Yemenikuta Mwenzenu

Ni kweli aisee anaweza kuitumia TRA kumnasa huyo jamaa. Sijui kama alikumbuka kureport hilo tukio polisi?

Hilo ni tapeli lililo kubuhuu hata namba ya gari itakuwa ya ujanja ujanja pole sana dada yangu milima haikutani lakini hukutana ipo siku mtakutana tu
 
dah,asante kwa angalizo na pole kwa yaliyokukuta. me huwa nina tabia moja, sipendi kujuana juana. mwisho wa siku wanaanza kunambia kuwa najisikia,mara naringa lakin ukweli unabaki pale pale!
Ukiona mtu anakuzoeazoea bila mpango kwenye mambo ya kazi,mali,pesa kuwa makini naye
 
Pole sana hao huwa wanakulevya from the moment you answer their first question, inasemekana wanatumia uchawi wanakunuizia kwamba uwe poyoyo kwa kila takwa lake usikae hata kimoja na dawa husika wanaweka chini ya ulimi anapoongea anakuwa kama anarelease pepo linalocontrol akili yako na reasoning capacity. .. wengine anakuwa kama anapiga miayo sana au kukusogelea sana anapokuongelesha ili huo uchawi ufanye kazi ya kukuingia kirahisi.
Tuombe ulinzi wa Mungu kila asubuhi maana mbinu za kutudhuru, kutukwaza na kuturudisha nyuma zipo nyingi mno.
Ulipoanza stori nikadhani ni ishu ya jana mitaa hiyo ya quality centre mana kulikuwa na ujambazi walikuwa wanarusha risasi hovyo mpk nasikia walijibizana na kikosi cha ffu maeneo ya kiwanda cha Araf
 
Nilivyoliona jina tu nikajua kuna mawili kama hajakufisadi basi kakutapeli!!
Pole sana
 
Pole sana ....
Nimejifunza kuwa makini zaidi na kustuka unapokutana na mtu kwa mara ya kwanza na kuonyesha kukuhitaji kwa jambo fulani kwa haraka.
Nikiwa form 3. Nlitoka kwenda kununua shat la shule. Wakat narudi nikakutana na mtu anamuulizia mama Juma katikati ya mji. That was 15 years ago. Sikuelewa mtu anauliziaje jina la mama flan katikat ya mji wakat hapo sio makaz ya watu ni eneo lina gas stations na banks na kituo cha bus. Nikamwambia simjui. Akaanza maelezo kwamba katokea songea huyo mama Juma kazaa mtoto ana kichwa cha ajabu akamkimbia so wamekuja nae ili wamkabidhi mwanae kama nataka kumuona yuki sehen flan. Akaja baba meingine akasema labda tukamuulizie sehem flan. Mi niliondoka very fast. Nlikua sijasikia bado wizi wa hvy ila nlikua mwoga sana wa stranger na namjua mamangu akikukuta na watu unajichelewesha utaipata hata kama unawajua.

nikisikiaga story za hv nakumbuka hy incident. Ila kwa kua nlikua form 3 na sikua na hata change ya hilo shat. Labda wangenibaka. Mungu tu alinisave siku ile
 

Kama ulimpa mkono ndiyo pale alipomaliza kila kitu,
Yani daah.
Pole sana dada yangu,
Kesi hii pia iliwahi kumkuta ndugu yangu wa karibu miaka kadhaa iliyopita.
siku hizi hupaswi kumpa mtu mkono hata kidogo.
kwa sababu kuna mambo mawili:
Ile mikono tayari imepakwa vitu fulani ili pindi utakapopitisha tu puani ukanusa shughuli imeisha.
au wengine wana madawa ya kienyeji akikushika tu mkono lolote atakalokwambia hubishi.
 
Mimi kuna ndugu yangu alikumbana naye mmoja kariakoo....akapumbazwa mpaka akaja nae mpaka geto....nikiwa nimetulia geto ghafla naona mwenzangu anakuja na kuanza kupekua....ile sehemu anapowekaga akiba zake.....kwa bahati nzuri siku ile nilifanya mabadiliko fulani ya kimpangilio humo chumbani....lakini kwa uharaka aliokuwa nao katika kutafuta na ukali wake pindi umuulizapo ulinifanya niwe na mashaka kwani haikuwa kawaida yake....na vile vile nilikuwa na taarifa za wizi wa aina hiyo.....kutoka nje nikamkuta mshikaji katulia nje huku akingoja mzigo wake........aliponiona ghafla akaanza kunichangamkia utasema tunajuana siku nyingi......nikamuuliza kiukali kuwa amemtuma nini jamaa kule ndani.....?? Niliuliza kwa ukali sana hadi akaanza kutetemeka na kuanza kujaza watu....ndipo tukamuita yule jamaa aliyekuwa akitafuta hela ndani....naye ili kumtoa wenge tukamtia kofi kubwa na tukamuuliza kwa ukali kuw huyu jamaa amekutuma nini....???

Jamaa akaanza kujikanyaga kanyaga na ndipo alipoanza kupokea kichapo kikali....mwishowe ikabidi niingilie ili asije kuuwawa na nikampeleka polisi.....
 
Kheeeeee hawa watu bado wapo nakumbuka mnamo mwaka 2008 hawao jamaa walishawai kunitokea maeneo ya tandika mchangani
 
Pole sana mkuu na hongera kwa kukariri ata namba ya gari, kama haikua ya magumashi utampata huyo mtu.Hii issue yako imewahi kunitokea mm pia hawa watu wapo na ukiingia anga zao unakua huna ujanja hata kidogo huwa natamani tujue namna ya kuwaepuka mana ni kazi sana.
Mimi ilinitokea ubungo darajani kama unaenda buguruni wakati huo nasoma UDSM nakaa nje ya mabibo hostel na nakumbuka ilikua siku ya boom, nilikutana na mzee mmoja na bibi (Sio wazee sana) wamekaa kama wananisubili wakaniita jina langu kosa nililofanya ni kuwasikiliza. Baada ya hapo walianza kunambia mambo mengi sana cha ajabu nilikua nashindwa hata kuwapinga wanalosema nilikua nimetoka atm nna laki 1 na nusu nikawapa yote wakanambia haitoshi niwapeleke atm wakachukue nyingine nikaenda nao atm wakabeba pesa yote ya boom. Wakati wote hata nikutane na wanafunzi naowajua wakinisalimia sijibu naona wananipotezea muda.
Baada ya kutoa pesa zote kwenye atm, kipindi hicho nilifanikiwa kununua bodaboda mana nilikua najitegemea hivyo nikaona ili nipunguze mzigo home ninunue bodaboda niwe napata kidogo, kuna dereva nilimpa akawa ananiletea hela kwa week siku hiyo bodaboda ilikua mbovu cha ajabu wale wazee walikua wanajua kuhusu hiyo pikipiki wakanambia wanataka niwape na pikipiki nikawambia haina shida ipo home wakasema tuongozane, hapo hata simu nimeshawapa mwenyewe tena nimetoa line nikawapa simu.
Tulipokaribia kufika home wakasema wananisubili karibu na home mimi nikawaletee pikipiki sikua najua chochote zaidi ya kusema ndio, kwa bahati nzuri nimefika home baba mwenye nyumba akaanza kunisemesha kama dk 3 ivi baada ya kumalizana nae nikaingia ndani kutoa pikipiki niwapelekee, ghafla kama fahamu zikaanza kurudi nikawa najiuliza hii pikipiki naipeleka wapi? kucheki mfukoni sina simu,sina hela. Hapo nikajua tayari nimeibiwa sikua na jinsi tena kwenda kuwacheki wale wazee sijawakuta, nilijaribu kuwa napita pale ubungo kwa mguu karibu miezi miwili ila sikuwaona tena, nikakata tamaa.

HUU WIZI WA AINA HUU UPO KWELI NA NI VIGUMU SANA KUTOKA.
 
 
si mazingaombwe wala nini, huyo jamaa alikumalizia pale pale cjuw wapi vile, pik...hotel. mhudumu aliyewaletea kinywaji alikuwa tayari ameandaliwa na hicho kinywaji ulichokunywa ndo kilikuwa kimefanyiwa majambozi

Ni mawazo yangu tu lakini

pole kwa yaliyokukuta, next time kuwa mwangalifu na stranger yeyote
 
kwakweli MsaMee coz niseMeMu ya kazi yake na katiMuza waJiBu wake,,!
 
Kwa ufupi ni pafyum mtu anajipulizia halafu anameza vidonge ambavyo vitazuia isimdhuru yy ila ana uwezo wa kumdhuru mtu alie karibu yake ukivuta ile harufu ambayo we utaona ni marashi ya kawaida tu.kumbe unavuta sumu.
 
Halafu dada yangu next time ukiitwa na mtu usiye mfahaam toa taarifa kwa watu wako wa karibu na pia usiende peke ako tafuta board guard na uwe nae.
 
Kuepuka haya nilishaacha kitambo kutembea na aina yoyote inaitwa card. Nina ID ya chuo na kazini. Nilishaacha kusalimiana na watu nisiowajua hasa wale wanaonichangamkia bila sababu. Miaka ya nyumba sana huko kuna muhindi koko mmoja alinikosakosa kunipeleka gesti.
 
Kuna sehemu umeediti au umefowadi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…