ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,758
- 9,589
Habari marafiki zangu
Natumai mko fiti na mnaendelea na shughuli,kazi na masomo yenu vyema
Leo nimeonelea nizungumze nanyi akina dada/wanawake wa humu mjengoni
kuhusu masuala yetu wanawake.
Moyoni mwangu niliwaza na kufikiri kuwa tuanzishe kitu ambacho kitatupa
umoja/ushirikiano/uhusiano wa karibu yetu na vilevile hata kutembeleana
kama itawezekana kwa wale walioko mkoa kwa mkoa,
na kupeana mambo ya baraka au huzuni pia kwani ziko ndani ya maisha
yetu ya kila siku. Kitu ambacho ningependa kuwashirikisha hususani
wanawake wenzangu, tuwe na jukwaa la akina mama au wanawake wa
jf. Mnaonaje tumshauri huyu Founder wetu atuwekee jukwaa hilo lihusulo
wanawake kama atapenda, jamani marafiki hili ni wazo langu tu ambalo
nimependa kuwashirikisha.
Hilo jukwaa tutakuwa tunazungumzia mambo mbalimbali yanayotuzunguka
yanayotupata, na vilevile tutajadili ni jinsi gani twaweza kuwasaidia wanawake
wa kitanzania katika matatizo/ misukosuko inayowakumba wanawake wenzetu
na vilevile tutajadili namna ya kumkomboa mwanamke aliyekandamizwa na
unyanyasaji toka upande wa pili. (Mfumo dume), kumpatia fursa ya kujikwamua
na kujinasua toka katika makucha hayo hususani wanawake waishio vijijini hasa.
Kitu kingine tutajadili na kupeana taratibu mbalimbali katika mambo yatuzungukayo
kama wanawake, hasa mambo mbalimbali kama ukiwa na shughuli yako unaweza
kutualika nasi tukajumuika nawe kufurahia hiyo shughuli yenyewe. mfano: ngoma,
kitcheni party, sendoff, tafrija fupi, mambo yahusuyo watoto wetu n.k. Hapo ndipo
tunafahamiana na kuleta ushirikiano na mahusiano mazuri katika yetu. Hili ni wazo
tu sijui kama wanawake wa humu mjengoni jf mtalifurahia na kulipenda na kulifanyia
kazi kama mko tayari basi msisite kufanya maamuzi na kutoa michango, ushauri na
jinsi gani twaweza kufanya haya yote kusaidiana na kuendelezana katika kuleta
maendeleo kwa mwanamke. Kama mtakuwa tayari tutawandaa viongozi wa kuongoza
kitu hichi na kuleta motisha katika majukwaa mengine. Ushauri tafadhali.
Kama mwanamke/ mdada wa jf utapenda kushirikiana nami katika hoja/wazo hili
basi usisite kuandika ushauri, kutoa maoni yako tufanyeje ili kuanzisha kitu hiki nami
nitamwomba Founder wetu, afuatilie na kulifanyia kazi kama atapenda naye.
Maoni/Ushauri wako mdada utafanya tuwe na jukwaa hili hapa jf. Naomba tuepuke
mizaha na maneno yasiyopendeza kwani hii wazo tu binafsi ambalo nimependa
kuwashirikisha nanyi kama mnapenda toeni maoni yenu hapa. TUFANYEJE KWA
JAMBO HILI (hata wewe mwanaume wa jf unaweza kutushauri ukipenda)
Copy: charminglady, sweetlady, Mamndenyi, snowhite, Paloma, Passion Lady, Zion Daughter
gfsonwin, Sean, Madame B, madame X, Preta, CUTE, na wanawake wengine waliopo
hapa jf mmu wote kwa ujumla wengine sijawashika majina yao mtanisamehe bure wapendwa.
Natumai mko fiti na mnaendelea na shughuli,kazi na masomo yenu vyema
Leo nimeonelea nizungumze nanyi akina dada/wanawake wa humu mjengoni
kuhusu masuala yetu wanawake.
Moyoni mwangu niliwaza na kufikiri kuwa tuanzishe kitu ambacho kitatupa
umoja/ushirikiano/uhusiano wa karibu yetu na vilevile hata kutembeleana
kama itawezekana kwa wale walioko mkoa kwa mkoa,
na kupeana mambo ya baraka au huzuni pia kwani ziko ndani ya maisha
yetu ya kila siku. Kitu ambacho ningependa kuwashirikisha hususani
wanawake wenzangu, tuwe na jukwaa la akina mama au wanawake wa
jf. Mnaonaje tumshauri huyu Founder wetu atuwekee jukwaa hilo lihusulo
wanawake kama atapenda, jamani marafiki hili ni wazo langu tu ambalo
nimependa kuwashirikisha.
Hilo jukwaa tutakuwa tunazungumzia mambo mbalimbali yanayotuzunguka
yanayotupata, na vilevile tutajadili ni jinsi gani twaweza kuwasaidia wanawake
wa kitanzania katika matatizo/ misukosuko inayowakumba wanawake wenzetu
na vilevile tutajadili namna ya kumkomboa mwanamke aliyekandamizwa na
unyanyasaji toka upande wa pili. (Mfumo dume), kumpatia fursa ya kujikwamua
na kujinasua toka katika makucha hayo hususani wanawake waishio vijijini hasa.
Kitu kingine tutajadili na kupeana taratibu mbalimbali katika mambo yatuzungukayo
kama wanawake, hasa mambo mbalimbali kama ukiwa na shughuli yako unaweza
kutualika nasi tukajumuika nawe kufurahia hiyo shughuli yenyewe. mfano: ngoma,
kitcheni party, sendoff, tafrija fupi, mambo yahusuyo watoto wetu n.k. Hapo ndipo
tunafahamiana na kuleta ushirikiano na mahusiano mazuri katika yetu. Hili ni wazo
tu sijui kama wanawake wa humu mjengoni jf mtalifurahia na kulipenda na kulifanyia
kazi kama mko tayari basi msisite kufanya maamuzi na kutoa michango, ushauri na
jinsi gani twaweza kufanya haya yote kusaidiana na kuendelezana katika kuleta
maendeleo kwa mwanamke. Kama mtakuwa tayari tutawandaa viongozi wa kuongoza
kitu hichi na kuleta motisha katika majukwaa mengine. Ushauri tafadhali.
Kama mwanamke/ mdada wa jf utapenda kushirikiana nami katika hoja/wazo hili
basi usisite kuandika ushauri, kutoa maoni yako tufanyeje ili kuanzisha kitu hiki nami
nitamwomba Founder wetu, afuatilie na kulifanyia kazi kama atapenda naye.
Maoni/Ushauri wako mdada utafanya tuwe na jukwaa hili hapa jf. Naomba tuepuke
mizaha na maneno yasiyopendeza kwani hii wazo tu binafsi ambalo nimependa
kuwashirikisha nanyi kama mnapenda toeni maoni yenu hapa. TUFANYEJE KWA
JAMBO HILI (hata wewe mwanaume wa jf unaweza kutushauri ukipenda)
Copy: charminglady, sweetlady, Mamndenyi, snowhite, Paloma, Passion Lady, Zion Daughter
gfsonwin, Sean, Madame B, madame X, Preta, CUTE, na wanawake wengine waliopo
hapa jf mmu wote kwa ujumla wengine sijawashika majina yao mtanisamehe bure wapendwa.
Last edited by a moderator: