Yawezekana Kukosa "Ubunifu" ndio tatizo letu kubwa?

Jibu ni kwamba Mwafrika ni mtoto wa Mzungu, maana yake ni kwamba Mzungu katulea, katufundisha kusema aeiou, katufundisha kusoma, kuandika kwa kifupi Mwafrika hawezi kufikiri nje ya kile Mzungu alichomwambia, na kila kitu ambacho tunakijua ni kile Mzungu alichotuambia, na haya ndiyo madhara ya kutawaliwa na ndiyo maana nchi ambazo hazikutawaliwa na Mzungu ziko mbali kimaendeleo kama Korea (zote mbili), Ujapani, Uchina, Taiwan!

Maadamu hatufanya reforms wakati tunapata Uhuru ktk kwa Mzungu basi hakuna kitu kitabadilika kwa maana hata tunachojifunza ni Mitaala ya Elimu yetu ni ya Mzungu, Mwanafunzi wa Kitanzania/Afrika anajua zaidi kuhusu Ulaya na USA klk anavyojua kuhusu Afrika!

Mwafrika ndiyo Binadamu pekee Dunia hii ambaye anatumia muda wake wote Shuleni kujifunza Lugha tu, hakuna mtu anayejifunza lugha kwa muda mrefu ukiondoa native speakers kama Mwafrika, kwa kifupi tunakwenda Shuleni kujifunza Lugha tu, Kiingereza/Kireno/Kifaransa au hata kihispani kutegemeana na Mkoloni wako, hivyo hakuna muda unaobaki kuwa wabunifu kwani tukishajua hizi lugha ndiyo kila kitu kimeisha!
Umeandika nonsense
 
Tatizo kubwa ni bado hatuja pata UHURU yaani kuna mfumo flani unatakiwa uufate ndio mtu/mtanzania afanikiwe.We hebu imagine yule sijui aliyekua Mku wa wilaya tena anaelimu ya dakta alivo pigwa tu chini na Magu ali lia lia as if sio msomi oor cjui nawategemezi cjui ntaishije msomi mzma je layman afanyaje xaxa ...Alaf kingine ikionekana tu raia wa kawaida anahoji tu kidogo ooh anapewa jna la UPINZANI du !!hivi kunawatu wanahati miliki kua mawazo ndio yako sahihi ya kujenga nnchi hii.Halafu vyombo vya usalama navyo cjui vinatumika pasipo kujua au ndio cjui kunabrunch za vyama humo?JAMANI kuna haja ya Katiba mpya maana hata type ya viongozi kama kibajaji ndio maana mkulu kama vile anatamani aongezewe idadi ya wabunge wakuteuliwa ili awaweke ma Dr na maProfeser wake kwenye baraza lamawaziri.
 
Hili ni tatizo kwamba kila kitu ukikisoma unakisoma kuwa kinamhusu Magufuli. Kinyume na fikra hizo Magufuli siyo mtu pekee Tanzania na Tanzania nzima siyo Magufuli. Nikirudia alichokisema Baba wa Taifa - Tanzania ya Watanzania na Watanzania ni wote! Unamfikiria sana Magufuli kiasi kwamba unashindwa kubuni kitu nje ya Magufuli.

Mzee mwanajiji na ww ni mpiga porojo fulani tu. Kama una ubunifu kipi kinakushinda kuuleta huo ubunifu wako ikawa msaada kwa watanzania wenzako? Nilitaraji ungeonyesha ubunifu waki kwa kuuweka hapa jukwaani au kuipa serekali iutumie kukwamua wananchi wake. Kinyume na hapo ni kwamba umetoa post hii ili watu wajue na ww bado upo.
 
Ubunifu ni moja ya mambo yanayotukwamisha mambo mengi. Na hata pale panapokuwa na wabunifu kunakosekana uthubutu na enthusiasm ya kufikia malengo. Wako wachache wetu ambao ni wabunifu, wamethubutu na kutimiza maono na mipango yao.

Hii inasababishwa na nini? Ni elimu, malezi na makuzi. Tunafundishwa kusilikiliza na kufuata tunavyoambiwa na mzazi, mwalimu, kiongozi wa dini etc. Mfano, wengi tumepitia tuition na "kusolve past papers" pengine kuanzia sekondari hadi chuo kikuu. Wachache walijisomea vitabu na kufaulu mitihani yao.

Huko mashuleni na vyuoni masomo kwa vitendo inaonekana ni anasa. Wanafunzi wanalia maabara hazina vifaa, wengine wanalia hawajapewa na serikali pesa za kujikimu kuwawezesha kuhudhuria mafunzo kwa vitendo.

Its high time serikali ifumue mfumo wa elimu na kuusuka upya, sustainably. Sio kila Rais au Waziri mpya anakuja na mfumo wake wa elimu. Hakuna anayefanya needs assessment, na hata ikifanywa it is not deep and detailed kuonyesha gaps na kung'amua areas of improvement kuhakikisha vijana wanapewa nafasi ya kuthubutu kubuni na kuwawezesha kuwekeza kwenye ubunifu huo. Kwa kweli hatupendi kujifunza vitu vipya, hatupendi challenges tutakuaje wabunifu?

Understanding is a weakness and we are "so understanding".
 
Chakula cha Mawazo: Unafikiri ni kwa kiasi gani ubunifu (creativity) una nafasi katika kubadilisha maisha mtu, kikundi cha watu, jamii au hata taifa kwa ujumla. Unafikiri Watanzania kama mtu mmoja mmoja na kwa ujumla wao ni wabunifu katika kushughulikia matatizo na changamoto mbalimbali zinazokabili maisha yao?

Kwamba, kama kitu hakikufundishwa darasani, au hatujaona watu wengine (hasa wa nchi zilizoendelea) hawajakifanya basi sisi hatuna namna ya kukifanya au hata kukifanya vizuri zaidi? Kwamba, bado tunashughulikia matatizo mengi kwa mbinu zile zile za miaka zaidi ya hamsini nyuma?

Ni kwanini inaonekana hata tunapojaribu kubuni masuluhisho ya mambo fulani bado tunafikiri kwa namna ya wastani mno?
WALIMA MPUNGA:Miaka ya nyuma maeneo yanayolima mpunga kwa wingi palikuwa na ndege inakuja kupuliza dawa kwa ajili ya ndege waharibifu.Baadae huduma ikaondolewa na ikabidi wananchi wapambane wenyewe.Ubunifu uliofanyika ni kutumia video na audio tapes kuzifunga shambani.Zikipigwa na upepo zinatoa mlio ambao unafanya quelea quelea wasitue.VIPI HAPO MKJJ?
 
Porojo za mpaka kufunga na kusali siku arobaini ili Magu awe rais huku ukijinasibu kuwa sasa gari limepata dereva. Leo yamekuwa matusi kwetu watanzania kuwa tumekosa ubunifu???

Kwa taarifa yako ukiwa chuo kikuu, ukawa mbunifu halafu ukawa UKAWA ukimaliza chuo mshukuru Mungu. Shetani wa nchi hii ni CCM na usifikiri ubunifu hutokea ghafla kama ilivyokuwa manna kwa waisrael kule Jangwani, huandaliwa hasa hasa na serikali (unayoipigia debe).

Watu kukosa ubunifu kunatokana na serikali kukosa ubunifu. Ubunifu pekee tulionao ni namna ya kuzuia mabomu ya machozi Polisi wakitupiga

Hivi hukumsikia Mdude Nyagali alivyopelekwa chumba cha mateso na kuvuliwa nguo zote halafu korodani zake kuvutwa mbele ya akina mama?? Tena jengo lina rangi za bendera ya taifa???

Mdude Nyagali kwa sasa ni mbunifu wa namna gani atalipa kisasi kwani imeandikwa jino kwa jino

Hapa penyewe naonesha ubunifu wangu wa kuandika huku nikitegemea 'kutekwa kibunifu' na 'kupotezwa kibunifu' kama rafiki yangu Ben Saanane (ambaye Majaliwa alisema apumzike kwa Amani kwa maskio yangu mabunifu)
 
Nimesoma mada na kurudia mara kadhaa, nilichokielewa 'Ubunifu' anaoongelea MMM ni kufanya mambo kwa njia tofauti na zile zilizozoeleka. Ni kufanya mambo kwa mtazamo mpya na tofauti

Hapa haongelei uvumbuzi, anazungumzia ni jinsi gani tunaweza kufanya mambo kwa namna tofauti ili tupate matokeo tofauti na kwa njia tofauti zenye tija!

Ni ukweli kuwa hakuna ubunifu katika mazingira yasiyosaidia ubunifu.
Na wala hakuna ubunifu ukitumia mbinu zile zile kwa lugha tofauti. Huo si ubunifu ni Insanity

Mag3 kazungumzia hoja ya mfumo ambayo tumeizungumzia sana ingawa haieleweki sana
Katika mfumo uliopo hatuwezi kuwa na ubunifu kwasababu ubunifu unahitaji utulivu

Mfumo wetu hautoi nafasi ya ubunifu wa kutosha, ni kweli tunahitaji kubadili lakini si kubadili sura, tunatakiwa tukae pamoja tufume kitu kitakachotuweka pamoja na kutupa nafasi za kufikiri

Leo tunawezaje kuwa wabunifu ikiwa haturuhusiwi kuzungumza, kutoa maoni, kutokubaliana n.k.?
Tunawezaje kuwa wabunifu kama hatutaki kusikia wenzetu wanabuni nini na tuboreshe vipi kwetu?

Tuanze na ubunifu mkubwa sana wa kujenga nidhamu ya kweli katika utaratibu wa kweli na haki
Utaratibu utakoheshimiwa na kila mmoja yaani katiba yetu itakayotujengea nidhamu ya kweli

Nidhamu ya kweli ni utaratibu unaoheshimiwa na kila mmoja, si utaratibu unaowekwa na mtu
Utaratibu unaopandikizwa si nidhamu ni woga, na woga ni sumu namba moja ya ubunifu

Kwasababu ya woga na si nidhamu ndiyo maana hawataki kusikia 'ubunifu' kwingine.

Woga unawaongoza katika ubunifu wa kufunga sauti za wabunifu wengine , na hapo hatutakuwa na ubunifu asilani kwasababu tutakuwa na ubunifu wa 'kuviziana' si ubunifu mwingine wowote

Bila kufumua mfumo uliopo usiotoa ubunifu, hakuna ubunifu hata kama tutakesha tunalia
 
Ubunifu ni matunda ya uhuru, ukipanda uhuru utavuna ubunifu. Ukipanda udikteta utavuna utaahira...ni kama kumkata mtoto miguu halafu unamtegemea huyo mtoto kuwa bingwa wa mbio za Olimpiki akikua, huo ni utaahira. Anachofanya Magufuli kwa sasa ni sawa na kuwekeza katika utaahira na ndio maana mataahira kama Bashite ndio wamekuwa mifano ya kuigwa.
 
Chakula cha Mawazo: Unafikiri ni kwa kiasi gani ubunifu (creativity) una nafasi katika kubadilisha maisha mtu, kikundi cha watu, jamii au hata taifa kwa ujumla. Unafikiri Watanzania kama mtu mmoja mmoja na kwa ujumla wao ni wabunifu katika kushughulikia matatizo na changamoto mbalimbali zinazokabili maisha yao?

Kwamba, kama kitu hakikufundishwa darasani, au hatujaona watu wengine (hasa wa nchi zilizoendelea) hawajakifanya basi sisi hatuna namna ya kukifanya au hata kukifanya vizuri zaidi? Kwamba, bado tunashughulikia matatizo mengi kwa mbinu zile zile za miaka zaidi ya hamsini nyuma?

Ni kwanini inaonekana hata tunapojaribu kubuni masuluhisho ya mambo fulani bado tunafikiri kwa namna ya wastani mno?
yaani.. miaka saba baadaye
 
Back
Top Bottom