiriki maridhiano.'"
Akizungumza leo Agosti 06, 2025 jijini Dar es Salaam, mara baada ya kutangaza rasmi kujiunga na Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Yericko amesema kuwa hali ya maridhiano ilianza kubadilika mara tu Lissu alipopewa nafasi ya kushiriki vikao vya mazungumzo licha ya kutokuwa mjumbe rasmi.
"Aliyeua maridhiano ni Tundu Lissu, tutawaambia aliwauaje. Baada ya ombi la waliokuwa uhamishoni kurejea na mikutano ya siasa kufunguliwa, aliporudi tu, Mwenyekiti Freeman Mbowe alimwalika Lissu kwenye vikao vya maridhiano wakati hakuwa mjumbe. Alikiomba kikao kwa kusema: 'Ninamuomba kwa heshima aliyekuwa mgombea urais ashiriki maridhiano.'"